Pinda azidi kuonesha makali

Pinda azidi kuonesha makali

2015tz

Member
Joined
Dec 10, 2014
Posts
24
Reaction score
5
sasa kuwahamisha Wakurugenzi wa Halmashauri
*Ni siku chache baada ya kuwahamisha wakuu wa wilaya


WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda ameendelea kukunjua makucha aliyoyaficha kwa muda mrefu na kuonyesha rangi yake halisi, baada ya kutangaza mpango wa kuwahamisha wakurugenzi waliokaa kituoni kwa muda mrefu na kujigeuza miungu watu.

Katika hatua yake hiyo Pinda amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza aandae orodha ya watumishi wa mkoa huo ambao wamekaa kwenye nafasi za ajira kwa zaidi ya miaka 10 na kumpelekea ili awahamishie vituo vingine.

Pinda ambaye aliwahi kuwa Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na baadaye kuwa Waziri Kamili katika Wizara hiyo, alikuwa mwiba mkali kwa watendaji wa halmashauri hatua iliyomfanya kuongoza kwa mafanikio wizara hiyo.

Hiyo ndiyo iliyolifanya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kulipuka kwa shangwe, vifijo na vigelegele wakati Rais Jakaya Kikwete alipowasilisha jina lake kwa Spika wa Bunge, Samuel Sitta wakati huo kumtangaza Pinda kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Pinda leo ametoa agizo hilo wakati akizungumza na viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Iringa waliofika kusikiliza majumuisho ya ziara ya siku sita ya Waziri Mkuu kwenye mkoa huo. Mkutano huo ulifanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi ulioko Mafinga, wilayani Mufindi.

“Tafuta wote waliokaa zaidi ya miaka 10. Ni lazima tuwabadilishe... niletee orodha mapema iwezekanavyo,” alisema Waziri Mkuu.

Alisema nia ya zoezi hilo ni kuongeza ufanisi kwani watumishi wakikaa sehemu moja kwa muda mrefu wanakuwa butu kwa kukosa ubunifu kwenye kazi zao, wanaota mizizi na kugeuka kuwa chanzo cha matatizo katika baadhi ya sehemu.
Alimtaka pia Mkuu huyo wa Mkoa pamoja na timu yake wasimamie vizuri ukusanyaji wa mapato ili kuongeza kiwango cha mapato cha mkoa huo. “Na siyo hilo tu, simamieni vizuri matumizi ya fedha zilizopangwa kwenye miradi mbalimbali ili kuleta maendeleo ya kweli kwa wananchi mnaowaongoza,” alisisitiza.
 
Sawa kuwahamisha watumishi inaweza kuwa ni jawabu lakini huwa si kutatua tatizo kwa kudumu.
Mtumishi akikosa aadhibiwe kwa haki. Kumhamisha mtumishi siku hizi ni dili kwa ajili kupata posho ya uhamisho.
 
Silly.
Aache kuhangaika.
Kama vipi akagombee ukamanda wa polisi ili aendelee kutupiga tuu.
Waziri mkuu ataagiza wanao ua albino nao wauwawe hata bila kufikishwa mahakamani?? Na analia na kulia! Baada ya hapo,kimyaaa. Albino wanauawa yeye anapanga wakurugenzi,ameshasahau jozi lake bungeni tayari.
Kama haitoshi,ana agiza wanajeshi wapige watu ili wasihoji kitu!
Leo kukurukakara anataka urais!
CCM mpitisheni Pinda kugombea urais ili mjue tunampenda kwa kiasi gani!
 
Mizengo oyeeee, natumaini na huyu wa kwetu ataondoka, alishakuwa hspa kwa miaka 15 sasa mpaka katufanya tuichukie serikali
 
Heshima kwake Mh Waziri Mkuu naamini kwa hatua hiyo itawafanya watenadji wazembe wawe makini kiutendaji na kurudisha nidhamu ya kazi serikalini.
 
Mkuu unataka kuwaaminisha nini wana JF???kuwa Pinda ni kiongozi bora eti?

Hivi tangu nchi hii inapata Uhuru aliwahi kutokea waziri mkuu wa hovyo kama Pinda?
 
makali yake ni ile amri ya wapigwe tu inayotumiwa na policcm, nothing else
 
acha kuongea maneno ya ovyo ovyo tu pinda amekua wazir mchapa kaz kuwai tokea tanzania hiii
 
Last edited by a moderator:
Maamuz magumu na mtu makin mtu muadilifu yaheshimiwe piga tu kwa maana ya kuheshimu mamlaka chadema waliipanda kichwa serikal
 
silly.
Aache kuhangaika.
Kama vipi akagombee ukamanda wa polisi ili aendelee kutupiga tuu.
Waziri mkuu ataagiza wanao ua albino nao wauwawe hata bila kufikishwa mahakamani?? Na analia na kulia! Baada ya hapo,kimyaaa. Albino wanauawa yeye anapanga wakurugenzi,ameshasahau jozi lake bungeni tayari.
Kama haitoshi,ana agiza wanajeshi wapige watu ili wasihoji kitu!
Leo kukurukakara anataka urais!
Ccm mpitisheni pinda kugombea urais ili mjue tunampenda kwa kiasi gani!

pinda alilia bungen kutofuraishwa na mauaji ya albino na kama bunge lingeridhia msombi yake hakikia sheria kal zingetungwa kwa wanao waua albino na tatizovlingekua limeisha mara moja pinda n mtu makin anae tambua nn ana kifanya tunajua mna mtaka yule iliiwe rais kumtandika jukwan na ccm makin haita wap yule mnae mtaka ili mumpige jukwana na maufisad yake ccm itaeleta kiongoz mwenye sifa za pinda
 
toeni hapa siasa za kinafiki alikuwa wap siku zote?
 
acha kuongea maneno ya ovyo ovyo tu pinda amekua wazir mchapa kaz kuwai tokea tanzania hiii

Vituko haviishi duniani hata pinda mwenyewe anajua kuwa ni dhaifu hivyo kusema ni mchapakazi anajua unamsanifu
 
Last edited by a moderator:
Mkuu unataka kuwaaminisha nini wana JF???kuwa Pinda ni kiongozi bora eti?

Hivi tangu nchi hii inapata Uhuru aliwahi kutokea waziri mkuu wa hovyo kama Pinda?

Wew acha upuuzi, Huwez mfananisha Waziri Mkuu Pinda, na huyo Lowasa wako,
 
Vituko haviishi duniani hata pinda mwenyewe anajua kuwa ni dhaifu hivyo kusema ni mchapakazi anajua unamsanifu

Acha kuongea utumbo wewe Njaa Mbaya sana kama jina lako, thibitisha udhaifu wa Waziri Mkuu. Waziri Mkuu Pinda amejitahidi kurejesha heshima ya serikali
 
Wew acha upuuzi, Huwez mfananisha Waziri Mkuu Pinda, na huyo Lowasa wako,

Kweli hawafanani kabisa huyu mzee wa kulialia yule mzee wa amri tu!halafu hii tabia ya kumchgulia mtu upande wa kuwa umeitoa wapi?au ndivyo ulivyoaminishwa kuwa huwezi kuona upungufu wa huku mpaka uwe kule???
 
Back
Top Bottom