Pressure inanifelisha maisha

Pressure inanifelisha maisha

dracular

JF-Expert Member
Joined
Dec 24, 2013
Posts
769
Reaction score
1,073
Habari za asubuhi ndugu zangu wa jf,

Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 31na mwenye urefu wa cm172 na uzito wa kg 66. Mwaka jana nlikuwa kwenye masailiano ambayo yanahitaji mtu apimwe afya yake.. nilikuwa safi kwa magonjwa yote isipokuwa waligundua pressure yangu ipo juu.

Vipimo vilikuwa vinasoma mpaka 172/105 hivyo ikapelekea mimi kukosa fursa hiyo. Niliporudi home nilijitafakari sana na kuanza kuchukua tahadhari za kupambana na ugonjwa huo kwanza nikaenda hospital kupima na majibu yakasomeka 130/80 na daktari yule akaniambia sina tatizo lolote la pressure kwani hata mapigo yangu ya moyo sio kama ya mgonjwa wa pressure (alitumia ile mashine ya kusikiliza maskioni).

Basi nikasema ngoja nikahakikishe tena hospital nyingine kule majibu yakasomeka 152/95 Dr. Akasema nichukue tahadhari hivyo mimi nikaamua kununua mashine na kuanza kujipima nyumbani na majibu yangu yakawa yana range 129/87.

Sasa ndugu zangu naombeni ushauri wenu nifanyaje ili niwe vizuri pia kwaajiri ya masailiano yajayo?

Na kwanini nikipimwa na daktari pressure inakuwa juu?

Nawakilisha kwenu ndugu zangu.

Nime attach na baadhi ya matokeo ya vipimo ninayopima hapa nyumbani

IMG_20210411_161436.jpg

IMG_20210411_170703.jpg
 
Jambo afande!!! Samahani kidogo... Masailiano ni kitu gani? Samahani lakini.
 
Pole ndugu, inonekana unawza sana jitahidi upunguze mawazo, hiyo ni sign imeaanza anza kula vema, jiepushe na chimvi, pombe,red meat kula mboga mboga kwa wingi na marunda, fanya mazoezi nk
 
Samahani nisadie jinsi ya kufuta uzi hizo picha za Kombat nimeziweka kwa bahati mbaya
Bonyez content ya uzi, utaona option ya moderate , unaweza futa au ku edit. Karibu Pm nikuelekeze vitu vya msingi
 
Samahani nisadie jinsi ya kufuta uzi hizo picha za Kombat nimeziweka kwa bahati mbaya
Pole Mkuu... Kweli unapressure.. umejisahau ukatupia na za gwanda kabisa.. anyway ingia sehem ya Edit then unamaliza zoezi..

Relax Mkuu, Maisha mafupi Sana.
 
Pole Mkuu... Kweli unapressure.. umejisahau ukatupia na za gwanda kabisa.. anyway ingia sehem ya Edit then unamaliza zoezi..

Relax Mkuu, Maisha mafupi Sana.
Ahsante kwa ushauri kaka
 
Inaelekea mkuu kila ukiitwa kwenye masailiano unakuwa na wasiwasi sana, na hiki ndicho kinapelekea preassure yako kusomeka juu kila mara uwapo kwenye usaili na mara uwapo nyumbani hali hurejea kuwa normal, hiyo kitu wewe mwenyewe ndiye unatakiwa kuidhibiti.

Relax mkuu hakuna jipya chini ya jua.
 
Inaelekea mkuu kila ukiitwa kwenye masailiano unakuwa na wasiwasi sana, na hiki ndicho kinapelekea preassure yako kusomeka juu kila mara uwapo kwenye usaili na mara uwapo nyumbani hali hurejea kuwa normal, hiyo kitu wewe mwenyewe ndiye unatakiwa kuidhibiti.
Relax mkuu hakuna jipya chini ya jua.
Thanks for this great advice
 
Tatizo ni kwamba siku ya usaili unapaniki mno ndo mana pressure inapanda. Relax utaajiriwa tu usiogope.
 
Pressure ya mwili mara nyingi hubadilika kulingana na situation uliyopo. Inaonekana wewe ukiitwa kwenye usaili au kuonana na daktari huwa unaingiwa na hofu inayofanya pressure yako kuwa juu kuliko kawaida. Kwa muono wangu mtu anahesabika kuwa na pressure ya juu ( hypertension) endapo pressure yake ni zaidi ya 145/90 kwa muda mrefu bila kurudi katika hali ya kawaida ( less or equal to 120/80). Kwa hiyo kwa uzoefu wangu huna pressure na huna sababu ya kujipa stress! Relax, fanya mazoezi na kula balanced diet
 
Pressure ya mwili mara nyingi hubadilika kulingana na situation uliyopo. Inaonekana wewe ukiitwa kwenye usaili au kuonana na daktari huwa unaingiwa na hofu inayofanya pressure yako kuwa juu kuliko kawaida. Kwa muono wangu mtu anahesabika kuwa na pressure ya juu ( hypertension) endapo pressure yake ni zaidi ya 145/90 kwa muda mrefu bila kurudi katika hali ya kawaida ( less or equal to 120/80). Kwa hiyo kwa uzoefu wangu huna pressure na huna sababu ya kujipa stress! Relax, fanya mazoezi na kula balanced diet
Ahsante kwa ushauri mzurii mimi pressure yangu huwa ina range 125/84 mara kwa mara hapo sijui imekaaje hiyo?
 
Ahsante kwa ushauri mzurii mimi pressure yangu huwa ina range 125/84 mara kwa mara hapo sijui imekaaje hiyo?
Hiyo bado ipo kwenye normal range Ila jitahidi isizidi 120/80. Fanya mazoezi, kula mlo kamili na kupunguza chumvi kidogo kwenye chakula
 
Hiyo bado ipo kwenye normal range Ila jitahidi isizidi 120/80. Fanya mazoezi, kula mlo kamili na kupunguza chumvi kidogo kwenye chakula
Lakini kikubwa kuliko yote,ondoa hofu, hiyo hofu ndiyo itakuletea ugonjwa halisi, pigana na hofu hiyo ndio adui yako wa kwanza kabisa.
 
Maybe hofu uwa inakujaa kisha moyo unaanza kurukaruka bila utaratibu
 
Back
Top Bottom