Ikumbukwe kwamba hivi karibuni kundi hili lilileta sintofahamu juu ya usalama wa raia na mali zaoi jijini Dar es Salaam.Kama kawaida Polisi walichukua jukumu lao la kuhakikisha usalama unakuwepo kwa kutoa taarifa kupitia vyombo vya habari wakidai kuwa ni wahuni wachache tu na kwamba wamedhibitiwa na Polisi.Taarifa hizo zilitolewa na Kamanda Polisi Kanda maalamu ya Dar es Salaam.Ukifuatilia taarifa zake zinaonyesha kuwa kundi hilo aidha lilikuzwa kupitia mitandao,lakini pia utaona haikuwa uzushi kama ilivyodaiwa na Kamanda Kova.
Ni ukweli usiopingika kundi hilo la Panya Road limevuta hisia kubwa katika jamii,na kwamba limeweza kuteka jamii kwa muda mrefu tangu lilipoanza uharifu hadi hali ilipotulia.Kwa nchi kama yetu haingii akilini kwa kundi hili kushika kasi kwa muda mfupi kama huo,ukizingatia kuwa kila raia anawajibika kuhakikisha amani inakuwapo nchini.Ni kwa nini dhana hii ya ulinzi inatoweka kwa mtanzania?
Jibu ni wazi kwamba,Tanzania ya sasa si ya zamani.Matabaka kati ya walionacho na wasiokuwa nacho limeongezeka mno kiasi cha kuona maskini hawana haki tena.Kiashiria hiki ni hatari mno kwa usalama wa nchi yetu.
Wapi tulikosea?Tulipoua Azimio la Arusha kila kila kitu kikaanza kupanganyika(fall apart).Viongozi wakaanza kuwa wenye sauti zaidi kuliko waaajiri wao(yaani wananchi). Miiko ya viongozi iliondolewa kinyemela.Hapa ndipo tulianza kuona kuota kwa shule zinaitwa English Medium Schools/English Academy Schools.Shule hizi zinawapeleka na kuwarudisha majumbani watoto kwa magari.Watoto hawabebi tena mfagio na dumu la maji.Watoto hawadeki madarasa yao nk.Hawa ni watoto wa wenye nacho.
Ni swali la kujiuliza,katika jamii iliyojengwa kwa misingi ya haki na usawa,iweje kuwepo na matabaka haya?Bila shaka jibu liko wazi kuwa ni ubibafsi wa viongozi wetu baada ya kuona Azimio la arusha linawabana wakaamua kuliua.Ikumbukwe,hata baada ya juhudi za kurejesha usawa huo kupitia Tume Ya KATIBA(Tume ya Warioba),bado watawala kupitia Bunge la Katiba wameamua kuitupilia mbali miiko ya viongozi ili waendeleza dhana ya matabaka.
Zipo hotuba za viongozi wa kisiasa waliodiriki kusema kuwa ukosefu wa ajira kwa vijana ni bomu linalosubiri kulipuka kama hatua madhubutu hazitachukuliwa na serikali.Viongozi hao walibezwa kwa kejeli na mawaziri wenye dhamana za ajira hivi majuzi.Sasa tunaona kilichojiri hivi punde kuhusu Panya Road!
Miaka ya 2004 ilitokea mivutano kati ya mgambo wa jiji la Dar ambapo wamachinga walimuua mgambo.Hizo zilikuwa dalili tosha za kutafuta ufumbuzi.lakini aidha kwa makusudi au kutokudhamiria serikali ilichukua au haikuchukua hatua.Hii ni ishara kuwa VICIOUS CYCLE OF POVERTY imeshika kasi.Natoa rai kwa serikali ichukue hatua kupambana na hali hii,sababu kama hakutakuwa na ulinganisho wa maisha katika jamii,amani ya nchi yetu itatoweka haraka sana.Vijana hao watakapochoka kusubiri unafuu wa maisha,hawatajali wewe nyumba yako inalindwa na mitambo maalumu, au una silaha gani wataingia na kuchukua wanachotaka sababu wana njaa.Vijana wasio na kazi ni wengi mno.Wanamaliza shule au vyuo mbali mbali wanabaki mtaani bila ajira.
Ni kwa nini wasijiite majina kama PANYA ROAD ili waweze kusikika haraka.Polisi wafanye tafiti za kina ni kwa nini kundi limeibuka kwa nguvu kubwa.Aidha serikali itafute suruhu ya kudumu kwa tatizo ajira kwa vijana.Leo Panya Road wako Dar,kesho Arusha,Mwanza,Mbeya na hatimaye nchi nzima na mwisho kabisa kundi la kigaidi.Tuchukue hatua kwa kujenga jamii inayopendana na kuwa na mgawanyo sawa wa rasilimali za nchi.
Nawasilisha.
Ni ukweli usiopingika kundi hilo la Panya Road limevuta hisia kubwa katika jamii,na kwamba limeweza kuteka jamii kwa muda mrefu tangu lilipoanza uharifu hadi hali ilipotulia.Kwa nchi kama yetu haingii akilini kwa kundi hili kushika kasi kwa muda mfupi kama huo,ukizingatia kuwa kila raia anawajibika kuhakikisha amani inakuwapo nchini.Ni kwa nini dhana hii ya ulinzi inatoweka kwa mtanzania?
Jibu ni wazi kwamba,Tanzania ya sasa si ya zamani.Matabaka kati ya walionacho na wasiokuwa nacho limeongezeka mno kiasi cha kuona maskini hawana haki tena.Kiashiria hiki ni hatari mno kwa usalama wa nchi yetu.
Wapi tulikosea?Tulipoua Azimio la Arusha kila kila kitu kikaanza kupanganyika(fall apart).Viongozi wakaanza kuwa wenye sauti zaidi kuliko waaajiri wao(yaani wananchi). Miiko ya viongozi iliondolewa kinyemela.Hapa ndipo tulianza kuona kuota kwa shule zinaitwa English Medium Schools/English Academy Schools.Shule hizi zinawapeleka na kuwarudisha majumbani watoto kwa magari.Watoto hawabebi tena mfagio na dumu la maji.Watoto hawadeki madarasa yao nk.Hawa ni watoto wa wenye nacho.
Ni swali la kujiuliza,katika jamii iliyojengwa kwa misingi ya haki na usawa,iweje kuwepo na matabaka haya?Bila shaka jibu liko wazi kuwa ni ubibafsi wa viongozi wetu baada ya kuona Azimio la arusha linawabana wakaamua kuliua.Ikumbukwe,hata baada ya juhudi za kurejesha usawa huo kupitia Tume Ya KATIBA(Tume ya Warioba),bado watawala kupitia Bunge la Katiba wameamua kuitupilia mbali miiko ya viongozi ili waendeleza dhana ya matabaka.
Zipo hotuba za viongozi wa kisiasa waliodiriki kusema kuwa ukosefu wa ajira kwa vijana ni bomu linalosubiri kulipuka kama hatua madhubutu hazitachukuliwa na serikali.Viongozi hao walibezwa kwa kejeli na mawaziri wenye dhamana za ajira hivi majuzi.Sasa tunaona kilichojiri hivi punde kuhusu Panya Road!
Miaka ya 2004 ilitokea mivutano kati ya mgambo wa jiji la Dar ambapo wamachinga walimuua mgambo.Hizo zilikuwa dalili tosha za kutafuta ufumbuzi.lakini aidha kwa makusudi au kutokudhamiria serikali ilichukua au haikuchukua hatua.Hii ni ishara kuwa VICIOUS CYCLE OF POVERTY imeshika kasi.Natoa rai kwa serikali ichukue hatua kupambana na hali hii,sababu kama hakutakuwa na ulinganisho wa maisha katika jamii,amani ya nchi yetu itatoweka haraka sana.Vijana hao watakapochoka kusubiri unafuu wa maisha,hawatajali wewe nyumba yako inalindwa na mitambo maalumu, au una silaha gani wataingia na kuchukua wanachotaka sababu wana njaa.Vijana wasio na kazi ni wengi mno.Wanamaliza shule au vyuo mbali mbali wanabaki mtaani bila ajira.
Ni kwa nini wasijiite majina kama PANYA ROAD ili waweze kusikika haraka.Polisi wafanye tafiti za kina ni kwa nini kundi limeibuka kwa nguvu kubwa.Aidha serikali itafute suruhu ya kudumu kwa tatizo ajira kwa vijana.Leo Panya Road wako Dar,kesho Arusha,Mwanza,Mbeya na hatimaye nchi nzima na mwisho kabisa kundi la kigaidi.Tuchukue hatua kwa kujenga jamii inayopendana na kuwa na mgawanyo sawa wa rasilimali za nchi.
Nawasilisha.