Pinda ameichagua Mtwara!

Pinda ameichagua Mtwara!

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,138
Waziri Mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda yuko mkoani Mtwara. Amekwenda kiserikali kushughulikia mgogoro wa gesi asilia huko. Taarifa zinaonesha kuwa Waziri Mkuu Pinda amefanya mikutano mbalimbali na wadau wa kijamii na kisiasa mkoani humo.

Waziri Mkuu Pinda anafahamu vyema kilichompeleka Mtwara. Pia,anafahamu jinsi ya kuwasilisha maoni yake kwa utatuzi wa mgogoro huo. Mh Pinda anajua fika kuwa wana-Mtwara hawataki sana maneno kwasasa.Wanahitaji matendo-utekelezaji wa ahadi moja baada ya nyingine juu ya gesi asilia Mtwara.

Waziri Mkuu Pinda,anajua fika kuwa sera ya 'Gawa na Tawala' huko Mtwara haifai kwa sasa. Sasa inahitajika 'Tawala kimatendo'. Watu wa Mtwara wanahitaji kutumia ipasavyo nafasi yao hii adimu kusikilizwa na kutekelezewa ahadi zao kwa ustawi wao.

Binafsi,siamini kama wanasiasa na viongozi wa kijamii wanaofanya mikutano na Mh Pinda wanaweza kuwaambia kivingine wana-Mtwara waliowaaminisha tayari kwanza wako nao pamoja na 'Gesi kwanza,siasa baadaye'. Wakiwageuka,itakuwa hatari zaidi.

Naamini kuwa Waziri Mkuu Pinda,aliyetoa sadaka hata Mkutano wa Bunge ulioanza leo Dodoma,atafikia muafaka na wana-Mtwara juu ya sintofahamu hii. Pinda ana uwezo mkubwa wa kuanzisha safari ya kimatendo ya Serikali juu ya kadhia hii. Kweli Mh Pinda ameichagua Mtwara!
 
Lakini, pamoja na Pinda kuichagua Mtwara, hivi ana uwezo wa kubadili mfumo ambao umekuwa ukitawala utendaji wa viongozi wetu kwa miongo yote hii mitano? Kwa maana, ukisoma kwa makini aliyoambiwa Pinda na wale aliokutana nao huko Mtwara utabaini wazi wazi kuwa tatizo hasa si gesi hii ya sasa, haya ya gesi ni matokeo ya matatizo ya wana-Mtwara ambayo yalianza tangu enzi za ukoloni. Pinda anaweza kuyarekebisha hayo kwa ziara ya siku hizi chache?
 
nadhnani kwa sasa hali ni tete wananchi na watawala wanahitaji muda kwa hiyo mradi usitishwe kwaanza mpaka pale kutakapokuwa na maelewano vinginevyo itakuwa imetangazwa ukanda wa vita na hii itakuja kusambaa maeneo mengine ukiangalia saikolojia ya wananchi wengi wanawaunga mkono wana mtwara
 
nadhnani kwa sasa hali ni tete wananchi na watawala wanahitaji muda kwa hiyo mradi usitishwe kwaanza mpaka pale kutakapokuwa na maelewano vinginevyo itakuwa imetangazwa ukanda wa vita na hii itakuja kusambaa maeneo mengine ukiangalia saikolojia ya wananchi wengi wanawaunga mkono wana mtwara
Ni kweli Mkuu
 
Lakini, pamoja na Pinda kuichagua Mtwara, hivi ana uwezo wa kubadili mfumo ambao umekuwa ukitawala utendaji wa viongozi wetu kwa miongo yote hii mitano? Kwa maana, ukisoma kwa makini aliyoambiwa Pinda na wale aliokutana nao huko Mtwara utabaini wazi wazi kuwa tatizo hasa si gesi hii ya sasa, haya ya gesi ni matokeo ya matatizo ya wana-Mtwara ambayo yalianza tangu enzi za ukoloni. Pinda anaweza kuyarekebisha hayo kwa ziara ya siku hizi chache?
Ni swali la msingi sana Mkuu
 
Kuna kauli inazidi kusambaa kwamba "kama ndege yake ina nafasi basi akiondoka asiumache Kanali SimbaKalia"...niujumbe tosha kwamba m-metudharau vya kutosha, Hatuhitaji tena siasa, bali ni utekelezaji, hata hapo site ya Dangote ni pori tupu tuna mashaka kuingizwa mkenge kwa hili!!
 
Kuna kauli inazidi kusambaa kwamba "kama ndege yake ina nafasi basi akiondoka asiumache Kanali SimbaKalia"...niujumbe tosha kwamba m-metudharau vya kutosha, Hatuhitaji tena siasa, bali ni utekelezaji, hata hapo site ya Dangote ni pori tupu tuna mashaka kuingizwa mkenge kwa hili!!
Si mchezo! Wapi THE BIG SHOW atupe taarifa?
 
Last edited by a moderator:
Kila jambo,litafutie busara ya kulimaliza -kila la mwana wa mkulima.
 
Waziri Mkuu kama anaenda kumaliza tatizo basi yafaa aanze na wale wote waliotoa kauli kuwa wana Mtwara wahaini zaidi ya hapo hakuna atakachopata maana kufanya mikutano na viongozi bado hakutatui tatizo zaidi ya kuitisha mkutano na awaambie wananchi kile wanachotaka kusikia,vinginevyo hakuna la maana analofanya hujko.
 
nadhnani kwa sasa hali ni tete wananchi na watawala wanahitaji muda kwa hiyo mradi usitishwe kwaanza mpaka pale kutakapokuwa na maelewano vinginevyo itakuwa imetangazwa ukanda wa vita na hii itakuja kusambaa maeneo mengine ukiangalia saikolojia ya wananchi wengi wanawaunga mkono wana mtwara
Ni sawa kabisa kwani wananchi wa sasa kinachotafutwa ni starting point na Mtwara huenda ikawa sehemu ya kuanzia kuna uwezekano hii ikasambaa sehemu nyingine pia,tatizo watu wamepigika na maisha huku wengine wakineemeka.Hii ni hatari serikali ijitathmini vipya,watu hawataki bra bra wanataka maendeleo yanayoonekana siyo ya kwenye makaratasi
 
Waziri Mkuu kama anaenda kumaliza tatizo basi yafaa aanze na wale wote waliotoa kauli kuwa wana Mtwara wahaini zaidi ya hapo hakuna atakachopata maana kufanya mikutano na viongozi bado hakutatui tatizo zaidi ya kuitisha mkutano na awaambie wananchi kile wanachotaka kusikia,vinginevyo hakuna la maana analofanya hujko.
walikosea sana kuwaita wanamtwara ni wahaini je wakiamua kuwa wahaini kweli nchi itaenda kweli?
 
the big analijua hili....ngoja atafunguka muda si mrefu...!!

mkuu sizinga naungana nawewe moja kwa moja kiongozi,hilo ndilo linaozungumzwa,simbakalia hana tena nafasi ya kukaa meza moja na wamakonde,pinda anashauriwa tu akiondoka aondoke nae,katika tamko la shura ya maimam na muungano wa madhehebu ya kipentekoste mtwara kote huko ameainishwa ya kwamba hatakiwi,by the way pinda lazima atambue suala si tu kuishia kuongea na hao viongozi tuh,wananchi wanachotaka kuskia ni kusitishwa kwa mradi huo wa ujenz wa bomba kutoka kwake,kwa sasa mbona kuko tulivu sana?kuko cool na watu wamekaa chonjo kusubiri kauli yake,awe makini watu wameshastuka sasa.
 
Teh..teh..Pinda nikupinde..mutoto ya mkulima toka Sumbawanga..karibu Mtwara.. 149554_543901958967228_244143237_n[1].jpg 149554_543901958967228_244143237_n[1].jpg
 
walikosea sana kuwaita wanamtwara ni wahaini je wakiamua kuwa wahaini kweli nchi itaenda kweli?
Ndio tatizo la viongozi wetu kukurupuka na kutoa matamko bila kufikiri madhara yake,tumeona nguvu ya umma kule Masasi na kile kilikuwa kikundi tu cha watu,je leo wananchi wakiamua kutumia nguvu zao hakuna atakayesalimika nchi hii.
 
Pinda hana lolote sanasana atawaambia wanamtwara waachane na gesi wafuge nyuki.ajiandae kutolewa mkuku la sio meno hanaa
 
​Ni wakati muafaka sasa kujadili katika katiba mpya umuhimu wa wananchi kuchaguwa wakuu wao wa mikoa ambao wanaelewa matakwa na shida ya wananchi wa mkoa husika!
 
Kuna kauli inazidi kusambaa kwamba "kama ndege yake ina nafasi basi akiondoka asiumache Kanali SimbaKalia"...niujumbe tosha kwamba m-metudharau vya kutosha, Hatuhitaji tena siasa, bali ni utekelezaji, hata hapo site ya Dangote ni pori tupu tuna mashaka kuingizwa mkenge kwa hili!!

Hawa watu wana lao jambo, ni kweli huyo Dangote wanaetangazia dunia ameanza ujenzi Msijute , wapi? pori tupu pale.

Mungu aingilie kati kubadili mawazo ya watu,tupumzishe hawa watu 2015...... too tired.
 
Back
Top Bottom