Polisi akipokea rushwa live



kwa usawa huu 1000/= unasema ni sadaka?ngoja tumwambie ngosha akuundie tume bila kusahau uandae nyaraka muhim za TITI ARA EI,

ok sikia ndgu,pesa inaweza kuwa ndogo kama ni mala moja kwa siku ila sio inapokuwa mala tatu,mfanp kwa watu wa daladala unakuta ndani ya safar moja anadakwa mala 4 na zaid!!
nakumbuka nilikuwa katika gari pale dsm nikitokea tegeta kwenda kariakoo tulikamatwa mala 5(tangi bovu,mwenge,victoria,magomeni hosptal na pale fire) na hao wote konda alienda na kitu mkononi......sasa jiulize wao huwa wanakuwa na huluma na wenzao?
 
Rushwa sisi ndio tunawapa, wakiikataa sisi ndio tutaumia. Besides, hiyo wanaenda kung'arishia viatu tu, kuwa mpole.
Kweli mkuu halafu ukute ni mshikaji wake wanajuana kampa ya maji yuko juani na hakuna sauti yoyote inayodai rushwa, au mimi sijasikia?
 
Wengi wao wanachukua kwa kutusaidia maana bila hivyo ni gari kituoni au mahakamani sijapenda kutoa huyo anaesaidia wakati yapo majambazi huko yanakula rushwa ya hatari na tunakua kimya...
 
Wanaume mda mwingine sijui wanakuaje hawajui kulindana kwenye shida, hyo kazi ya trafic ni ngumu sana wanakaangwa na jua mshahara wenyewe ni majanga. Mpeni kidogo ya kunywa azam soda siyo mbaya

Kuna mmoja mdigi flani trafic barabara ya mbeya iringa alinisimamisha nikakunjwa elfu kumi bandia nikampa wale huwa hawaiangalii wanaikunjia mfukoni wanaenda kuzihesabu nyumbani kwao
 
Imeruhusiwa kabisa elfu 5 ya kubrashi viatu
 
Adhabu hii inawahusu wote wawili aliyetoa na aliyopokea rushwa maana kutoa in kosa na kupokea ni kosa.
 
Ndio maana binadamu tunasifika kwa unafiki uliopitiliza.. Wengi wetu hapa tukikamatwa kwa makosa yaliyo dhahiri tunawabembeleza hao hao maaskari watuachie kwa kuwadakisha kitu kidogo.. Wenye ujasiri wa kutowabembeleza askari ili wasiandikiwe kosa ni almost nil.. Halafu leo tunakuja hapa tunawalaumu na kuwasema vibaya hao hao askari kwa makosa dhahiri tuliyoyafanya, lakini wakaamua kuchukua kidogo na kutuacha..

Mie ntaendelea kuwaheshimu tu, na kuzungumza nao pindi nikifanya kosa linalohitaji faini.. Uchumi wa kulipa 30 sina..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…