Polisi wazuia ndoa ya mtoto wa darasa la sita mkoani Shinyanga

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397
Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga kwa kushirikiana na shirika la Agape linalopambana na uvunjifu wa haki za watoto wakike limefanikiwa kuzuia ndoa ya mtoto wa darasa la sita aliyekuwa anaolewa na mwanaume wa miaka 26 kwa mahali ya ng’ombe 14.

ITV ilifika katika kijiji cha Mwigumbi kata ya Maganzo wilayani Kishapu na kukutana na sakata hilo ambapo punde tu baada ya polisi kuvamia eneo hilo wazazi wa watoto hao walikimbia na kujificha pasipojulikana ndipo polisi walipowakamata vijana hao na kuwafikisha katika kituo cha polisi cha Maganzo ambapo Msaidizi wa Kamanda wa Jeshi la polisi mkoani Shinyanga Greyfton Mushi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.

Aidha baadhi ya wakazi wa maeneo hayo walioshuhudia tukio hilo wametoa maoni yao na kuiomba serikali kuwachukulia hatua kali wahusika ili iwe fundisho kwa watu wenye tamaa ya kupata mali kwa kuozesha watoto wadogo.

John Miyola ni Mkurugenzi wa shirika la Agape amesema ndoa na mimba za umri mdogo zinachangiwa na baadhi ya viongozi wa kata na vijiji kushindwa kutambua wajibu wao katika jamii huku mkuu wa wilaya ya Kishapu Bi.hawa Ng’humbi akiagiza watendaji hao pamoja na wazazi wanaohusika kukamatwa na kuchukuliwa hatua kali za kusheria.

Chanzo: ITV
 
Muoaji ndio mwenye kosa alambe mvua za kutosha ili iwe fundisho kwa wenye tabia kma zake
 
Kukosekana kwa maarifa na uelewa wa Elimu Ndiko kunachangia Haya Mambo yatokee maeneo mbalimbali nchini!
 
Kishapu kuna tatizo kubwa san a la mimba za utotoni, angalao haya mashirika kama Agape na TGNP wamepiga kambi huko wanajaribu kukimbizana nao.

lazima serikali ichukue hatua kali kabisa, huu ni ubakaji , ni uvunjivu wa haki za msingi za mtoto za kupata elimu.

Mkuu wa wilaya atoke ofisini achukue hatua
 
Back
Top Bottom