Inside10
JF-Expert Member
- May 20, 2011
- 33,783
- 40,564
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dare es Salaam limewakamata watu wanne na pikipiki zao, kwa tuhuma za kusababisha kero na fujo kwenye makazi ya watu kufuatia vyombo vyao vya moto ambavyo wanaviendesha kutoa kelele za milio mikali ya milipuko, suala ambalo ni kosa na kinyume cha Sheria ya Usalama Barabarani.
Jeshi hilo limewataja watuhumiwa hao kuwa ni Abdallah Masumbuko mkazi wa Tabata, Julius Dismas, mkazi wa Mwananyamala, Salehe Ally, mkazi wa Kijitonyama, Mohamed Rashid mkazi
wa Magomeni, ambao wote wapo mahabusu na hatua zaidi zinachukuliwa ili kuwafikisha kwenye mamlaka zingine za kisheria.
Jeshi la Polisi linatoa wito kwa watumiaji wote wa barabara wakiwemo waendesha vyombo vya moto kuendelea kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za usalama barabarani pasipo kubugudhi watu wengine.
Jeshi hilo limewataja watuhumiwa hao kuwa ni Abdallah Masumbuko mkazi wa Tabata, Julius Dismas, mkazi wa Mwananyamala, Salehe Ally, mkazi wa Kijitonyama, Mohamed Rashid mkazi
wa Magomeni, ambao wote wapo mahabusu na hatua zaidi zinachukuliwa ili kuwafikisha kwenye mamlaka zingine za kisheria.
Jeshi la Polisi linatoa wito kwa watumiaji wote wa barabara wakiwemo waendesha vyombo vya moto kuendelea kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za usalama barabarani pasipo kubugudhi watu wengine.