GE2025 Polisi: Msitumike kama chanzo cha uchochezi na uvunjivu wa amani wa taifa

GE2025 Polisi: Msitumike kama chanzo cha uchochezi na uvunjivu wa amani wa taifa

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

DuaZaMama

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2025
Posts
1,882
Reaction score
4,129
Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani wa Wilaya ya Ileje, Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP) Kisbert Kapondo, ametoa elimu kwa waendesha bodaboda wa Kata ya Itumba Wilaya ya Ileje Mkoani Songwe akiwataka kuepuka kujihusisha na vitendo vya uvunjifu wa amani.

Akizungumza Oktoba 19, 2025 na wasafirishaji hao katika kijiwe chao, ASP Kapondo aliwaeleza kuwa wao ni wadau muhimu wa usalama barabarani na maendeleo kwa jamii, hivyo wanapaswa kuwa mfano wa kuigwa katika kutii sheria na kudumisha amani, hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi.

Aidha, ASP Kapondo aliwasihi wasitumika na watu wenye nia ovu wanaotaka kuvuruga amani kwa kutumia wao kama nguzo ya chombo cha uchochezi, huku akisisitiza kuwa Jeshi la Polisi halitasita kuchukua hatua za kisheria kwa yeyote atakayebainika kushiriki kwenye uvunjifu wa amani au kuvunja sheria kwa njia yoyote ile.

1761216921965.png


1761216939586.png
 
Back
Top Bottom