Acheni kuteka na kuua watu 📌
Tendeni haki 📌
Wasikilizeni wananchi 📌
Punguzeni ufisadi 📌
Ruhusuni katiba mpya 📌
Inueni uchumi wa watu wenu 📌
Ruhusuni tume huru ya uchaguzi 📌
Shughulikeni na ajira kwa vijana 📌
Punguzeni nepotism 📌
Kutoyazingatia haya machache kutazidi kuchochea moto mioyoni mwa watu. Na nchi haitakuwa salama. Kunaweza kuwa na utulivu lakini kusiwe na amani. Ni kama kuwa na bomu chini ya kitanda chako!
Kwa sasa mnaweza kufurahi na kupongezana kuwa mmefanikiwa kuzuia maandamano tena kwa gharama kubwa ya ku-mobilize jeshi utafikiri nchi imo vitani lakini wananchi mnaowaongoza wana hasira na visasi. Na huwezi kutawala watu ambao hawakukuchagua na hawakutaki. Wengi walishajaribu wakashindwa na hawakuwa na mwisho mwema.
Samia atajaribu kutawala kwa kutumia mitutu ya bunduki, kuteka na kuua watu lakini hataweza na, kama historia ni mwalimu sahihi, hatakuwa na mwisho mzuri. Na ataishia katika pipa la takataka la historia kama kiongozi katili, muuaji, fisadi na asiyejali.
Anajua hakuchaguliwa na wananchi. Anajua hakupata kura milioni 32. Anajua hakushinda kwa 98%. Anajua uchaguzi ulivurugika. Anajua alijiapisha kimagumashi. Anajua siyo rais halali. Anajua anaongoza serikali haramu. Basi angalau ajaribu kutenda haki ili ajikongoje na hii miaka mitano yake ambayo itakuwa mirefu na ya mateso sana kwake hasa akiendelea na huu udikteta wake.
Mungu Aendelee kuibariki nchi yetu hii nzuri yenye kila kitu lakini inaharibiwa na wanasiasa wasio na maono, walafi, wauaji, mafisadi na wasiojali! 🙏🏿🙏🏿🙏🏿🙏🏿