Professional Okwi asaini 2yrs,amshukuru tajiri Mo Dewji

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Aug 24, 2011
49,199
103,733
Mganda Okwi mwenye umri wa miaka 26 amesani Simba SC kandarasi ya miaka miwili jana, taarifa zinadokeza hivyo.

Okwi ambaye yupo kwenye kikosi cha kwanza timu ya Taifa ya Uganda kama mshambuliaji, amemshukuru Mohamed Dewji kwa kusimama kidete kuhakikisha anafanikisha dili hilo.

Okwi amewaahidi mashabiki wa Simba kuwa wasubiri kazi nzito toka kwake, na amewashukuru kwa kumuamini
 
Wewe unajua ana miaka mingapi ?

Ivi Okwi ni mkubwa kuliko Kamusoko?
au Yondani au Zulu Mkataumeme au Kanavaro au Bissou, au Tambwe ?

Okwi kaoa mwaka juzi tu na ndoa yake ilionekana kwa wapenda soka wote

Lete umri wao na wake tuone nani mkubwa zaidi.
Kuoa ni kipimo cha umri?
 
Vibibi vizee vya Kariakoo...Miaka10 ..Yanga bingwa mara 7..anzisheni NGO (Mikia Foundation) inachosha kila siku sisi mabingwa...Canavaro kunyanyua kwapa amechoka
 
Mganda Okwi mwenye umri wa miaka 26 amesani Simba SC kandarasi ya miaka miwili jana, taarifa zinadokeza hivyo.

Okwi ambaye yupo kwenye kikosi cha kwanza timu ya Taifa ya Uganda kama mshambuliaji, amemshukuru Mohamed Dewji kwa kusimama kidete kuhakikisha anafanikisha dili hilo.

Okwi amewaahidi mashabiki wa Simba kuwa wasubiri kazi nzito toka kwake, na amewashukuru kwa kumuamini
Hili ndo jibu la rufaa ya Simba toka FIFA? Wabongo bwana rahisi kuwanyamazisha kama mtoto mdogo kwa pipi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom