Pongezi Kwa CHADEMA

jnuswe

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2010
Posts
1,270
Reaction score
549
Wana JF,

Mimi baada ya kutafakari kwa kina kwa ushindani uliopo na chuki inayojitokeza kati ya vyama vikuu viwili vya siasa CHADEMA na CCM nimekuja kugundua kwamba CHADEMA imeweza kufanya kazi kubwa sana ya kuidhoofisha CCM kwa mwaka 2012 na 2013 kwa kueneza sera zake zinazokubalika kwa Watanzania. Sifurahi chuki baina ya hivi vyama viwili lakini hakuna jinsi kwa sababu ndio hali halisi kuwa waliozoea kutawala baada ya kuona uwezekano huo unaweza usiwepo kabisa 2015 wameamua kueneza siasa za chuki.

Uthibitisho wa kwamba CHADEMA imefanya kazi kubwa ya kuidhoofisha CCM ni siasa za maji taka na chuki inayojitokeza baina ya vyama hivi viwili pasipo kuisahau NCCR Mageuzi. Haina shaka kwamba chuki hii ya CCM dhidi ya vyama vinzani ni hofu ya kuondoka madarakani

CCM walidhani historia ya vyama vya upinzani nchini Tanzania ya kuanza kwa nguvu na wao CCM kuvidhoofisha itafanikiwa kwa CHADEMA sasa wamekuja kugundua muda unaenda badala ya CHADEMA kudhohofika kinaimarika zaidi

Natoa pongezi kwa uongozi wa CHADEMA ngazi ya Taifa , Kanda, Mikoa , Wilaya hadi ngazi ya msingi matunda ya kazi yenu yameonekana

Nawasilisha
 
naungana na ww huo ndo ukwl mtupu...ccm watajuta kuchakachua ushindi wa dr slaa
 
Pamoja kamanda, ndani ya CDM ukiwa msaliti tuu unatoswa. Chama kilichojaa Intelejensia kinachompambana na majaribu mengi ikiwa kuuwawa kwa wananchama wake, kupigwa mabomu, kuonewa bungeni, kbambikiwa kesi n.k.
 
Hiki ni kipindi cha mapambano ambapo ni wajibu wa watanzania wanaoitakia mema nchi yetu kushiriki mapambano haya kwa namna yoyote wanayoweza, kuanzia katika mazungumzo ya kawaida mtaani, hapa JF na pia kuangalia namna ya kuchangia katika harakati hizi. tunahitaji kuwafariji wale wahanga wa moja kwa moja wa harakati hizi, mfano makamanda walio na kesi, familia zao ambazo zinaathirika moja kwa moja, majeruhi wa hasira kali ya vyombo vya usalama ambavyo vinatumika sasa kulinda chama ambacho kinashuhudia kupoteza nguvu kwa maana ya mamlaka ya wananchi na kinabakia na vyombo vya dola. kitapambana kama nyati aliyejeruhiwa na hakitakuwa na huruma. matamko ya PIGA UA kutoka kwa wakuu wa serikali (Pinda, Wassira, vyombo vya habari vya serikali, etc.) ni viashiria kwamba vita imepamba moto
 
kweli mkuu hata mimi chadema napongeza kwa kazi kumbwa walioifanya. Ccm wakisikia chadema wanataka kukukimbia matumbo joto, sasahivi wanatapatapa tu
 
Chadema chini ya jemedari mbowe na slaa aaa ccmhawali hawalali jamani, njia nyeupe kwenda ikulu
 
Wengi tumekuwa Manaibu Katibu Itikadi na Uenezi wa Chadema bila kujijua, hii inatokana na kelele nyingi tunazopiga Bungeni, Redioni, TV, kuandika sana magazetini, mitaani, vyuoni, mashuleni, mahakamani, maofisini, magerezani, polisi, vyombo vyetu vya usafiri kama daladala, melini na katika ndege, mahospitalini na kwingineko. Kote huko Chadema inazungumzwa sana hata watoto wadogo kuanzia cheke chekea wanahubiri Chadema kwa "Alama ya V"

Alama za Chadema ni:
Alama ya V: Alama hii maana tofauti zenye lengo linalokaribiana sana kufanana.


1. Left wing beliefs are usually progressive in nature, they look to the future, aim to support those who cannot support themselves, are idealist and believe in equality. People who are left wing believe in taxation to redistribute opportunity and wealth - things like a national health service, and job seeker’s allowance are fundamentally left wing ideas. They believe in equality over the freedom to fail.


2. Right wing beliefs value tradition, they are about equity, survival of the fittest, and they believe in economic freedom. They typically believe that business shouldn’t be regulated, and that we should all look after ourselves. Right wing people tend believe they shouldn’t have to pay for someone else’s education or health service. They believe in freedom to succeed over equality.

Hakika ukitaka debe tupu lisitike, jaza maji. Kuhamisha toka sehemu moja kwenda nyingine ni kueneza ujumbe au kulinyamazisha kwa kulipiga ni kuendeleza ngoma waisikiayo ngoma hiyo huingia kucheza.

Tangazo la Waziri wetu Mkuu aliyerithi Cheo hiki kwa Dharura ya Lowassa badala ya kutoa machozi sasa ametamka kwamba Chadema na wapinzani wengine RASMI WAPIGWE na Polisi. Hapo zamani Polisi walipiga, tukilia na kumwambia Pinda tumepigwa alitudanganya kwamba atawawajibisha hawa viranja wa "Madarasa" Sasa bila shaka WATAVUKA MIPAKA MAANA BABA KAWAAMBIA WAANZE KUTUCHAPA.
Mh. Pinda, umesema waanze kutuchapa au waendelee kutuchapa? Kama ni kupiga mbona walianza zamani sana? Usugu huu wa Watanzania unaouona sasa ni matokeo ya kutuchapa sana, sasa umetoa amri ya wao kutuchapa nadhani sasa watatuua mbele ya Ikulu.
 
Hili liko wazi kila mtu analiona,cha kushauri na kusisitiza katika mikutano yao CDM wawasisitize wananchi hasa vijana kujitokeza kwa wingi katika kuboresha daftari la kudumu la wapiga kura ili waweze kujiandikisha pia kwenye vitambulisho vya uraia ili 2015 kiwe kishindo kikuu
 
tanzania zamu yetu imefika ya kushuhudia mabadiliko ndani ya utawala wa taifa'namshukuru Mungu kwa sababu wengi wetu tutapewa nafasi ya kushuhudia hilo'ccm imewatesa sana babu zetu baba zetu na sasa wanatutesa na sisi'tanzania haiwezi kuwa nchi inayotawaliwa na chama kimoja na majina yale yale miaka nenda rudi'ushauri wangu kwa ccm kubalini upepo unaokuja na zaidi ya tsunami'
Ile michezo yenu ya kurubuni na kuiba kura umekwisha'kazi mnayo
 

Ni dhahiri tunaanza kunena kwa lugha bila kulazimishwa.fredom hiyoooooooooooooooooooooo
 
Yes, Kazi ni nzuri so far, lakini nafikiri kazi ni kubwa zaidi kuelekea 2015, changamoto kwa chadema ni nyingi mno, ukizingatia kesi zinafunguliwa mfululizo; makada wake kununuliwa; kuwekewe vikwazo wakati wa kukitangaza chama kupitia maandamano na mikutano ya hadhara n.k
 
Tanzania bila CCM inawezekana, Watanzania tubadilike tusikubali kununuliwa kama karanga kwa nafasi tena CCM iendelee kutuibia rasilimali zetu tulizoachiwa na wazalendo wa kweli wa nchi hii, tusiwape tena nafasi CCM waendelee kutupa Huduma mbovu za Afya na Elimu tubadilike
 

Watapinga tu, ngoja waje hapa utaona watakavyowaka. Takwimu zipo tangu CDM imeanza kushiriki katika chaguzi mbali mbali imekuwa ikipanda kwa kuongeza viti, lakini ngoja uone walivyo wasahaulifu hata viti vya udiwani ilivyopata chadema wiki moja na nusu tu iliyopita watajifanya wamesahau..
 
Nashauri sasa ifunguliwe account ya bank inayoitwa okoa chadema dhidi ya kesi.hii tasaidia kulipa gharama za usafiri kwa mawakili na washitakiwa kwa kesi za mbali.

Benki zetu haziko huru!
Zinaweza kuzuiwa na POLICCM!
Labda viongozi watupe namna mbadala maana hawa magamba wanataka kwenda na aliye hai kama afaye maji!
 
Naona CCM sasa wanataka eti kutuaminisha kuwa CDM na viongozi wake ni magaidi. Kwa ujinga wa CCM na maelekezo yake kwa vyombo vya usalama na sheria vinavyoshiba kutoka kwao wanaona eti wananchi watawapenda, hivi hawajui kwa sasa kampeni zinapigwa kila kona? Mfano mtu wa kijijini ambaye hajui kinchoendelea kwa sasa anaeleweshwa na wa mjini. CCM ni chama cha kigaidi namba moja, walimuua Kolimba, wakamuua Professor Malima, wakamuua Imran Kombe, na juzi wametega bomu wakaua watu. CCM ni waujai na hawatakaa kuturudisha nyuma enzi za CUF. Come 2015 wataona kitakachotokea! Wao ni wachache sisi ni wengi, by numbers lazima waishe tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…