Hayo ni maneno ya mchungaji alipopewa kutoa neno la shukrani katika maeneo ya makaburini ambapo mke wake alikuwa anazikwa. Mchungaji huyu aliyesifika kwa kusimamia sheria kali za dini na imani ya madhehebu ya dini ya Zoari alitamka hayo maneno kiufasaha kama vile mzungu kutoka Uingereza anavotamka, wakati huo machozi yakimlenga lenga.