Polepole ana mgombea wake mfukoni?

Ojuolegbha

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2020
Posts
1,770
Reaction score
1,173
POLEPOLE ANA MGOMBEA WAKE MFUKONI?

Lilipoulizwa swali la huenda kupitishwa kwa mgombea mmoja kwenye kugombea nafasi ya Urais ikawa ni uoga wa kushindwa kwenye mkutano mkuu, Dkt. Dennis Muchunguzi anasema hakuna uoga wowote kwasababu wajumbe wa mkutano mkuu ambao ndio WAPIGA kura ndio waliamua wenyewe kumpendekeza mgombea ambaye ni Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa nafasi ya Urais na Dkt. Hussein Mwinyi kwa nafasi ya Urais wa Zanzibar, hivyo wazi halikutoka kwa mgombea.

Dkt. Muchunguzi ambaye ni mchambuzi wa masuala ya Siasa na Mwanazuoni alipoulizwa kuwa huenda Ndg. Polepole ana mgombea wake mfukoni akasema hajui mifuko yake.

Hayo yamezungumzwa kwenye Podcast ya Kikao cha Dharura na Kabwanga

Vipi wewe unadhani Ndg. Polepole ana Mgombea wake mfukoni?
 

Attachments

  • VID-20250720-WA0030(1).mp4
    19.7 MB
Kwa utafiti nilioufanya nathibitisha kusema huyu mama hawamtaki watanzania.Utaratibu uliotumika kumpitisha ni wa kinyume na utaratibu na waliolazimisha huo utaratibu ni wahuni tu kutoka msoga na lengo lao ni kuendelea kuwa washika remote
 
Vyovyote itakavyokuwa nafasi ya urais haipaswi kutolewa kwa kuhurumiana ni nafasi nyeti na muhimu sana katika kulipeleka taifa mbele. Hatupaswi kuwa na nafasi ya viti maalum linapokuja jambo nyeti la urais wa nchi, akae pembeni utaratibu sahihi wa kumpata mgombea urais apatikane kwa vigezo vya ubora unaotakiwa
 
Ukitekwa na magaidi katika ambush ukawekewa bunduki kichwani ukubali jambo, ukikubali, halafu ukawa umenusuru uhai wako, baadaye ukakubali kuwa pale nilikubali jambo kwa sababu nilikuwa nimetekwa tu, waungwana tutakuelewa.

Tutaelewa kuwa kunusuru maisha yako lilikuwa jambo muhinu kabisa, hayo mambo ya kusema uliyolazimishwa kusema, mandhali ushatetea uhai wako, tunaweza kuyarejea.

Kuhusu Polepoke kuwa na mgombea wake mfukoni, kila mtu anaruhusiwa kuwa na mgonbea wake mfukoni, au hata yeye mwenyewe kuwa mgombea kama amefikisha vigezo.

Hiyo ni haki ya kikatiba na kibinadamu.

Tatizo liko wapi?

Polepole hatakiwi kuwa na mgombea wake anatakiwa kum support mgombea wa Kikwete tu?
 
Fuateni katiba ya chama chenu acheni uhuni - polepole yupo sahihi 100%.

Ruhusuni wagombea wengine nao wachukue form za urais ili wapimane ubavu. mkishamoa mshindi wetu ndiyo mumlete wapambane na Tundu Antipas Lissu - the game changer.
 
Kwa utafiti nilioufanya nathibitisha kusema huyu mama hawamtaki watanzania.Utaratibu uliotumika kumpitisha ni wa kinyume na utaratibu na waliolazimisha huo utaratibu ni wahuni tu kutoka msoga na lengo lao ni kuendelea kuwa washika remote
Nje ya mada, we hujui ht maana ya utafiti achilia mbali unafanyikaje
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…