Papa aongoza Jumapili ya matawi kanisa likiwa tupu

Shadow7

JF-Expert Member
Sep 28, 2020
13,812
20,223
Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Francis leo hii ameongoza ibada ya Jumapili ya Matawi, katika kanisa la Mtakatifu Petro Basilica likiwa tupu kabisa kutokana na vizuizi vya kukabiliana na virusi vya corona.



Katika ibada hiyo inayofanyika kwa namna hiyo kwa mwaka wa pili mfululizo Papa amewataka watu kujisogeza karibu katika kuwasaidia masikini na wagonjwa.



Katika nyakati za kabla ya janga la corona, Jumapili ya Matawi, ambayo inaashiria mwanzo wa Wiki Takatifu kwa Wakatoliki kuelekea siku ya Pasaka, maelfu ya watu wakiwa wameshika matawi mikononi walikuwa wakishiriki ibada hiyo ya wazi katika kanisa hilo Mtakatifu Basilica.
 
Halikuwa tupu, huyu ,piga picha hakuwa mtu?
 
Mdudu korona anaweza penya tuu hapo, Mungu tuu ana tusaidia.
 
Hawezi kuwa mjinga ka meko
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…