Tunahitaji kumuajiri housemaid nyumbani kwetu ambako mimi na mke wangu tunao watoto wawili tu, na msichana wa kazi mmoja.
Lengo kuu la professional housemaid ni kuongea na kuwafundisha watoto lugha ya kiingereza pindi watokapo nursery school. Housemaid atasaidia kazi nyingine za kulea watoto na kazi nyingine kaka atakavyopangiwa na mwajiri wake.
Mdada huyu awe na sifa zifuatazo;
Awe msichana mwenye umri kati ya 25 na 30
Awe anajua na kuongea kiingereza vizuri
Awe na cheti cha form 4
Awe tayari kutumia kiingereza muda wote akiwa kazini
Remunerations
Mshahara ni Tshs. 120,000 kwa mwezi, pamoja na likizo ya mwezi moja yenye malipo.
Hongera sana Kagosaki! Jamani kazi kwenu, wenye ndugu msaidieni Kagosaki apate mdada wa kazi mwenye kuongea kimombo vizuri ili asiwapotoshe watoto wake.