TANZIA President Bingu wa Mutharika of Malawi is dead!

Hizi si tetesi tena, ni kweli kafariki dunia. Hapa ndipo utajua kwamba T.B. Joshua tabiri zake huwa za kweli. Wazimbabwe walidhani ni Mugabe, wao wakakataa kuwa hawakumtaja Mugabe. Majuzi kasema kifo chake kimekaribia zaidi.

Prophet TB Joshua Says

yes alitabiri ila kumbuka pia alisema muda ukifika atataja jina na nchi kitu ambacho hajafanya bado.
 
Kwa bahati mbaya hakutaja jina la rais atakayekufa,kwa hiyo hakuna anayeweza kuconfirm kwamba alikuwa anamlenga mgabe au mwingine. Lakini kwa kuwa jumapili tu amesistiza kwamba mfaji yupo karibu sana kuondoka na leo ndiyo amekufa huyu basi bila shaka huyu ndiye aliyelengwa. Kama kweli Joshua alikuwa anaona katika maono yatokanayo na Mungu basi ni dhahiri hata Joshua mwenyewe alikuwa hajui ni yupi wa kufa, zaidi ya kuelekezwa na Mungu kwamba kuna mtu atakufa. But hofu yangu ni kuwa isijekuwa Joshua anafanya kazi kwa nguvu za ibilisi. Maana sidhani kama katika utabiri, Mungu atamfunulia mtu hili, ili afanye nalo nini? Na lina fundisho gani katika imani? Napata mashaka katika hilo.

sina uhakika na imani yako ila kama ukiwa ni mkristo na unasoma biblia, ningalikuuliza je,Yesu alijua kifo chake? ukipatia kujibu basi huna sababu kudoubt haya ya Joshua.
 
Utabiri wa tb joshua watimia,alisema ndani ya miezi miwili kuna rais barani africa atakufa watu wakagues mugabe.

Mungu kasema "wanadamu mtakufa hakika" husemi au hata ku-acknowledge, akisema TB haraka kushuhudia, kweli hiki ni kizazi cha nyoka!!!!
 
sina uhakika na imani yako ila kama ukiwa ni mkristo na unasoma biblia, ningalikuuliza je,Yesu alijua kifo chake? ukipatia kujibu basi huna sababu kudoubt haya ya Joshua.

Nikujibu mimi, yesu alijua kifo chake, yeye mwenyewe alijua kifo chake, hakutabiriwa na TB joshua wa enzi hizo. maandiko yanasema "ana hasara azitegemeaye nguvu za mwanaadam"
 
sina uhakika na imani yako ila kama ukiwa ni mkristo na unasoma biblia, ningalikuuliza je,Yesu alijua kifo chake? ukipatia kujibu basi huna sababu kudoubt haya ya Joshua.
Swali lako ni irrelevant? Yesu kujua kifo chake ni tofauti kabisa na TB Joshua kujua kifo cha Mutharika. What does it aid to faith? Labda kama TB Joshua anaweza kufanya maombi ili Mutharika aamke kutoka kwa wafu basi hilo litakuwa na mchango katika kuongeza imani. Hili la kusema tu atakufa, mbona hata shehe yahya alikuwa anaweza? Hebu soma Mathayo 24 sura ile yote, then utaelewa maana ya manabii wa uongo. binafsi utabiri huu unanifanya nimweke TB Joshua kwenye mashaka kama kweli anafanya kazi ya Mungu au ni mkono wa Ibilisi.
 
Rais wa Malawi Bingu wa Mutharika bado yupo kwenye COMA, hajafariki kama habari zilivyoenea kwenye mitandao. Amesafirishwa kwenda kupata matibabu nchini South Africa na atapelekwa katika Hospital ya Milpark Hospital, Johannesburg. Bado yupo njiani na ndege yake bado haijafika, lakini anategemewa kuingia muda wowote kuanzania sasa, anasubiriwa hapa Airport na chopa ipo tayari kumpeleka ICU, Ila hali yake ni tia maji tia maji kama alivyokuwa rais wa Zambia Marehemu Levy Mwanawasa.
 
mnamchuria kifo hajafa bado
cardiac arrest watu wanadhani kafa
labd tupate taarifa kamili kutoka ikulu ya malawi
angekufa kweli BBC CNN na local medias wangeshatangaza hadi mdaa huu naandika hakuna taarifa kamili
Vyanzo vyangu vya habari malawi vimethibitisha Dr Bingu wa Mutharika amefariki wanapeleka mwili wake south africa ili kuandaa mazingira ya utawala nchi hiyo.....utabiri wa TB Joshua umetimia
 
Rais wa Malawi Bingu wa Mutharika bado yupo kwenye COMA, hajafariki kama habari zilivyoenea kwenye mitandao. Amesafirishwa kwenda kupata matibabu nchini South Africa na atapelekwa katika Hospital ya Milpark Hospital, Johannesburg. Bado yupo njiani na ndege yake bado haijafika, lakini anategemewa kuingia muda wowote kuanzania sasa, anasubiriwa hapa Airport na chopa ipo tayari kumpeleka ICU, Ila hali yake ni tia maji tia maji kama alivyokuwa rais wa Zambia Marehemu Levy Mwanawasa.

Source plz!!!!!
 
Back
Top Bottom