Hili shambulio mimi nililisikia mapema Jumamosi kupitia media (radio, tv, mitandao) na nimeendelea kupata taarifa zaidi kupitia njia hizo hizo kila mmoja akisema lake huku kazi yangu mimi ikiwa ni kuchuja opinions za wanaochangia mjadala. Ni kupitia njia hizo nimewasikia mashuhuda wakisema kuwa huyu mshambuliaji alikuwa ni mwenzao, sasa kuthibitisha au kukanusha hilo siwezi maana hata huko Florida sijawahi kufika!
Hayo mambo ya sodoma, sijui moto nk ni mambo yaliyo beyond our imagination na ndio maana tunajadili tunayoweza. Mfano Mungu akishusha moto duniani kama ilivyokuwa kwa big bang nakuwa na mashaka hata wasio mashoga watateketea. Katika opinion ya muombolezaji mmoja wapo kutoka Australia amesema kwamba "jamii ya mashoga tuko wengi zaidi ya mnavyodhani". Na je, unajua kwamba hawa jamaa hata Tanzania wapo na wanafurahia matendo yao japo hakuna sheria iliyowaruhusu (au sheria inayowakataza!)!?