Pasco wa JF naomba nikuulize

mara alitokea dereva wa zitto na kujumuika nao na ilipotimu saa sita za ucku aliondoka nao (PM7) kwa kauli hii unafikiri Zitto atafurukuta ndani ya chadema hadi kukabidhiwa kijiti cha kuwania nafac ya Urais
 

Umetishaaaaa Good analysis!!! Nimepata kitu hapa "The Best vs The Choosen One"
 
Mkuu Pasco hivi kutakuwa na athari gani iwapo kwa EL na ZZK wasipoteuliwa na vyama vyao?
Kuhusu muundo wa serikali ijayo (2015) unapendekeza iweje? (hint.Make Katiba to remain constant or slighly change to happen).
 
Ni kigezo gani umetumia kwa Zito ili usemeanafa kama sio unataka kuingiza cdm mkenge.ZITTO mwenyewe yuko kimya kwenye kuimarisha chama wenzeke wanazunguka nchi nzima na M4C yeye anzunguka nje ya nchi kwa mambo.
 

Hivi kuna tofauti gani kati Pasco na mimi kuwa na uhalali wakutoa maoni/msimamo nani anafaa kuwa Rais wa Tanzania? Je mimi pia mtanisikiliza nikitoa msimamo wangu kwamba anayefaa kuwa rais wa Tanzania 2015 ni Adrew Chenge? Kwa hiyo maoni ya Pasco kuhusu nani anweza kuwa rais wa Tanzania yanaweza kuwa sawasawa na ya mwendawazimu mwingine yeyote ambaye kulingana na uelewa au hata maslahi yake atamtaja Membe, Zitto au hata Lowassa kuwa anaweza kuwa rais wa Tanzania 2015.
 
Mode, naomba ifunge hii thread, niliulizwa swali moja, nikajibu, aliyeuliza ameridhika, sasa imeshamaliza relevance yake na haina mashiko tena, nashauri ifungwe!.
Pasco.
 
Mzimu wa Mwanahalisi unawatesa sana... unaikumbuka hii

Masalia ya Zitto yapukutishwa CHADEMA

 
Ungekuwa unafuatilia misimamo ya Pasco wala usingepata shida. Pasco amekuwa very consistent about watu anaowaunga mkono. Hizi thread sasa inabidi tuzianzishie peer review process.
 
Pasco siku zote hueleweki points zako,Hunaga msimamo wowote siku zote.
Huyo Pasco ni mchumia tumbo wa kawaida sana.
Wala usipote muda sana kumjadili hapa.

Ana rangi nyingi kuliko kinyonga.
Watu kama hao enzi za Adoph Hitler walikuwa wanachomwa moto tu.
 
Mbona jibu la Pasco ni rahisi tu, jibu ni 2014/2015!
 
Pasco swali dogo la nyongeza,Na wewe utagombea uwakilishi ktk jimbo/sehemu gani na tiketi ya chama gani?
Very unfortunately mpaka sasa hapa nilipo, sina chama, yaani sio mwanachama wa chama chochote cha siasa!. Kwa vile uchaguzi ujao wa 2015, mgombea huru ni rukhsa, hilo linafikirika na nikiamua naweza kugombea popote!.
Pasco.
 

Vyombo vya habari, wachambuzi na waandishi wengi katika masuala ya kijamii, kisiasa na kiuchumi nchini tumekuwa na kasumba ya:
  • Kuhabarisha
  • Kushawishi
  • Kushabikia
Badala ya kuchambua mbivu na mbichi na kuwaacha walaji wajue kipi ni bora kwa afya zao. Jukumu letu si kutoa hitimisho.

Hitimisho la nani anafaa na nani hafai ni kazi ya wananchi ambao wana dhamana ya kutumbukiza kura zao ndani ya ballot box. Hili la kwamba fulani na fulani ni chanda cha dhahabu, fulani na fulani hawana ubora kwa nafasi fulani bila kuleta mizani iliyotumika ni kutufikisha huko huko kwenye misingi ya wachambuzi kuhabarisha, kushabikia na kushawishi.

Pamoja na kwamba uhabarishaji ni jambo la msingi katika jamii, lakini vyombo vya habari pamoja na wachambuzi katika masuala ya uongozi nchini tunatakiwa kupanda ngazi moja juu zaidi katika kuchambua ngano na maguu shambani ili uvunaji unapowadia wavunaji wanakuwa na upeo wa kuelewa yapi magugu kuyatenga mbali na ngano itakayowekwa ghalani kwa ajili ya afya za watumiaji.

Narudia nilichokisema katika mada mbalimbali huko nyuma kwamba, uhariri katika vyombo mbalimbali vya habari nchini ni wa mantiki isiyo na kiwango kwa sababu ya uhariri wa kishabiki na kushawishi kuegemea upande fulani bila kuiangalia sarafu pande zote mbili. Hali kadhalika waandishi pamoja na ujuzi wa uchambuzi walio nao uandishi wao umeegemea zaidi kuhabarisha, kushabikia na kushawishi kitu ambacho ni kinyume cha taaluma ya ujuzi na uwajibika kwa jamii kwani ni uandishi ni chombo muhimu cha kuelimisha wananchi si kuwachagulia viongozi.

Hakuna mgombea uongozi anayekuwa perfect, kwani kila binadamu ana udhaifu wake. Pamoja na ukweli huo kuna mengi yanayotakiwa kuangaliwa katika maisha ya mtu katika kupima uwezo wake katika kuongoza nchi.
Familia yake:
Muhimu kuangalia mtu uwezo anaokuwa nao katika kuongoza, kusetirika na ushirikiano anaokuwa nao katika familia yake kuanzia mume/mke na watoto wake, hali kadhalika mafanikio katika familia ni kipimo mojawapo, vinginevyo huwezi kujua uwezo wake kikamilifu.
Historia ya maisha yake:
Katika jamii wagombea wengi hujitahidi kuwa karibu na jamii wanazotaka kutumikia, isiwe kipindi cha papo kwa papo, kinachoangaliwa zaidi maisha yake tangu utotoni katika familia yake, shuleni, kazini, nk
Utumishi kwa umma:
Mambo kadhaa hutakiwa kuangaliwa utumishi wa mtu katika jamii kuangalia mafanikio yake katika shughuli alizofanikisha, uwezo wake wa kubuni mambo ya maendeleo kwa jamii, uwezo wa kusimamia miradi au kazi alizofanya au anazofanya, mahusiano yake na staff awapo katika shughuli hizo na jinsi anavyoweza kuwaunganisha wananchi na viongozi wenzake katika utumishi na uwajibikaji bila ubinafsi.
Alama za uongozi bora na udhaifu wake:
Katika nafasi hizo hapo juu, kwa kuangalia kwa undani mambo kadhaa yatajitokeza ikiwa ni pamoja na mafanikio yake. Hali kadhalika udhaifu wake utajitokeza kwa nafasi fulani fulani pamoja na kuonyesha mafanikio. Hayo yataweza kuleta picha ya uwezo wake kama kiongozi atakayefaa au la.
Kupima uwezo wake katika kushauri na kushaurika, busara katika maamuzi, uwezo wa kujali viongozi wenzake na wananchi, uwezo wa kupambanua udhaifu katika uongozi na kujitahidi kujenga taswira ya uwajibikaji kazini, pia muhimu zaidi kisaikolojia kujitambua udhaifu wake huweza kumjengea uwazi katika kushaurika.
Kama binadamu kwa vyo vyote kuna udhaifu kwani hakuna malaika, madhaifu yaanikwe ili kuwa na kipimo cha kuchagua unafuu katika wadhaifu kadhaa, ukifunikwa hatari yake majuto ni mjukuu, kwani akishakalia kiti cha Ikulu yuko juu na sheria inamlinda, pagumu kumnyoshea na kumkashifu.

Haya ndiyo tunayotakiwa kuyafanya badala ya mfumo wa propaganda uliozoeleka ambao hufanya tuwahimize wapiga kura wampigie kura fulani badala ya kuwafafanulia sifa na madhaifu ya viongozi hao wapiga kura watumia busara kutokana na ubora wa hawa wagombea. Wananchi wengi ambao ndio wenye ku-cast ballots kwenye ballot box hawawajui vizuri wagombea kwani kila mgombea anaeleza mazuri tu. Vyombo vya habari hupenya kila mahala na kisheria wana haki ya kupata kumbukumbu mbalimbali za wagombea kwa minajili ya kuelimisha jamii kwa kupima uwezo na udhaifu wao.
 
Baada ya Edward Lowassa kusifiwa na rais Magufuli kuwa ni Superman, namdurufu kidogo Lowassa kwa kujikumbusha niliwahi kusema nini kuhusu mtu huyu.
P
 
Na hivi karibuni,hasa leo,umechomoza kama mpiga zumari wa Zitto Zuberi Kabwe

Hali ya kisiasa nchini Tanzania iliyopo Nini kinachokuaminisha kuwa hawa ni bora? Karibu Pasco,karibuni wana-JF wote tujadili

cc Pasco
Mkuu the leaned brother Petro E. Mselewa, naamini baada ya alichofanya Zitto jana mbele ya rais Mama Samia, kumuombea Mbowe aachiwe, utakuwa unakubaliana na mimi Zitto ni number nyingine, extra ordinary.
p
 
Jamaa alikuja baadae kutuambia Jiwe ndio kiongozi bora muda ukaenda akaja kusema Makonda ndio anastahili kuwa rais..confusing!!
 
Nime note Zitto anatajwa tajwa sana humu jukwaani, nikaona na mimi nijikumbushe niliwahi kuandika nini kumhusu mtu huyu.
All and all, huyu Zitto sio mtu wa mchezo mchezo, he is a man to watch very closely!, sio mtu wa kawaida!.
P
 
Nime note Zitto anatajwa tajwa sana humu jukwaani, nikaona na mimi nijikumbushe niliwahi kuandika nini kumhusu mtu huyu.
All and all, huyu Zitto sio mtu wa mchezo mchezo, he is a man to watch very closely!, sio mtu wa kawaida!.
P
I second you Paschal..

Huyu bwana Jepesi tunaomfahamu hatushangai sana wasiomfahamu wanamchukulia poa.

Inahitaji uwezo wa ziada wamfahamu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…