Original komedy kwishiney

Status
Not open for further replies.
...labda mzee wa quality plaza atawapa ajira ya ku-entertain wageni wanaomtembelea ofisin kwake.:eyebrows:
 
we rejao hawa jamaa si mnawatumia kukusanya watu kwenye kampeni zenu??imekuwaje tena

Imekuwa je tena nani kakudanganya hii hali ngumu ya kiuchumi imetufikia sisi wananchi tu?
 
Wamefuliaaaaaaaaaaaaa dhambi ya kuwasema wenzao wamefulia inawatafunaaaaaaa!!
 
Wote mliochangia mnachuki binafsi na hawa washikaji. Mbona jamaa ni creative sana, na mimi sijaona hapa Tanzania wenye vipaji kama kundi hili, waigizaji wengine wanaigiza kwa mtindo wa miaka ya 47'. kama hao wa EATV ndiyo wamechoka kabisa huwezi kuwalinganisha na akina masanja hata kidogo, hata wale wa channel ten na star tv wote hao hawana vipaji, hata mizengwe siku hizi hakuna kitu. Ukweli ni kuwa Orijino komedi wapo juu!!
 
Wakati wao sasa umepita yafaa wajitaftie kwa njia nyingine ili watakaposhindwa kujikimu watokee wasanii wengine wawaigize wamefulia kama walivyo waigiza wenzao hapo awali
 
Watanzania; Ukianza kuonyesha kipaji utatiwa moyo sana na kupongezwa.Ukipata mafanikio tegemea vikwazo na maneno ya kukatisha tamaa...mbaya zaidi ukianguka kila mtu utamsikia " tulijua tu".

Ukipata mafaniko kwenye nchi hii kuwa makini sana na chunga nyendo zako..usimkanyage hata sisimizi hata kwa bahati mbaya!!!
 

Mkuu umenikumbusha huyu jamaa manji aliishia wapi? Tangia msema kweli athibitishe yeye ni fisadi sijamsikia tena
 
afadhar wapotee nanilihi zao kbs...yan waliniudhi cku ile wanadhihaki matokeo ya uchaguz igunga as if wao ndo ccm,.

Walitumwa na njaa zao zikashindwa kuwasitiri
 

Hawa wa EATV mwanzo walianza vizuri kwa stail yao mpya kabisa ila baadae wakaja kuwaiga hawa waliofulia
 
Walikuwa hawaijui ccm, wanakutumia kara moja na kukutupa kama toilet paper na sasa tunamsubiri huyu wa hakunaga nae afulie
 
Si unajua mgema akisifiwa tembo ulitia maji?
 

My comment has nothing to do with the actuality on whether hawa wasanii wamefulia au la, ila sidhani mtu kuwa na nyumba na/au biashara ndogo ndogo ndio kigezo cha mtu kuwa na uchumi mzuri. Uzoefu wangu juu ya kufanya biashara kama side activity ni kuwa watu wengi hu-subsidize biashara zao na main activities (especially ajira zao) na inapotokea main activity imeondoka na biashara nayo huyumba.

Sidhani kama ni rocket science, ila ukweli ni kwamba biashara ni ajira in its own right, usipoisimamia mwenyewe utakuwa umempa mtu mtaji wa bure.
 
Warudi wamuombe Msamaha mengi na siku nyingine wajifunze kutokunyea kambi
 
Kwa jinsi ninavyoona mimi nahisi(kama ni kweli TBC wamekatisha nao mkataba) nahisi Management ya sasa ya TBC itakuwa ina matatizo ama wanataka waondokane na mikataba yote ambayo iliingiwa wakati wa TIDO/kuondoa program zilizoanzishwa enzi za TIDO.....

Vipindi vingi vya burudani vilivyoanzishwa enzi za TIDO havipo sasa.....Mfano Bongo Dar es Salaam, Burudani ni Nyumbani, Orijino Komedi Show, Boda 2 Boda na hata matangazo ya Live ya michezo ya Ligi Kuu ya Uingereza......Kwa ujumla TBC kwa sasa inarudi nyuma kwa kasi badala ya kuendelea mbele...

Kiukweli hauwezi ukawalinganisha Ze Comedy wa EATV na Orijino Komedi.....Wale wa EATV ni bure kabisa,hawana jipya zadi ya kuwaiga Orijino Komedi.....Hata Futuhi ina uafadhali.....

Kwangu mimi VITUKO SHOW ya Channel Ten ndio Mwanzo mwisho......King Majuto, Onyango, Mwita Maranya, Sharo Milionea, Masele Chapombe, Mzee Pembe, Mzee Toffi, Asha Boko, Shangazi/Madoido, Senga, Chilli, Mkono,Kingwendu, Erick na wengine.....Hawa jamaa wako juu kuliko maelezo

 
Last edited by a moderator:
Ni wehu tu,sasa watamkumbuka Mzee mengi baada yakupata vitz wajiona wanalingana na manji wakaanza kutukana kituo cha ITV eti hakiko katika viwango hawakujua kuwa wao walikuwa wanatumika kama kipaza sauti!!!!Sasa waende kwa Manji wakachekeshe Quality Plaza langoni.
 
walijisahau kiasi kwamba wakakosa ubunifu zaidi au yawezekana ndio kiwango chao kilipofikia so hawana jipya .. na kupenda kutumika pasipo kufikiria itawagharimu
 
Hivi kwani lazima waajiliwe na TBC?! Mbona kuna njia nyingin za kufanya kipindi hapohapo TBC, Wanaweza wadhamini na kurecord vipindi vyao af wananunua muda wa kurushwa vipindi vyao TBC (nina uhakika hawawezi kukosa 'Sponsor' wakiamua). Wanafanya ka kile kipindi cha 'Mkasi' cha EATV ambacho ni cha akina AY au kipindi cha 'Daladala' cha Dan Kijo
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…