Hapa nakubaliana na nyinyi kuwa kompyuta hii ina matatizo mawili yaani bei na jinsi ya kuitumia (internet), Hata ukiwa unaishi kwenye nchi zenye speed nzuri ya internet bado unaweza ukawa sehemu ambayo huna internet labda ufanye teathering au uweke sim card ambapo ni gharama nyingine tena. Na kama umezoea 30 - 50 mb speed teathering inaboa mno mpaka uwe na 4G ambapo mpaka sasa ni ghali mno.
Nadhani Google wenyewe wanalenga kuzitangulia kampuni nyingine kwenye mafanikio ya cloud kwa miaka ya baadae, ndio maana wanaendelea kuzi-push computer hizi. Huenda teknolojia hii ikipevupa na kukubalika basi wao tayari watakuwa wameshazitangulia kampuni nyingi na OS zote kwa mafanikio ya kompyuta za mtindo huu. 4G LTE na teathering cost itakaposhuka huenda watu wakaanza kuzikubali ingawa sio kwa bei hii. hata hivyo zipo chromebook za bei rahisi mno. (£200)
Kwa sasa baadhi ya kampuni kubwa katika nchi zilizoendelea zimeanza kutumia cloud computing kwa kiwango kikubwa kwa sababu ya data safety na universal data access (yaani huhitaji kuwa kwenye computer fulani ili kuzipata data fulani) Google inazizidi kampuni nyingi za tech kwa future forecast.
Tusubiri ni wakati tu ndio utakatujulisha kama Google wataweza kuuteka ulimwengu wa laptop kama walivyofanya kwenye simu mpaka sasa.