Pikipiki ni kifo

Kiranja Mkuu

JF-Expert Member
Feb 18, 2010
4,059
4,055
Pikipiki zaua 181 kwa miezi minne


JUMLA ya watu 181 wamefariki dunia kwa ajali za pikipiki katika ajali 1,414 zilizotokea kote nchini katika kipindi cha miezi minne kuanzia Januari, huku zikiacha majeruhi 1,206, imeelezwa.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam jana wakati akitangaza mabadiliko ya tarehe za kuadhimisha Wiki ya Usalama Barabarani, Mwenyekiti wa baraza linalosimamia masuala hayo, Abbas Kandoro alisema ajali nyingi zilitokana na mwendo wa kasi.

"Ajali nyingi zinatokana na abiria kushabikia mwendo wa kasi na wengi kutovaa kofia za kujikinga kichwa," alisema Kandoro, ambaye pia ni mkuu wa mkoa wa Mwanza.

Alisema ndio maana kaulimbiu ya mwaka huu ni "ajali inaua, inajeruhi; usishabikie mwendo wa kasi; mpanda pikipiki vaa kofia ngumu" ambayo aslisema inalenga kuwaelimisha wapandaji wa usafiri huo kuwa makini.

Ongezeko hilo la ajali linaonekana kwenda sambamba na ongezeko la vyombo hivyo vya usafiri, ambavyo katika mwaka mmoja uliopita pikipiki zimekuwa moja ya vyombo vinavyotegemewa sana kwa usafiri wa abiria.

Ongezeko la idadi ya pikipiki linaonekana kuchochewa na unafuu wa bei tangu vyombo hivyo vianze kuingizwa kutoka China na nchi nyingine za Asia. Lakini mara kadhaa polisi wamekuwa wakilalamika kuwa waendeshaji wa vyombo hivyo hawana leseni wala ujuzi wa kutosha na hivyo kufanya operesheni za mara kwa mara kuwakamata.

Akielezea mabadiliko ya tarehe za kuadhimisha siku hiyo, Kandoro alisema katika mwaka huu ambao ni wa kueleke uchaguzi mkuu, siku ya usalama barabarani imebadilishwa na kufanyika mwezi Julai na kwamba kitaifa itanyika mkoani Tanga.

Kandoro alisema wamebadilisha siku hiyo kutoka mwezi Septemba kwa ajili ya kupisha shughuli za uchaguzi mkuu na kwamba wiki ya usalama itafanyika kuanzia Julai 19 hadi 24 ambapo itakwenda sambamba na zoezi la ukaguzi wa magari.

Alisema polisi wa usalama barabarani wataanza ukaguzi wa magari katika wiki hiyo na kuwataka wamiliki wa magari kuhakikisha wanayapeleka ili yakaguliwe na kubandika stika.

“Kwa jiji la Dar es salaam ukaguzi utafanyika katika vituo vya Polisi trafiki ,Ikiwa ni Trafili Ilala, Temeke,Oysterbay na mikoani watapeleka vituo vya polisi wa usalama barabarani,” alisema Kandoro.
 
kweli na tatizo kubwa la hawa waendesha pikipiki ni uzoefu,kasi, fujo na kutozoea chombo chenyewe mtu anajifunza asubui mchana anabebe abiria na anapita barabani kwa spidi kubwa unafikiri kinatokea nn na miundo mbinu yetu mibovu unakuta mtu anapita mainroad wakati kuna service road nzuri tu pembeni lakini wapi
 
Hawa waendesha pikipiki wengi wao (hasa wanaoendesha hizi pikipiki za biashara za kichina) hawazingatii sheria za barabarani na wanaendesha kwa mwendo kasi utafikiri wapo mashindanoni.
 
kama tunajua hili ni tatizo kwa nini tusipige marufuku pikipiki kutumika kama chombo cha usafiri wa umma?
 
Dawa ni sisi wananchi kukataa kutumia pikipiki kama chombo cha usafiri wa umma.

Utakataaje kutumia pikipiki wakati hujapewa usafiri badala ya pikipiki?? kwingine daladala hazifiki zaishia njiani utaachaje kupanda pikipiki??
 
Mbona kwetu Zenji twazitumia na hakuna ajali atii.... nyie wabara vipi tuwaletee madereva ama ?
 
Nimeona matrafiki wameanza zoezi la kukagua leseni zao, kama mapolisi watakuwa serious hii kitu itaisha, mtu hana leseni ya kuendesha pikipiki halafu anapakia abiria tena hadi watano. Tutakwisha!! Na nyie abiria mnakubalije kutungwa kama senene jamani????
 
kama tunajua hili ni tatizo kwa nini tusipige marufuku pikipiki kutumika kama chombo cha usafiri wa umma?

tutakuwa tunawanyima haki watu wanaoendesha pikipiki kimakini na wanaotumia kama chombo chao cha usafiri kila siku,wendawazimu wachache wasisababishe tuhukumu watu wengine ambao wako makini.
 
Jamani tatizo sio pikipiki, tatizo ni madereva wengi wao wawapo barabarani huwa kama akili zao hazipo kwa kazi wayofanya kuwa wamebeba abiria hivyo wanapenda kuji-show barabarani, kuovateki kwa masifa, hawana habari kuwa amebeba roho ya mtu na yake pia, yaani utafikiri wanavuta bangi wakati mwingine nashindwa hata kuwajaji, wanapenda masindano yasiyo na faida na wengi wao hawana taaluma ya matumizi ya barabara na alama zake ili mradi kajifunza pikipiki basi hata leseni hawana. hilo linachangia kwa kiasi kikubwa ajali nyingi za pikipiki.
 
Back
Top Bottom