Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 36,357
- 23,759
Ndugu zangu Watanzania,
Huyu Padri Ameonyesha waziwazi kuwa na chuki binafsi na Rais wetu Mpendwa,ameonyesha tangia awali kuwa na kinyongo na utawala huu, ameonyesha kuwa na dharau na maneno ya dharau sana awamu hii.
Inaonyesha ni mtu mwenye Ubaguzi wa kidini na mtu aliyejaa kiburi moyoni Mwake na kuonyesha kana kwamba yeye ni bora ama mwenye akili nyingi au mwenye kujua kila kitu . Yaani ni kama amejivika Umungu Mtu.
Kitendo na hatua ya kutamka hadharani maneno ya Kwamba kama Rais Ana neno azungumze ilikuwa ni Dharau kubwa sana kwa Rais na Taasisi ya Urais. Ni kebehi na kutaka kuitweza ama kumtweza,kumshushia heshima na kumdhalilisha Rais wetu.
Ni maneno ya kiburi na yaliyokosa Adabu na heshima kwa kiongozi wa kidini mbele ya Rais. Ikumbukwe ya Kuwa Rais Wa Nchi ambaye ni Mkuu wa Nchi , Kiongozi wa Serikali na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama ni Mfariji wa Taifa . Ni Kiongozi Ambaye huwezi kusema Kama ana Neno basi azungumze. Hivi kweli inaingia akilini Hii kweli?
Unaweza pata wapi ujasiri wa kuongea na kutamka maneno haya mbele ya Rais mtu Unayejitambua na mwenye heshima? Yaani unamwambia Mkuu wa Nchi aliyeacha shughuli za kulitumikia Taifa nakuja kuungana na waombolezaji kuwapa pole na kuwafariji kuwa kama ana neno?
Hivi unajua Ratiba za Rais Wewe? Hivi unajua majukumu ya Rais ya kila siku? Hivi unajua kuna mawaziri wanakosa hata nafasi ya kumuona na kuzungumza na Rais ana kwa ana ? Hivi unajua maandalizi ya safari ya kumtoa Rais Ikulu mpaka kuja kwako kutoa pole na faraja kwa waombolezaji?
Hivi mtu mwenye ufahamu na adabu huwezi ukafikiria jambo hilo kuwa ni Heshima kubwa kuwa na Mkuu wa Nchi mbele yenu?
Huyu Padri inapaswa aonywe ,afundishwe,akemewe na kuaswa kuwa aache Dharau na aheshimu Mamlaka ya Urais na Rais . Hata kama ana chuki binafsi na Rais wetu kutokana na sababu zake binafsi ama za Udini ama vyovyote iwavyo Basi ajue ya kuwa Rais wetu yupo hapo alipo kwa mujibu wa sheria na katiba ya Nchi. Hayupo hapo alipo kwa bahati mbaya ama kubahatisha.
Na kamwe hawezi kumshusha wala kumfanya lolote lile. Atake ama asitake Ataendelea kuongozwa na Rais Samia . Apende ama asipende Rais wa Nchi hii ni Mmoja Tu Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan Mama wa shoka , chuma cha reli, shujaa wa Afrika na jasiri muongoza njia.
Nampongeza sana Rais wetu Mpendwa kwa kukataa kuzungumza na badala yake kuamua kuondoka zake ili kwenda kuendelea na ratiba zingine za kuwatumikia watanzania na Taifa letu kwa ujumla wake.
Mwisho ni kuwa yeyote na kwa mtu yeyote yule mwenye chuki binafsi na Rais wetu kutokana na sababu zake zozote zile za kijinga jinga kamwe na katu hataweza kushusha heshima ,hadhi na Thamani ya Rais wetu. Heshima ya Rais wetu itaendelea kusalia palepale. Na kamwe hakuna mkono wa mwanadamu yeyote yule awaye utakaoweza kumshusha Rais wetu. Rais Samia ni Mpango wa Mungu Mwenyewe na ni chaguo la Mungu Mwenyewe kuliongoza Taifa letu.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Huyu Padri Ameonyesha waziwazi kuwa na chuki binafsi na Rais wetu Mpendwa,ameonyesha tangia awali kuwa na kinyongo na utawala huu, ameonyesha kuwa na dharau na maneno ya dharau sana awamu hii.
Inaonyesha ni mtu mwenye Ubaguzi wa kidini na mtu aliyejaa kiburi moyoni Mwake na kuonyesha kana kwamba yeye ni bora ama mwenye akili nyingi au mwenye kujua kila kitu . Yaani ni kama amejivika Umungu Mtu.
Kitendo na hatua ya kutamka hadharani maneno ya Kwamba kama Rais Ana neno azungumze ilikuwa ni Dharau kubwa sana kwa Rais na Taasisi ya Urais. Ni kebehi na kutaka kuitweza ama kumtweza,kumshushia heshima na kumdhalilisha Rais wetu.
Ni maneno ya kiburi na yaliyokosa Adabu na heshima kwa kiongozi wa kidini mbele ya Rais. Ikumbukwe ya Kuwa Rais Wa Nchi ambaye ni Mkuu wa Nchi , Kiongozi wa Serikali na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama ni Mfariji wa Taifa . Ni Kiongozi Ambaye huwezi kusema Kama ana Neno basi azungumze. Hivi kweli inaingia akilini Hii kweli?
Unaweza pata wapi ujasiri wa kuongea na kutamka maneno haya mbele ya Rais mtu Unayejitambua na mwenye heshima? Yaani unamwambia Mkuu wa Nchi aliyeacha shughuli za kulitumikia Taifa nakuja kuungana na waombolezaji kuwapa pole na kuwafariji kuwa kama ana neno?
Hivi unajua Ratiba za Rais Wewe? Hivi unajua majukumu ya Rais ya kila siku? Hivi unajua kuna mawaziri wanakosa hata nafasi ya kumuona na kuzungumza na Rais ana kwa ana ? Hivi unajua maandalizi ya safari ya kumtoa Rais Ikulu mpaka kuja kwako kutoa pole na faraja kwa waombolezaji?
Hivi mtu mwenye ufahamu na adabu huwezi ukafikiria jambo hilo kuwa ni Heshima kubwa kuwa na Mkuu wa Nchi mbele yenu?
Huyu Padri inapaswa aonywe ,afundishwe,akemewe na kuaswa kuwa aache Dharau na aheshimu Mamlaka ya Urais na Rais . Hata kama ana chuki binafsi na Rais wetu kutokana na sababu zake binafsi ama za Udini ama vyovyote iwavyo Basi ajue ya kuwa Rais wetu yupo hapo alipo kwa mujibu wa sheria na katiba ya Nchi. Hayupo hapo alipo kwa bahati mbaya ama kubahatisha.
Na kamwe hawezi kumshusha wala kumfanya lolote lile. Atake ama asitake Ataendelea kuongozwa na Rais Samia . Apende ama asipende Rais wa Nchi hii ni Mmoja Tu Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan Mama wa shoka , chuma cha reli, shujaa wa Afrika na jasiri muongoza njia.
Nampongeza sana Rais wetu Mpendwa kwa kukataa kuzungumza na badala yake kuamua kuondoka zake ili kwenda kuendelea na ratiba zingine za kuwatumikia watanzania na Taifa letu kwa ujumla wake.
Mwisho ni kuwa yeyote na kwa mtu yeyote yule mwenye chuki binafsi na Rais wetu kutokana na sababu zake zozote zile za kijinga jinga kamwe na katu hataweza kushusha heshima ,hadhi na Thamani ya Rais wetu. Heshima ya Rais wetu itaendelea kusalia palepale. Na kamwe hakuna mkono wa mwanadamu yeyote yule awaye utakaoweza kumshusha Rais wetu. Rais Samia ni Mpango wa Mungu Mwenyewe na ni chaguo la Mungu Mwenyewe kuliongoza Taifa letu.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.