Press Release: Ukweli Kuhusu Loliondo

Press Release: Ukweli Kuhusu Loliondo

Na serikali yetu ilivyokosa hoja hapo watajua wameshamaliza kazi,......
 
Kwanini hakikutumika Kiswahili kuwawezesha wahusika kupata maana ya ufafanuzi huu? Waandishi wa habari wakichakachua kwa tafsiri yao watalaumiwa?

Nadhani anafikiri kutumia lugha hii atakuwa anapunguza ukali wa maneno (tafsida).
 
sawa ni kweli yoooote uliyosema mh waziri ila nina maswali ya msingi sana, naomba unipatie majibu au ufafanuzi:

.

2. Je, miaka yote hii serikali ilikuwa wapi wakati watu wanafanya shughuli zao za kiuchumi na kijamii katika ardhi ile? Kwa nini hawakuchukua hatua kwa wakati hadi kusuburi miaka nenda rudi ili ndipo waje wawa-evict wananchi?

Majibu ndugu Waziri...


The Government took this decision with the understanding that environment conservation is as important for eco-system protection as it is for community livelihood and community development. On 26th of March, this year, therefore, Hon. Khamis Sued Kagasheki, Minister for Natural Resources and Tourism, using powers invested into him (me) under Wildlife Conservation Act No. 5 of 2009, Section 16 (4) announced this Government position partly also as effort by Government to resolve a land use conflict that has existed in Loliondo Game Controlled Area for the past 20 years.

Kwa hiyo ndugu waziri unataka kuliambia jukwaa hili kuwa wizara yako ilikuwa inahangaika kuwatimua hawa waliokalia Loliondo kwa muda wa miaka ishirini bila mafanikio !?
 
Mtu mmoja anaweza kuishi sehemu illegally. Kijiji hakiwezi kuishi sehemu illegally...

Kijiji kinaweza kuishi illegally kama wanakijiji wake hawakuchukua hatua kukisajili mahala husika ili kitambulike katika mifumo iliyopo ya kiutawala.
 
Yaani huu ni wizi wa mchana kweupe kabisa vijiji vya loliondo vimepimwa na kupewa hatimiliki leo waziri anasema wamekuwapo illegally? Wananchi maisha yetu yamewekwa rehani zaidi ya tunavyofikiri.
 
Nini ??

Hujui lolote huyu fisadi namba mbili, yeye na mwenzake wamewekwa pale kulinda miradi ya hao hao majangili na kuhakikisha safari ijayo wanyama wanapanda ndege zaidi ...!! Unajua huyu kaoa wapi na wanafanya biashara gani na hao hao waarabu..?

Hii kama ilivyokuwa ile issue ya barabara serengeti itawatokea puani hasa kule wanapopiga mizinga mapesa kila siku na mabakuli yao...

Mh. Kagasheki ndio moja ya viongozi imara kwenye serikali goi goi ya Kikwete. Tatizo ni kwamba kapewa mbuzi ndani ya gunia. Huyu mzee anachojaribu ni kuikoa serikali ya Mr. Dhaifu.

Hongera Mh. Kwa kazi nzuri, ila huyu Tahi.ra anayeitwa rais ndo bure kabisa na genge lake la wajambazi na wauza madawa wakina Riz1 ambao walishaiuza Loliondo kwa ndugu zao waarabu wa Dubai......Chondechonde Mheshimiwa Kagasheki. Usikate Tamaa wananchi tunakupenda sana
 
Sheikh Khamis tuambie waarabu ( au wazungu) wana ekari ngapi huko Loliondo?Poor Masai ,who can read in English?
Wakenya kidogo wanajua kimombo!!!Vipi mbunge wao anasemaje?
 
Ningeomba Mh. Waziri atuweke kinagaubaga ni mgogoro upi wa ardhi ambao umekuwepo zaidi ya miaka 20 iliyopita wakati hiyo ardhi imetengwa kwa ajili ya GCA tangu mwaka 1974? What hapenned in the past 20 years na serikali, given all its powers, kushindwa kuutatua kwa miaka yote hiyo? La sivyo wananchi wana legitimate claims kuhusu hilo eneo!
 
Kijiji kinaweza kuishi illegally kama wanakijiji wake hawakuchukua hatua kukisajili mahala husika ili kitambulike katika mifumo iliyopo ya kiutawala.

HAPANA. Big NOOOOOOOOOOO...

Hapo sheria ndio yenye matatizo sio wanakijiji...
 
Na mikataba mnatumia lugha hii hii halafu mnawapa maasai watie saini...
Mkiambiwa kuongea kingereza,wengine mnataka kujitoa kugombea ubunge Afrika mashariki.....
 
haha hii press release kwa ajili ya waraabu hivi kagasheki wamasai kiswahili kinawapiga chenga je englsi hahaha umeboaa. owamae
 
Unawezaje kusema wamasai wanaishi nchini kwao ilegally. Wakoloni, tanganyika, na tanzania siziliwakuta hapo na mifugo yao wakiishi na wanyama pori kwa amani? Serikali ndio illegal kwa kuwapora ardhi yao na kuwapa waarabu kwa vipande vya fedha.
 
Ningeomba Mh. Waziri atuweke kinagaubaga ni mgogoro upi wa ardhi ambao umekuwepo zaidi ya miaka 20 iliyopita wakati hiyo ardhi imetengwa kwa ajili ya GCA tangu mwaka 1974? What hapenned in the past 20 years na serikali, given all its powers, kushindwa kuutatua kwa miaka yote hiyo? La sivyo wananchi wana legitimate claims kuhusu hilo eneo!

Mkuu hii issue imeanza tokea kipindi cha ukoloni. Wanahistoria wanasema kuwa wanachofanya serikali ya sasa ni mwendelezo wa kilichokuwa kinafanywa na serikali ya kikoloni, lakini serikali ya sasa inafanya kwa gia ya "investors".

Mwaka 1959, watu wote waliokuwa wanaishi eneo la Serenegeti walifukuzwa na serikali ya kikoloni ya Kiingereza ili kufanya eneo hilo kuwa mbuga ya kitaifa. Baadhi ya watu waliofukuzwa walikuwa ni Wamasai ambao waliishia kwenda kuanza makazi mapya eneo la hifadhi la Ngorongoro na Loliondo.

Baada ya uhuru serikali au watu fulani serikalini wameendelea kuwa na jicho ya ulafi kwa kutenga ardhi kwa ajili ya utalii wa picha na wageni kuwindia wanyama. Kwa sasa ulafi huu uko zaidi Loliondo. Mwaka 1992, Otterlo Business Corporation Ltd (inasemekana hii siyo kampuni bali ni kikundi tuu cha watu kutoka Uarabuni) ilipewa Pori tengefu la Loliondo (Game Controlled Area) kwa ajili ya kuwindia wanyama.

Otterlo Business Corporation Ltd hawana ardhi, bali wamepewa tuu leseni ya kuwinda wanyama kwenye korido ya ardhi inayopakana na hifadhi pori ya taifa. Hata hivyo, kinadharia wanaweza kuwinda mpaka panya kuzunguka ofisi ya mkuu wa wilaya hiyo.

Kila panapokuwa na mgogoro baina Otterlo Business Corporation Ltd na Wamasai, serikali inakuwa upande wa Otterlo Business Corporation Ltd. Utakumbuka nini kilitokea mwaka 2009. Pamoja na kwamba Otterlo Business Corporation Ltd na Wamasai walifikia suluhisho na kurudi kwenye eneo husika, mwaka 2011 serikali ilianza tena chokocho zake kwa kuja na mpango wa kuifanya hiyo korido kuwa pori tengefu, chini ya Sheria ya Hifadhi ya Wanyama No. 5 ya mwaka 2009.

Kipindi cha ukoloni, pori tengefu ilikuwa ni sehemu ya kuwindia wanyama. Hii ni tofauti na sehemu ya wazi (open area) ambayo hairuhusiwi kuwindia wanyama. Kwa vile matumizi ya ardhi kwa ajili ya kilimo na ufugaji yalikuwa ni sehemu ya wazi, Game Controlled Area iliangukia kwenye ardhi ya vijiji.

Hili jina la "Game Controlled Area" limeendelea kuwepo hata baada ya uhuru bila kuwa na maana yoyote. Kama walivyofanya wakoloni, serikali ya sasa imeendelea kutumia concept ya "Game Controlled Area" kwa nia ya kuwachanganya watu na kweli imefanikiwa kwa hilo.

Jaribu kujiuliza kwa nini "Game Controlled Area" ziko Tanzana tuu?
 
Mkuu hii issue imeanza tokea kipindi cha ukoloni. Wanahistoria wanasema kuwa wanachofanya serikali ya sasa ni mwendelezo wa kilichokuwa kinafanywa na serikali ya kikoloni, lakini serikali ya sasa inafanya kwa gia ya "investors".

Mwaka 1959, watu wote waliokuwa wanaishi eneo la Serenegeti walifukuzwa na serikali ya kikoloni ya Kiingereza ili kufanya eneo hilo kuwa mbuga ya kitaifa. Baadhi ya watu waliofukuzwa walikuwa ni Wamasai ambao waliishia kwenda kuanza makazi mapya eneo la hifadhi la Ngorongoro na Loliondo.

Baada ya uhuru serikali au watu fulani serikalini wameendelea kuwa na jicho ya ulafi kwa kutenga ardhi kwa ajili ya utalii wa picha na wageni kuwindia wanyama. Kwa sasa ulafi huu uko zaidi Loliondo. Mwaka 1992, Otterlo Business Corporation Ltd (inasemekana hii siyo kampuni bali ni kikundi tuu cha watu kutoka Uarabuni) ilipewa Pori tengefu la Loliondo (Game Controlled Area) kwa ajili ya kuwindia wanyama.

Otterlo Business Corporation Ltd hawana ardhi, bali wamepewa tuu leseni ya kuwinda wanyama kwenye korido ya ardhi inayopakana na hifadhi pori ya taifa. Hata hivyo, kinadharia wanaweza kuwinda mpaka panya kuzunguka ofisi ya mkuu wa wilaya hiyo.

Kila panapokuwa na mgogoro baina Otterlo Business Corporation Ltd na Wamasai, serikali inakuwa upande wa Otterlo Business Corporation Ltd. Utakumbuka nini kilitokea mwaka 2009. Pamoja na kwamba Otterlo Business Corporation Ltd na Wamasai walifikia suluhisho na kurudi kwenye eneo husika, mwaka 2011 serikali ilianza tena chokocho zake kwa kuja na mpango wa kuifanya hiyo korido kuwa pori tengefu, chini ya Sheria ya Hifadhi ya Wanyama No. 5 ya mwaka 2009.

Kipindi cha ukoloni, pori tengefu ilikuwa ni sehemu ya kuwindia wanyama. Hii ni tofauti na sehemu ya wazi (open area) ambayo hairuhusiwi kuwindia wanyama. Kwa vile matumizi ya ardhi kwa ajili ya kilimo na ufugaji yalikuwa ni sehemu ya wazi, Game Controlled Area iliangukia kwenye ardhi ya vijiji.

Hili jina la "Game Controlled Area" limeendelea kuwepo hata baada ya uhuru bila kuwa na maana yoyote. Kama walivyofanya wakoloni, serikali ya sasa imeendelea kutumia concept ya "Game Controlled Area" kwa nia ya kuwachanganya watu na kweli imefanikiwa kwa hilo.

Jaribu kujiuliza kwa nini "Game Controlled Area" ziko Tanzana tuu?

Mkuu EMT, asante kwa kuiweka hii historical perspective ya mgogoro huu wa Loliondo, kitu ambacho hakikuwekwa wazi kwenye hii 'ress release' na ndo maana nikahoji kwamba in fairness, this hould have been highlighted.

Nikubaliane na wewe..and it is a fact kwamba historically conservation in Tanzania has inherited the 'comand and control' approach ya wakoloni enzi zile. kilichobadilika, kimsingi, ni utawala tu, lakini approach bado ni ile ile na watu wamekuwa 'wakaidi' kubadilika ijapokuwa siku hizi kumekuwa na alternative approaches za conservation sema zenyewe zina-involve more devolution bythe state...giving more than what they used to take....sasa hapa ndo kwenye mgogoro mkuu. Issue ya Loliondo, ni classical example ya collision kati ya state na communities kwenye conservation, state ikihimiza 'comand and control ( sheria ya wanyamapor, waziri mwenye dhamana na mamlaka, kutenga hayo maeneo Tengefu-GCAs, NP, GRs nk) huku wananchi wakililia ardhi ambayo historically, ni ya kwao, wameishi hapo, wameishi na hao wanyama, hawajacompromise ecological integrity tangu wakati huo..ila sasa wanasingiziwa kila aina ya bad conservation behavior, na kwamba eti 'wanaonewa huruma tu' kwa kupewa eneo la shughuli zao na serikali!

Ndio maana nasema kama kweli wame -aim kuelimisha jamii, basi they should come out kuelezea kiini hasa cha huu mgogoro maana sijaona popote kwen press release ambapo ortelo imetajwa au mwekezaji ametajwa!

Asante tena mkuu EMT kwa hiyo perspective na ni maoni yangu kuwa mtu yeyote akitaka kuanalyse objectively hii issue ya Loliondo lazima aelewe unakoanzia.
 
Last edited by a moderator:
Kama kweli hao wamasai wanaishi hapo kinyume na sheria:
1. Kwa nini serikali imewaacha wakivunja sheria kwa muda wotye huo?
2. Kwa nini serikali nayo inavunja sheria yake na kugawa eneo la hifadhi kwa wavunja sheria?
3. Utawala wa sheria unataka wavunja sheria washtakiwe. Kwa nini serikali haiwashitaki wamasai hao badala yake inawagawia ardhi?
4. Kama serikali ina haki katika suala hili mbona inatumia nguvu kubwa sana kutisha watu wake?

Serikali iache ubabaishaji.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom