Paracetamol (Acetaminophen)

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
58,636
Reaction score
220,350
Habari za leo wapendwa, paracetamol ni dawa ambayo inapatikana kirahisi madukani na intatumika sana Paracetamol inatumika kupunguza homa na maumivu katika mwilini. Ni bora tufahamu dose na madhara ya paracetamol inapozidi katika mwili.

kwa njia ya mdomo mtu mzima anatakiwa anywe 0.5g-1.0 g kila baada ya masaa 6 na usizidishe 4.0g kwa siku.

Kwa njia ya haja kubwa mtu mzima: 0.5g-1.0g kila baada ya masaa 4-6 na asizidishe 4.0g kwa siku.


kwa kutuliza homa kwa watoto
njia ya mdomo;
mtoto wa miezi 3-5 dose ni 60mg kila baada ya masaa 4-6
mtoto wa miezi 6 mpaka mwaka mmoja 120mg kila baada ya masaa 4-6
mtoto wa miaka 2 -3 180mg kila baada ya masaa 4-6
mtoto wa miaka 4-5 240mg kila baada ya masaa 4-6
6-7yrs 240-250 mg kila baada ya masaa 4-6
8-9yrs 360-375mg kila baada ya masaa 4-6
10-11yrs 480-500mg kila baada ya masaa 4-6
12-15yrs 480-750mg kila baada ya masaa 4-6
16-17 0.5g -1g kila baada ya masaa 4-6
Dose zisizidi 4 kwa siku.

Kwa njia ya haja kubwa:
miezi 3-11 60mg-125mg kila baada ya masaa 4-6
mwaka 1-4 125-250 mg kila baada ya masaa 4-6
miaka 5-11; 250-500mg kila baada ya masaa 4-6
miaka 12-17 500mg kila baada ya masa 4-6
Dose zisidi nne kwa siku.

Paracetamo ya maji yenye ujazo wa 500mg/5ml hairuhusiwi kwa watoto chini ya umri wa miaka 16. Hairuhusiwi kwa watoto wa chini ya miezi miwili kwa njia ya mdomo; chini ya miezi 3 kupitia njia ya haja kubwa. Kwa njia ya sindano inatakiwa kibali maalumu cha kutibu watoto wadogo au wenye uzito chini ya kilo 10.

Wanywa pombe, kabla ya kunya paracetamol angalia unywaji wako wa pombe katika masaa 24 yaliyopita, ambao hawapati chakula cha kutosha mwilini pia ni vizuri kuangalia ulaji wao katika masaa 24 kabla ya kunywa paracetamol.

Uzidishaji wa paracetamol mwilini unasababisha kuharibika kwa mfumo wa figo.

Paracetamol haina madhara kwa wajawazito pia wamama wanaonyonyesha dose moja/mbili si tatizo.

Source: BNF.
 
Utakuwa nesi wewe au doctor! Mimi huwa napiga km pain killer.
 
Mkuu dawa unayokunywa kupitia mdomoni hupitia kwenye mfumo wa chakula kabla haijafika kwenye mzunguko wa damu na kufikia eneo lengwa, ni tofauti na dawa unayopata kupitia sindano, mishipa ya damu au njia ya haja kubwa. Mwenye uamuzi wa njia ya dawa ni daktari na hii inatoka na ugonjwa na maumivu yako. Kuna dawa mgonjwa hupewa kupitia njia ya haja kubwa.
 
Kwa mtu mzma inatakiwa masaa mangapi ndio aanze kunywa pombe baada ya kumeza paracetamol Sky Eclat
 
Kwa mtu mzma inatakiwa masaa mangapi ndio aanze kunywa pombe baada ya kumeza paracetamol Sky Eclat
Beer moja au glass moja ya wine ni sawa lakini kusuburi baada ya masaa 24 ni bora zaidi kwani vyote vina chujwa kwenye ini.
 
Ni ipi njia pendekezwa?Kinywani au kwa haja kubwa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…