Pi (3.14159...) Katika Biblia

Iselamagazi

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2011
Posts
6,083
Reaction score
6,234
Hi everyone.

Katika kitabu cha Wafalme (1Fal 7:23-26), tunasoma kuwa Mfalme Sulemani aliagiza mtu mmoja aitwaye Hiramu kutoka Tiro, kutengeneza beseni(?) kubwa la maji (mfano wa mcheduara) kwa ajili ya kupamba Hekalu Jipya.

Ni wazi kuwa ili utengeneze chombo chenye umbo la mcheduara (cylindrical shaped object) itakulazimu angalau ujue matumizi ya Pi.

Ebu tuangalie vipimo alivyotumia huyu Hiramu mtu mwenye hekima na akili aliyetengeneza beseni(?) kubwa la shaba.

Kipenyo = mikono 10 (180 cubits), urefu kwenda juu = mikono 5 (90 cubits), Pi = 3.14159..., mzingo (circumference)?

Mzingo = Pi*kipenyo au 2*Pi*nusu kipenyo.
= 3.14159*10 = 31.4159 (appr. 30)

"Tena akafanya bahari ..., na uzi wa mikono therathini kuizunguka kabisa". Rejea 1Fal 7:23-26.

Swali la kujiuliza: hivi huyu Hiramu alijuaje kuwa ni lazima kutumia Pi enzi zile za zamani kabla ya sayansi na maarifa havijashika kasi kubwa?

(Ikumbukwe, Hiramu aliishi miaka 1011 BC)
 
Angalizo: Kitabu cha Wafalme, siyo mathematical text book wala architectural manual.
Si dhumuni la Kitabu cha Wafalme kufundisha thamani halisi ya Pi, lengo hasa ni kuonyesha namna Mfalme Sulemani alivyojitahidi kujenga Hekalu Jipya lakini pamoja na hayo bado tunapata picha ya scientific facts ktk Holy Scriptures!
 
Sorry kama hutapata jibu la moja kwa moja,kuna mistari inayosema kwamba Mungu aliwashushia ufahamu maarifa kwa kazi hiyo akiwemo huyo na wengine.

Japo Sikumbuki mstari na sura kamili,
 
Jambo la msingi kabisa hapa ni Je Hiramu alijuaje kutumia Pi wakati huo?
Hapa nataka kukujibu hivi;
ni wazi kabisa kila kitu kimeanzia kwa Mungu. Biblia inasema Kumcha Bwana ndiyo chanzo cha Maarifa. Suleiman alimcha Bwana akapata maarifa hayo.
Pili; Hivi ni baadhi tu ya kukujulisha kuwa Biblia ni Neno lenye Pumzi ya Mungu
Nawasilisha
 

There is no evidence that he used Pi katika ukokotozi wake, huenda alitumia very basic means!
 
hakuna jipya chin ya juu vyote vilikuwepo, kanun nying ni majina ya watu labda wao walianzisha ila walitumia majina mengine kukokotoa
 

Hata hivyo angalia vizuri hiyo hesabu ya Hiramu, the guy was off, na naweza kusema kuwa huo mcheduara wake haukuwa perfect; Kama diameter ilikuwa 10 cubits, na mzingo 30 cubits basi kama ni kutumia pie alitumia 3.0!...kitu ambacho hakipo. Kwa hakika mzingo ulitakiwe uwe 31.4 cubits. Au mimi nimeanza kusahau hesabu za primary wakuu?
 

Kumbuka kwamba Farao na wataalam wake walishakokotoa Pi zaidi ya miaka elf 4 iliyopita (miaka mingi kabla ya solomon)!! Kwa hiyo tusirahisishe tu kwamba walifunuliwa na Mungu, TUJADILI KISAYANSI ZAIDI. Hiyo fomula ni ya kitambo sana kabla ya biblia na ukristo kwa ujumla.
 
hakuna jipya chin ya juu vyote vilikuwepo, kanun nying ni majina ya watu labda wao walianzisha ila walitumia majina mengine kukokotoa

Hakuna anayedaiwa kuinvent pi mkuu, ni ya kitaambo sana kabla hata baba yake solomon hajakanyaga juu ya nchi!
 

Fikiria vizuri hivi unajua hiyo ilikuwa ni mwaka gani? Kwanini mzingo usingekuwa 50 au 100 au 10 lakini ukawa 30 ambayo ni karibu kabisa na 31.4? The guy was brilliant coz pi imekuja kugundulika very far from then na haya ndio yale ya kina Da Vinci anachora mchoro ambao hata yeye hajui ni nini but tunakuja kutumia miaka mingi sana baadae.
 

Si kweli Mkuu, wakati Solomon anajenga hekalu lake Wagiriki na waMisri wa kale walishajua pi looong before Solomon was born!
 

Kosa kubwa ulilolisema katika swali lako ni kuwa pi ilijulikanaje zama za kabla ya sayansi? Nitakupa mfano, uhandisi wa majengo uliotumiwa kujenga mapiramidi ya Misri ulikuwa ni wa hali ya juu sana. Mapiramidi yalijengwa kabla ya Musa kwa sababu Musa baadaye ndiye aliwaondoa Wana wa Israel katika utumwa uliowafanya kujenga mapiramidi hayo. Na Musa ndiye aliyeandika vitabu vitano vya Agano la Kale (Mwanzo, Kutoka, Walawi, Hesabu na Kumbukumbu ya Torati).

Mimi Biblia yangu inasema hivi: Wana wa Israel waliondoka Misri 1520 BC. Na Mfalme Suleman alitawala 970 BC.

Sasa nikuulize, hiyo sayansi unayoizungumzia ilianza lini? Kama unazungumzia mwanzo wa sayansi iwe pale Bwana wetu Yesu Kristo alipopeleka Fadhila zake nchi za Magharibi, basi unazungumzia maugunduzi ya Wanasayansi wa leo wakiwemo Mathematicians na Physicists uliowasoma darasani. Baada ya Mwanakondoo aliyechinjwa kutawazwa kama ilivyo katika Ufunuo wa Yohana Aya ya 4, Aya ya 5 na Aya ya 6 ndipo dunia ikajaliwa sayansi na teknologia ya magari, treni na ndege na kuifanya dunia kuwa ndogo sana.

Lakini sayansi hii ilikuwa ni mwendelezo wa maarifa ambayo yalikuwepo tangu zama za kabla ya kuja kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Kulikuwa na refinements kulingana na mahitaji makubwa ya kuenezwa kwa neno kutoka Ulaya kwenda dunia yooote zaidi ya Israel. Kina Vasco daGama, kina Marcopolo, sema wewe na hao wengine.

Kwa hiyo pi ilikuwepo kabla ya Yesu Kristo.
 
There is no evidence that he used Pi katika ukokotozi wake, huenda alitumia very basic means!

Sema tu, alitumia Pi bila kujua kutokana na uzoefu wa miaka mingi akifanya kazi ya uashi.
 

Duh hivi Tanzania/Tanganyika ilikuwepo wakati huo? Nani alikuwepo? Hata historia ya kile alichokifanya haikuwekwa/haipo?? Sijui kabila langu lilikuwepo (Nyamwezi)???
 
kwa wagunduzi na watafiti ng'amueni hapa

kwa mtazamo wangu sisi wanadamu ni waungu hivyo tuna uungu ndani yetu
kwaini tulipuliziwa pumzi ya Mungu hivyo tuna maarifa, hekima na uungu wa
kufanya kitu kikawepo, ila hatujaamua kufanya hivyo
 
That is why non theists are perplexed when we talk about Omnipotent God.
 

Bado sijajua sababu iliyosababisha nikashindwa kukuelewa ........!!!!!!!
 
Bado sijajua sababu iliyosababisha nikashindwa kukuelewa ........!!!!!!!

Uliuliza kama pi ilikuwepo kabla ya sayansi? Jibu langu ni sayansi ilianza lini? Sayansi ilikuwepo hata kabla ya Musa,ndiyo nimekupa tangu kipindi cha kujengwa mapiramidi. Sayansi ya sasa ndiyo unayotaka iitwe sayansi lakini ni mwendelezo tu wa sayansi hiyo hiyo iliyokuwepo ndani ya Ufalme wa Mungu. Baada ya fadhila za Bwana wetu Yesu Kristo kusambaa nchi za magharibi mahitaji yalikuwa ni mengi na mapana zaidi duniani. Dunia ilijaa Mataifa Teule tofauti na hapo awali ambapo Taifa Teule lilkuwa ni Israel tu. Je unjua Wazungu walivyokuwa wanaishi kabla na baada ya Ukristo?
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…