BIN BOR
JF-Expert Member
- Nov 23, 2010
- 1,013
- 407
Polisi walikuwa wanaranda kutafuta baa ambazo hazijafungwa saa sita usiku. Mara wakaiona baa moja ina wateja. Walipoingia pale, walevi karibu wote wakakimbia isipokuwa mmoja aliyelewa sana akaanguka chini kutoka kwenye stuli ndefu. Akawa kama kapoteza fahamu hivi. Polisi mmoja akamwagia maji na kumpepea yule mlevi akazinduka. Maongezi yakawa hivi......
Mlevi : Nini kinaendelea hapa?
Polisi : Ulianguka, ukapoteza fahamu. Sasa umezinduka amka twende kituoni.
Mlevi : Uliniona wakati naanguka?
Polisi : Ndio
Mlevi : Unanifahamu mimi?
Polisi : Hata! Sikufahamu.
Mlevi : Sasa afande, kama hunifahamu ulijuaje kuwa ni mimi ndiye niliyeanguka?
Mlevi : Nini kinaendelea hapa?
Polisi : Ulianguka, ukapoteza fahamu. Sasa umezinduka amka twende kituoni.
Mlevi : Uliniona wakati naanguka?
Polisi : Ndio
Mlevi : Unanifahamu mimi?
Polisi : Hata! Sikufahamu.
Mlevi : Sasa afande, kama hunifahamu ulijuaje kuwa ni mimi ndiye niliyeanguka?