Pesa za Escrow zatumika kampeni za Lowassa

Pesa za Escrow zatumika kampeni za Lowassa

fishseller

Member
Joined
Jun 13, 2012
Posts
30
Reaction score
19
Ndugu zangu, hili wazo limeniijia kichwani baada ya gazeti la Mtanzania kuandika habari kuwa mwenyekiti wa kamati ya bajeti Andrew Chenge amejiuzulu nafasi yake ya uenyekiti wa kamati ya bunge ya bajeti kutokana na kuhusishwa kwake na kashfa ya Escrow.

Wote tunafahamu kuwa Chenge ni mshauri na mfadhili mkubwa wa kampeni za Lowassa na kuna mpango kwenye kambi ya Lowassa ya kumfanya waziri mkuu kama wakipata ushindi baada ya uchaguzi mkuu.

Wiki mbili zilizopita, kundi la Lowassa liliwaonga wajumbe wa mkutano mkuu shilingi milioni mbili kila mmoja kama zawadi ya sikukuu ya Krismasi.

Kuna wajumbe takribani 2,300 kwahiyo Lowassa atakuwa ametoa zaidi ya shillingi bilioni 2.

Swali ambalo wengi wetu hatujiulizi ni kwamba hizi fedha zinatoka wapi na atakapoingia madarakani atazilipa kutoka wapi. Je, fedha alizopewa Chenge zinatumika pia kuwaadaa watanzania?
 
Team-Lowasa ni genge la wanyang'anyi tu hili.

Don't try it at home!
 
Acha siasa za kukafshiana. hizo milioni mbili kwenda kwa kila mjumbe una uhakika gani nazo? Siasa mbovu hiyo. Thibitisha basi.
 
acha siasa uchwara za kumuhusisha mweshimiwa na madudu yenu,mwanzo mwisho wa escrow saga wapi alipotajwa lowassa? au kisa tu mnaona nyota imeng'aa mnaleta ubwabwajaji wa maneno? endeleeni kusema sie tunachanja mbuga..magogoni hiyoo,mwezi wa kumi kinaeleweka
via TEAM lowassa
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom