Polisi mtwara wakimbia makazi

Polisi mtwara wakimbia makazi

Hii nayo ni moja ya habari za uchochezi na tuwe makini na habari kama hizi!
nadhani watanzania hawajajua kwamba kwa nini tuna polisi na kwa bahati mbaya kuna watu wanatumia mwanya huu kufanya uchochezi kweli kw a maslah yao binafsi.hawa ni wanasiasa waliofilisika kutoka katika chama ambacho mnakijua vizuri.
 
Ndo wajifunze kuishi na watu, wewe umpige mtu virungu mchana kumbe umepanga kwenye nyumba yake na usiku unaenda kulala, aisee hata kama ni mimi nakutimua. Sasa mnaishi mtaa mmoja then unambutua halafu badaye iweje?
hivi wewe unadhani tuna haja ya kuwa na polisi katika jamii? kama wakiwepo, unadhani hawatakiwi kuwa na silaha yeyote,au wanatakiwa wawe nazo? kama wanatakiwa wawe nazo; ni silaha za aina gani unadhani wanatakiwa kuwa nazo na kwa nini? kama wakiwa nazo; unadhani zitakuwa ni kwa ajili ya nini kama sio kupigia watu (wanaovunja sheria halafu wakajifanya vijeba!)
 
nadhani watanzania hawajajua kwamba kwa nini tuna polisi na kwa bahati mbaya kuna watu wanatumia mwanya huu kufanya uchochezi kweli kw a maslah yao binafsi.hawa ni wanasiasa waliofilisika kutoka katika chama ambacho mnakijua vizuri.

Hapo nipo na ww mkuu, polisi alaumiwe kwa lipi?hv kweli hawajui majukumu ya polisi? Je polisi wakiagizwa kisha wakaidi unadhani nn kitatokea, unadhani polisi wanapenda kuwatesa ndugu zao? Ujue kuna wkt polisi hulipua mabomu ya machozi wakati huohuo machozi yakimtoka kwa ajili ya ndugu zake, AFANYE NN? ZAIDI YA KUTEKELEZA ALICHOAMURIWA, TAFAKARINI VIZURI
 
Polisiccm kwa kutumika kisiasa wanajikuta wananunua kesi..itafika siku nchi hii vita kuu ya wananchi ni dhidi ya hao jamaa ambao wanasahau kuwa nao ni wananchi wa Tanzania na hawajui wanajididimiza kwa kutetea uozo
 
tunakoelekea hakuna dalili njema ya mahusiano wanananchi na vyombo vya dola hususani jeshi la police

ni kweli kabisa mkuu lakini kwa kila nafasi aliyonayo mtu wa nchi hii atimize wajibu wake siasa kwenye kazi haitakiwi
 
kwa hali ilivyo sasa namshukuru Mungu kukosa kazi ya polisi Tanzania kwa ajili ya rushwa na unafiki ulijaa kwenye kundi hili la majambazi.
 
Hapo nipo na ww mkuu, polisi alaumiwe kwa lipi?hv kweli hawajui majukumu ya polisi? Je polisi wakiagizwa kisha wakaidi unadhani nn kitatokea, unadhani polisi wanapenda kuwatesa ndugu zao? Ujue kuna wkt polisi hulipua mabomu ya machozi wakati huohuo machozi yakimtoka kwa ajili ya ndugu zake, AFANYE NN? ZAIDI YA KUTEKELEZA ALICHOAMURIWA, TAFAKARINI VIZURI
Na si hivyo tu,suala la kujiuliza ni je? tunayajua majukumu ya polisi? kama ndio; tunadhani wanatakiwa wawe hawayatekelezi! kama ndio kwa nini! na kama wakitekeleza tunalalamika;je! tuna haja ya kuwa na polisi? ujue mpaka sasa bado mimi sijaona kosa la polisi wa Mtwara.Hebu kama kuna anaeliona aniambie.Na nawashangaa sana watu wanaowahamasisha raia wawe wanapambana na polisi. Najiuliza kama kweli wanafikiri kwa kutumia akili kama wanavyofanya watu wengine au ............
 
Kuwapiga polisi wanawaonea hao ni wajumbe mmesahau usemi wa mjumbe hauwawi?
 
Back
Top Bottom