Preview SABABU 7 ZA KWA NINI KILA MWANAUME ANAHITAJI MWANAMKE SAHIHI KAMA MKEWE WA NDOA:

Said S Yande

JF-Expert Member
Mar 16, 2013
874
637
SABABU 7 ZA KWA NINI KILA MWANAUME ANAHITAJI MWANAMKE SAHIHI KAMA MKEWE WA NDOA:

Kwangu kipindi ambacho kilinivutia sana ni kipindi cha kampeni za uchaguzi nchini Marekani.

Ni pale Obama akiwa katika kampeni kwenye moja ya majimbo kugombea duru ya pili ya uraisi aliposimamisha hotuba yake na kutambua uwepo wa mkewe Michelle.

Obama alisema, “Mke wangu amekuwa bega kwa bega na mimi tokea niko chuo, kuna kipindi nilishindwa kulipa ada ila yeye ndiye aliyenilipia”

Obama akaenda mbali zaidi na kukiri mbele ya jamii ya kimataifa kwamba asingekuwepo hapo alipo kama sio mke wake Michelle.

Hivyo basi, nashauri kwamba mwanamke ambae mwanaume atakua nae huenda akawa chachu ya mafanikio na baraka kwake au anaweza akamrudisha nyuma kabisa katika mipango yake.

Sababu kuu 7 za kwanini iwe isiwe mwanaume lazima upate mwanamke alie sahihi.

1. Kila mwanamke anao uwezo wa kukuridhisha kimapenzi ila mwanamke sahihi na bora pekee ndiye anaeweza kuku-challenge kiakili na kuwa ‘intellectually inspired’.

2. Mwanamke yeyote anaweza kukuteka kihisia, ila yule sahihi pekee ndiye mwenye uwezo wa kukuteka kiroho na ukamtumikia Mungu wako.

3. Mwanamke yeyote anaweza akakushawishi muandike mpango wa harusi (wedding plan), ila mwanamke sahihi peke yake ndie mwenye uwezo wa kukuandikia na kukushauri mpango wa biashara (business plan)

4. Kila mwanamke anaweza akakubusu tena ‘French kiss’ ila mwanamke bora pekee ndiye mwenye uwezo wa kukutamkia maneno yaliyojaa busara na hekima.

5. Kila mwanamke anaweza akakupenda sana tu tena kama una pesa, ila mwanamke aliye bora pekee ndiye anaeweza kusimama na wewe hata kukuinua pale utakapokuwa huna kitu.

6. Mwanamke yeyote anao uwezo wa kukushibisha kwa kukupikia chakula kitamu, ila mwanamke bora pekee ndiye mwenye uwezo wa kukulisha chakula cha ubongo.

7. Kila mwanamke anao uwezo wa kukushawishi chumbani ila mwanamke bora pekee ndiye mwenye uwezo wa kukushawishi umrudie Mungu wako na ukumbuke wema wake maishani mwako.

Mwisho ngoja nihitimishe kwa kusema hivi ukisoma vitabu vya kihistoria kuhusu Winstom Churchhill mpaka Abraham Lincoln, na kutoka kwa Nelson Mandela mpaka kwa Martin Luther King Jr lao moja kwamba “No matter how strong a Man is, he is only as strong as the Woman he marries” Kwa tafsiri yangu ya kuunga unga isiyo sahihi sana Wanamaanisha “haijalishi ni kwa kiasi gani mwanaume una nguvu, nguvu zako zina athiriwa kwa kiasi kikubwa na mwanamke uliemuoa”.
Karibuni kwa mafundisho zaidi bila kusahau usiache kufanyia kazi kwa vitendo.
 

Attachments

  • FB_IMG_1552451266278.jpg
    FB_IMG_1552451266278.jpg
    45.9 KB · Views: 23
Back
Top Bottom