Profesa Sospeter Muhongo Tazama ulivyochemka

Hivi sana wanasingizia miundombinu mibovu! Nipo njiani kuelekea Mahenge Ulanga, ngoja nikajionee!

Mkuu Mahenge na Ulanga ni maeneo mawili tofauti wewe unaelekea wapi hasa?
 
umeme ukikatika kidogo tu UNALALAMIKA.... kwani Prof. Muhongo ni Mungu..? Maintenance in many areas may need electrical power cut-off for sometime....

Unalalamikaaa utafikiri U LACK OXYGEN.... jifunze kufikiri na acha kulalama...

 
Prof Muhongo has lost a staunch supporter of his. He has lost me. He hasn't delivered on any one of his promises including that of involving the public in gas & oil contracts review
 
Prof. Muhongo alikuja na gia kali kwenye hiyo wizara kama Tibaijuka nae alivyoingia pale wizara ya Ardhi na wote sasa wamelowa kama bata aliyenyeshewa mvua; chezea mkweree na mafia yake wewe!! Siku hizi mkweree hamuachi Muhongo kwenye ziara zake , ona alikwenda nae marekani, Canada [ kule akakutanishwa na Barrick ] na juzi Oman walikosaini mikataba mingi hata hawajui ni ya nini kwani muda wote walikuwa wanashangalia dali ya dhahabu!! Zote hizo zikiwa ni mbinu za kupunguza kasi yake!!
 
Wanachotaka wananchi ni umeme wa uhakika wakati wote na siyo maneno ya kisiasa yasiyokuwa na mshiko. Ni muhimu Wizara ikaweka mikakati endelevu ya kuondokana na tatizo la umeme kuliko kudanganya.
 
Mtu anaitwa Muongo then unategemea nini toka kwake? Nimekereka sana na hiyo kauli yake, toka asubuhi ya saa 12 huku hakuna umeme.
 
waongo hawa.. Wakishasoma wakielimika basi wanafikiri watanzania wote hawana elim
 
Mgao hakuna ila umeme unakatikakatika! Profesa Muhongo kawa muongo!
 

Muhongo=Muongo
 
Ubaya wa hapa JF huwezi jua aliyeanzisha uzi ni nani na anamwangalia vipi anayemtuhumu. inawezekana kabisa aliyeanzisha uzi huu ni mwathilika wa juhudi za prof za kuondoa mgao wa umeme, anafanya juhudi kumvunja moyo ili dili lake liendelee...
 
ccm hawakosi la kusingizia kila kitu kina sababu na mchawi wake yupo. umeme- miundombinu, uchumi- mataifa ya nje, vurugu- chadema, etc. kumbe wao ndio waanzilishi wa haya yote udini, ahadi hewa, etc
 

magamba wataamini na wataendelea kuamini lakini watu wenye uelewa wao hawataamini milele hadi tutakapo ona power station ambazo ni cheap zinajengwa.
 
Ubaya wa hapa JF huwezi jua aliyeanzisha uzi ni nani na anamwangalia vipi anayemtuhumu. inawezekana kabisa aliyeanzisha uzi huu ni mwathilika wa juhudi za prof za kuondoa mgao wa umeme, anafanya juhudi kumvunja moyo ili dili lake liendelee...

inawezekana.
 

Kama kweli Waziri wa Nishati na Madini Mh Prof. Sospeter anamaanisha hicho anachokisema basi Tanesco waanzishe utaratibu wa fidia kwa usumbufu na uharibifu unaotokana na kukatika katika kwa umeme, hapo tutaamini hicho anachosema. Mfano vyakula nilivyoweka kwenye fridge na freezer vimeharibika inabidi nitupe, wiki mbili zilizopita radio na TV viliungua, je Tanesco wako tayari kunilipa? vinginevyo ni upuuzi mtupu kusema hakutakuwa na mgao.

 
Ubaya wa hapa JF huwezi jua aliyeanzisha uzi ni nani na anamwangalia vipi anayemtuhumu. inawezekana kabisa aliyeanzisha uzi huu ni mwathilika wa juhudi za prof za kuondoa mgao wa umeme, anafanya juhudi kumvunja moyo ili dili lake liendelee...

Mimi ndo mleta uzi huu, katika watu nawaamini ndani ya baraza jipya huyu jamaa nime na namkubali sana, kwanza shule yake ndefu, amefanya shughuli nyingi za kimataifa, ni kichwa, ila, cha kushangaza anasema hakutakuwa na mgao wakati eneo nilipo sasa kuna mgao. Hali hii sio ya matengenezo ya kawaida, mie mwenyewe pande za umeme nimepitia mbona, ila kwa matengenezo ya kawaida hapa imepita, ni kero. Na kama wajumbe wanavyoripoti, sehemu mbalimbali pana matatizo ya kukatika kwa umeme kwa muda mrefu... Haya, kwa hapa Korogwe, anamaliza kusoma magazeti tu, umeme umekatika, wakati hayo magazeti yameeleza ahadi ya Huyo jamaa kuwa katu, hakutatokea mgao hapa Tanzania, Nimueleweje?
 
umeme ukikatika kidogo tu UNALALAMIKA.... kwani Prof. Muhongo ni Mungu..? Maintenance in many areas may need electrical power cut-off for sometime....

Unalalamikaaa utafikiri U LACK OXYGEN.... jifunze kufikiri na acha kulalama...

Inategemea na hicho ninacholalamikia. Hata mtoto wa miaka 6 pia angelalamika, hili halihitaji degree 4 wala 6. Elimu ya mtaani tu yatosha. We mtu gazeti linasomwa kuwa katu hakutakuwa na mgao wa umeme Tanzania hii, dakika mbili umeme unakatika na hii noi kawaida katika eneo hili. we unasema napenda kulalamika, au na wewe ni mwenzao nini? N.y.a.m.b.a.f.fffffuuuuu
 

Kama mida hiyo ulikuwa korogwe na umeme ukakatika basi Mbeya pia umeme ulikatika kuanzia saa 12:45 asubuhi hadi saa mbili. na kwamba kwa muda wa siku kumi sasa kumekuwa na katizo la umeme si chini ya masaa mawili kila siku aidha saa moja asubuhi; saa saba au saa kumi na moja jioni.
HISIA ZANGU NI KWAMBA TZ KUNA MGAO TENA MKALI KULIKO MIGAO ILOTANGULIA ISIPOKUWA HAWA JAMAA WAMEBADILI NAMNA YA KUKATA UMEME!!
 
Wakati wa Ngeleja mgao ilikuwa unatangazwa, sasa hivi wakati wa Prof Muhongo mgao hautangazwi, hiyo ndio tafauti kubwa
 
Binafsi sina nia mbaya na prof. Muhongo. Tatizo lake ni kwamba alituaminisha watanzania kuwa hakutakuwa na mgao kamwe, maana ule uliokuwepo ulikuwa wa kupangwa. Bw Zitto aliposema kuwa mgao haukwepeki watu wakamsakama, kuwa anawatetea kina Mhando, Sasa watanzania hebu tuwe wakweli, kati ya Prof. Muhongo na Zitto nani aliwaambia watanzania ukweli??? ingawa tatizo sio Muhongo ila ni ccm, bado Muhongo anatakiwa arudi tena atuambie watanzania, huu mgao unaoendelea kwa sasa ameutengeneza nani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…