Polisi na maafisa Maliasili Bunda

Polisi na maafisa Maliasili Bunda

jaffari odhiambo

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2014
Posts
526
Reaction score
13
Polisi na maliasili Bunda wamechachamaa kukamata wanaoleta mkaa mjini hapa jana na leo. Polisi na hao maliasili wanawasaka waleta mkaa kwa kutumia gari la maliasili na wakiwakamata wanachukua na baisikeli zao.

Jamani hili suala linakera sana maana hao wanaoleta mkaa sio wakataji wa moto maana wao wamenunua ili wauze na kupata angalau pesa ya matumizi. Sasa kama hali ya kijijini ni ngumu vile tujuavyo kweli hawa sio kwamba wananyanyaswa?

Halafu huo mkaa wanagawana na ukibaki wanauza na kugawana pesa. Je, mbona wao sasa wanauza?
 
Heheheeee hao polisi wanashindwa kutafuta wajambazi wanakalia kukamata wenye mkaa. Je, huyo aliyeuwawa hapo Bunda watuhumiwa walikamatwa? Ama polisi wamelala tu? Mbona hapa Moshi hamna huo ujinga? Poleni sana.
 
Jamani hawa polisi nao ni wanyang'anyi maana wanamkamata mlalahoi sasa sijui ataishije. Hawa polisi hawako makini.
 
Kama kijijini kuna maisha magumu serikali iruhusu uchomaji wa mkaa na kumaliza misitu?.eti wawakamate wachomaji hivi unajua uchomaji mkaa ulivyo? Mimi nimewahi choma mkaa kabla ya kuwa kolokoloni kiukweli kutukamata ni ngumu mno kwani huwa tunaweka watoa taarifa kila kona kuwa wakiaona askari wanakuja msituni watujulishe na kweli tulikuwa tulikuwa tunajulishwa na hatukamatwi ila walipoanza kukamata wabebaji mkaa tu mambo yakawa magumu sana maana mkaa ukakosa hivyo niliacha hiyo kazi kuepuka jela
 
Wakikamatwa wabebaji mkaa hukosa wanunuaji katika eneo la kuzalishia hivyo mchomaji huacha maana wa kumuuzia mkaa wake.
 
Polisi wa nchi hii noma kweli kweli... mbona wanaonewa sana hawa wachuuzi wadogo wadogo halaf wanaacha majambazi wakubwa
 
Inawezekana hawawajui hao majambazi ila ukiwataja hapa jf najua watawafuatilia tu.
 
Hii kadhia iliwahi kutukuta Moshi; tulikuwa na gunia 3 kwenye pick-up tukasimamishwa na wahuni wanatumia private car (Noah) wakajitambulisha ni wa mazingira wakatwambia tuwaoneshe vibali vya mkaa. tukawauliza ni vibali vipi nao wakatuuliza kwa nini hatuvijui sisi, na kama hatuna vibali ni kosa wanatunyang'anya mkaa. Tukagoma, wakaanza kututishia kama vipi tuwape Tsh 100,000. kuna jamaa yangu anafahamiana na jamaa wa misitu (TFS) akampigia akatuagiza twende ofisini kwao, tulivyofika tukaoneshwa sheria ya misitu na vifungu vinavyotutaka kulipia ushuru tena kwa uzito, kg. Tukalipia 10,500@ (31500/=). Wale jamaa wa mazingira hovyo sana.
 
Polisi kazi yao ni kupenda vya bure ndo maana wanawakamata wanyonge wasiokuwa na uwezo.
 
Polisi na maliasili Bunda wamechachamaa kukamata wanaoleta mkaa mjini hapa jana na leo. Polisi na hao maliasili wanawasaka waleta mkaa kwa kutumia gari la maliasili na wakiwakamata wanachukua na baisikeli zao.

Jamani hili suala linakera sana maana hao wanaoleta mkaa sio wakataji wa moto maana wao wamenunua ili wauze na kupata angalau pesa ya matumizi. Sasa kama hali ya kijijini ni ngumu vile tujuavyo kweli hawa sio kwamba wananyanyaswa?

Halafu huo mkaa wanagawana na ukibaki wanauza na kugawana pesa. Je, mbona wao sasa wanauza?

Wacha uzushi we mtoto ws kiume.

Biashara ya mazao ya misitu tanzania nzima imeingia mkenge, ---- mawakala wa misitu wanaitwa TFS, kazi yao ni kuhakikisha misitu haiharibiwi ambapo madhara yake kila mtu anayajua. Kuepuka kamatakamata hyo ni kuwa na lessen ya uvunaji ili uvune kihalali.

Si kweli kuwa wanagawana pesa hizo, labda kama umefanikiwa kuwashawishi rushwa, wakiuza wanauza kwa bei ya serikali na hivyo kuongeza makusanyo.

Mlisha kalili kuwa polisi waonevu basi tu mmawapinga hata kwa suala jema
 
Wacha uzushi we mtoto ws kiume.

Biashara ya mazao ya misitu tanzania nzima imeingia mkenge, ---- mawakala wa misitu wanaitwa TFS, kazi yao ni kuhakikisha misitu haiharibiwi ambapo madhara yake kila mtu anayajua. Kuepuka kamatakamata hyo ni kuwa na lessen ya uvunaji ili uvune kihalali.

Si kweli kuwa wanagawana pesa hizo, labda kama umefanikiwa kuwashawishi rushwa, wakiuza wanauza kwa bei ya serikali na hivyo kuongeza makusanyo.

Mlisha kalili kuwa polisi waonevu basi tu mmawapinga hata kwa suala jema


Wewe usiseme watu wamekariri yawezekana ana uhakika na anachokisema.
 
Huku kwetu wanatoza ushuru wa gunia na baiskel,acpo kuanayo ananyang'anywa vyote kisha anapigiwa kila kifaa elfu 2o
 
Kama kijijini kuna maisha magumu serikali iruhusu uchomaji wa mkaa na kumaliza misitu?.eti wawakamate wachomaji hivi unajua uchomaji mkaa ulivyo? Mimi nimewahi choma mkaa kabla ya kuwa kolokoloni kiukweli kutukamata ni ngumu mno kwani huwa tunaweka watoa taarifa kila kona kuwa wakiaona askari wanakuja msituni watujulishe na kweli tulikuwa tulikuwa tunajulishwa na hatukamatwi ila walipoanza kukamata wabebaji mkaa tu mambo yakawa magumu sana maana mkaa ukakosa hivyo niliacha hiyo kazi kuepuka jela


Mkuu miondombinu iliyopo ni ya mkaa kuchomwa tu! umewahi kujiuliza ni watanzania wangapi wanaotumia mkaa kupikia? Hivi ikitokea mkaa ukapotea ghafla mjini hali za watu zitakuaje. Zaidi ya asilimia 80 ya watanzania wanaoishi mjini wanategemea mkaa kupikia, huwezi kuokoa misitu bila kua na nishati mbadala ya uhakika.
 
Wewe usiseme watu wamekariri yawezekana ana uhakika na anachokisema.


#Ntamaholo wewe yawezekana ni mmoja kati ya hao wanaokamata. Hao watu wanauza mkaa kwa hawa wauzaji wa rejareja hapa mjini. Pia mikaa mingine wanapeleka makwao sasa unapobisha unakuwa na akili gani hiyo? Uhakika tunao na kamatakamata hiyo ndo ilimuua yule mama wa maliasili wa kule bondeni kuelekea Taasisi aitwaye BOKE maana alikuwa hatari sana kwa kukamata wakiwa na MATEMBO. Wapo na wanawake wengine na wanaume wengine wanakatia hapa mjini. Hivyo kama unakataa basi wewe ni mmoja wa wakamataji hao mnaowasumbua walalahoi. Kuna mzee mmoja tu wa kijaluo ambaye wanaogopa kumkamata hata wakikutana naye wanmuacha.
 
Mkuu miondombinu iliyopo ni ya mkaa kuchomwa tu! umewahi kujiuliza ni watanzania wangapi wanaotumia mkaa kupikia? Hivi ikitokea mkaa ukapotea ghafla mjini hali za watu zitakuaje. Zaidi ya asilimia 80 ya watanzania wanaoishi mjini wanategemea mkaa kupikia, huwezi kuokoa misitu bila kua na nishati mbadala ya uhakika.

Mkaa ukiondoshwa nishat mbadala itapatikana. Kwa mtu anayefikiria vizur si vema kuacha ukataji holela wa misitu eti kutafta mkaa. Tunawaandalia tanganyika gani watoto wetu?

Huyo mzee wa kijaluo atakuwa mchawi, hata kigoma yupo ana tdi hakamatwi na polisi wala maliasili, walishamwacha.

Ukweli ni kuwa, tunaitengeneza jamii mpya, iwapo tutatumia ma.sa.bu.ri kufikiri wanaonewa, hapo tunawatangazia umaskini watoto wetu.

By the way, hakuna aliyewakatalia kuuza mkaa, ila wanasimamiwa ili wafuate sheria ya maliasili.

Sijui mnashauri sheria isifuatwe kisa kuwatuza maskini?

Kama wanahisi wanaibiwa, wakubali kwenda kulipia kila gunia ofisi za maliasili, waache kulalamika
 
Tatizo ni uamuzi wanani awe kiongozi pale bunda. Walishindwa kuchagua mbunge sahihi sasa acha wakome ubishi.
Tena nasikia ndiyo wilaya ya mwisho kwa umasikini Tanzania.
Mlipokea kanga na chumvi na vibukubuku ndo sasa vinawatokea mapuani.
Hakuna cha bure zaidi ya maisha bora kwa kila mtanzania kupitia T 2005-2015 Kikwete tumechoka, pinda liwalo na liwe-a.k.a wapigwe tu.
 
Tatizo ni uamuzi wanani awe kiongozi pale bunda. Walishindwa kuchagua mbunge sahihi sasa acha wakome ubishi.
Tena nasikia ndiyo wilaya ya mwisho kwa umasikini Tanzania.
Mlipokea kanga na chumvi na vibukubuku ndo sasa vinawatokea mapuani.
Hakuna cha bure zaidi ya maisha bora kwa kila mtanzania kupitia T 2005-2015 Kikwete tumechoka, pinda liwalo na liwe-a.k.a wapigwe tu.

Hata kama wangemchagua nani, lzm ulinzi wa misitu uimarishwe. Ukiangalia mazao ya misitu mwanza hutoka kigoma na tabora, lkn kwa operation iliyofanyika na inayoendelea ya TFS, milango na biashara nyingine za misitu zimekuwa adimu mwanza. Beria korofi ni kakonko ambapo ni jimbo la mhabwe kwa mkosamali, kutoka kasulu kuna buyogela na machali kote wanaofanya biashara ya misitu wako hoi, wamefiliska. Uvinza kunakoendelea uvunaji yupo kafulila nako kama huna leseni ya uvunaji hakipiti kitu.

Huko unakodhani wako salama kwa kuchagua unaoamini ni wanamapinduzi, nenda arumeru mash ukionekana na upanga porini utajuta kuzaliwa. Kule unaruhusiwa kuokota kuni iliyoanguka siyo kukata. Ukikata kuni kila mwananchi ni mlinzi, lzm ukamatwe.

Arusha na moshi wako vizuri kwenye uhifadhi wa mazingira hawana huruma na mvunaji haram
 
Back
Top Bottom