Pesa anazogawa Rais Magufuli kama njugu anazipata wapi? Nani kaziidhinisha?

britanicca

JF-Expert Member
May 20, 2015
16,288
33,948
Nimefuatilia kupitia YouTube yanayoendelea huko Tanzania, hasa kwenye ziara za mkuu wa nchi,

Napenda jinsi anavyoonekana kuguswa na matatizo ya watanzania hasa wanaomlilia,

Kuna kina mama wengi wameonewa, kuna watoto yatima na maskini wanaonewa na kudhulumiwa,

Nimeona video zao zinasikitisha
Mpaka machozi yanaweza kutoka,
Rais kusema kweli
Nimefurahishwa na kitendo chake kuwafariji wajane naa wazee wanaonyanyasika kwa kuwagawia Hela moja kwa moja,

Nina maswali machache

1. Hela hiyo inakuwa imeidhinishwa na nani mpaka kuigawa hivo? Au tutegemee mwaka mwingine C.A.G kutaja trillion nyingine ambayo haionekani imeenda wapi?

2. Au ni makato ya mshahara wake na aliowateua katika kutumia mishahara yao kutatua matatizo ya wanyonge? Maana kwa taarifa zisizo rasmi rais Ana posho ya 15,000,000 kila mwezi, hivo kama anatumia mshahara wake hakuna shida,
Mkuu mleta mada, rais analo fungu la mengineyo, linafika milioni 100 kwa mwezi. Inategemea na aina ya maisha ya mtu mwenyewe.

Marais wengine hizi fedha walikuwa wananunulia masuti na kuhonga madada warembo wa mijini. Wengine ndio aina ya Ngosha, anashiriki moja kwa moja kwenye kuchangia mambo mbalimbali.

3. Je Rais hujui kwamba wajane na watu wenye matatizo kama ya hao unaowapa hela wapo chungu nzima Tanzania??
Na so wote watapata fursa ya kukutana na wewe kukueleza, wengine hautafika maeneo walipo,

4. Vipi usalama wa huyo unayemkabidhi Hela hadharani, si atavamiwa?

Pendekezo langu
A. Uwepo mfuko maalumu wa kuwasaidia watu hawa nchi nzima kama TASAFF walivokuwa wanasaidia wazee kuliko kugawa tu Hela mkononi, maana hata ambao hutawafikia watafikiwa kama sheria na utaratibu wa mfuko ulioanzishwa itafuatwa,

B. Viongozi wawajibike wasisubiri ziara ya rais ndo wanaanza kuhaha na kujifanya wanachapa kazi wakati kama wangekuwa wanachapa kazi matatizo kama hayo yangepungua kabisa,

C. Rais wangu angaza watu wanaokiuka na kuwanyanywasa wajane kiwepo kitengo maalumu kila.wilaya cha kusikiliza kero hizo, au ianze mahakama ya kutetea wanyonge kama ilivyo ya mafisadi,


Mwisho mi sijapendezwa na utaratibu wa kugawa hela mkononi, maana unapompa huyo mjane au kipofu unamuweka katika hatari zaid ya kuvamiwa usiku na majambazi kuzichukua Hela ulizompa, angalau ungekua unawapa kwa siri, japo najua kwa siri haitakupa sifa kama lengo lilivyo,

Britannica

Hapo jana iliripotiwa kwamba Rais Magufuli kamlipia faini Mchungaji Msigwa, ambaye mbunge wa CHADEMA kutoka huko Iringa.

Alimlipia shilingi milioni 38! Rais wetu huyu amekuwa na mazoea ya kuwapa watu hela akiwa kwenye ziara zake huko mikoani. Huwa anatoa kiasi tofauti tofauti. Huwa anatoa laki tano, milioni moja, mbili, n.k.

Jana ndio katoa hiyo milioni 38. Kwa wanaojua, huyu Rais wetu huwa anazitoa wapi hizo pesa?

Kwenye akaunti yake? Yeye ana pesa nyingi sana? Huwa anaenda hazina na kuchota pesa ambazo anakuja anawapa wanaomuomba?

Yawezekana labda kweli ana hela nyingi. Yaani pesa zake mwenyewe zilizopo kwenye akaunti yake/zake. Kama ni hivyo basi sawa. Binafsi siwezi kumpangia mtu matumizi ya pesa zake.

Miaka takriban 13 iliyopita niliwahi kuuliza kama kuna mtu anaujua mshahara wa Rais wa Tanzania. Nilianzisha uzi humu JF kuhusu mshahara wake.

Mpaka sasa sijawahi kuona mtu mwenye taarifa sahihi kuhusu jambo hilo kwani kiasi ambacho hutajwa si kimoja. Hiyo ni ishara kwamba hakuna ajuaye kwa uhakika.

Milioni 38 ni pesa nyingi sana kwa mtu kuzitoa tu kirahisi rahisi namna hiyo. Ndio hapa najiuliza, huwa anazitoa wapi hizo pesa?


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binafsi sijapenda staili ya Mheshimiwa Rais ya kutafuta kupigiwa makofi kwa kuwarubuni wananchi kwa fedha keshi anazogawa ili aonekane anawapenda sana. Jana nimeshuhudia akimpa mlemavu pesa taslimu Tsh. milioni moja. Sisemi mlemavu hastahili ila utaratibu huu kwa mtu ambaye ni Rais si wa kistaraabu kabisa.

FB_IMG_1488490138540.jpg


Mambo ninayojiuliza ni haya:-

1. Fedha hizo zinatoka mfuko gani?

2. Je kama kuna mfuko ambao Rais akiwa na ziara anazichota apendavyo , kwanini kusiwe na utaratibu ili watu wengi wafikiwe kuliko kumpa mtu mmoja? Kuna walemavu wangapi mitaani?

3. Je lengo la kampeni ya kugawa fedha keshi ni lipi? Je ni kuonyesha ikulu ina pesa au jeuri tu?

Maswali ni mengi sana, ila naona hapa wananchi tunaibiwa. Mtu anayesema serikali haina chakula anagawaje pesa kama njugu mtaani.?
 
I am convinced zinatoka mfukoni mwake, but I was confused tena, maana mkurugenzi alionyesha zile 10m zinatoka kwa serikali. Full of confussion. Kuna balance ingetakiwa kufanyika ingependeza zaidi.
 
Kodi, nasikia watumishi wa umma wanalalamika hakuna kupanda vyeo wala nyongeza ya mishahara. Madai yao wanapigwa kalenda tu.......makato yao yanaongezeka......nasikia eti bodi wanakula asilimia 15 ya "basic salary".
Sina uhakika kama mafao yanalipwa.
Wafanya biashara wamebanwa kila kona......nk nk nk..
 
Anazipata hazina. Kumbuka kuwa Ikulu can spend as much money as it wants, pia bajeti ya jeshi na ikulu huwa hazipitishwi na bunge. Wao wakihitaji pesa huwa wanaenda tu kuchota hazina...
Mmmmh!! Mkuu aliekuambia nan kuwa bajet ya ikulu haipitishwi bungen?? Kuna kitu kinaitwa bajeti ya ofis ya rais inapitishwa bungen,acha upotoshaji.....!!!
 
Mmmmh!! Mkuu aliekuambia nan kuwa bajet ya ikulu haipitishwi bungen?? Kuna kitu kinaitwa bajeti ya ofis ya rais inapitishwa bungen,acha upotoshaji.....!!!
Bajeti ya wizara na bajeti ya ikulu ni vitu viwili tofauti... Wizara ya ofisi ya Rais lazima ipite bungeni kama za wizara nyingine...
 
Anatafuta sifa kwa kugawa kodi za wananchi wakati wananchi walipotoa fedha zao kuwasaidia waathirika wa tetemeko Kagera alizipeleka kukarabati miundo mbinu ya serekali tofauti na malengo yake.
 
milioni moja ndogo hata kwa mshahara wake anaweza toa,labda useme mabilion kama ya hostel za udsm
Mkuu vepeee?, hiyo milioni moja Ni kwa mtu mmoja, akitoa kwa watu Mia inakuwaje?, Kumbuka juzi Kati Kuna mgonjwa kwao huko naye alipelekewa posho Kama hiyo badala ya kuboresha huduma ya hospitali. Swali la mleta Uzi Ni kwa nini kusiwe Na taasisi maalumu ya kusaidia makundi maalumu kwa uratibu unaoeleweka?.
 
Hii inanikumbusha enzi mabutu, alipo fika wakati ambao wananchi wamemchoka, alikua anakutana na maandamano njiani akitokea kijiji kwake basi anawapa pesa cash. basi wananchi wakajua kuwa kumbe tukiandamana tunapewa pesa , kakawa ndio kamchezo kao.
 
Back
Top Bottom