Penzi langu

Dr leader

JF-Expert Member
Joined
Jun 28, 2016
Posts
1,043
Reaction score
1,314
Penzi langu

Kama nikiyapa pesa, siku ikinisaliti?
Sitaki kulipepesa, hii haitaji siti
Sio yule wa madesa, kuyamwagiwa manoti
Nimeridhi penzi langu, nalitoa kwa kalamu

Nimliwazaji wangu, peke anayenisema
Nimpaye tunu yangu, nikiwa nimeumia
Ajua furaha yangu, hachoki kunisemea
Nimeridhi penzi langu, nalitoa kwa kalamu

Mashallah mliwaza, kwenye magumu navuka
Sitachoka kumuwaza, popote ninapofika
Na sitaki kumkwaza, sababu sijapevuka
Nimeridhi penzi langu, nalitoa kwa kalamu

Huniasa nisichoke, niandike kila siku
Nakua sana mpweke, tena na kubwa shauku
Mkono sipomshika, naganda kama sumaku
Nimeridhi penzi langu, nalitoa kwa kalamu

Abuuabdillah ✍️🇹🇿
0718569091
Kilimanjaro
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…