Operesheni ya mwaka mzima yaifuta Ccm Karagwe!

Operesheni ya mwaka mzima yaifuta Ccm Karagwe!

mpk

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2012
Posts
3,115
Reaction score
3,864
Weekend hii ulikuwa unatimia mwaka mmoja tangu kuanza kwa operesheni ya kuifuta Ccm katika jimbo la Karagwe. Operesheni hii ilkuwa na lengo la kufikisha chama kila kitongoji iliyoungana na program ya Chadema ni msingi. Imejengwa misingi 374, Matawi 68 na kukusanya kadi za Ccm 3057, Cuf 91, TLP 57 na UDP 1, kuunda vikundi vya akina mama katika kata 9. Operesheni imekomba wenyeviti wa vitongoji 9 ingawa serikali haikubali kuitisha uchaguzi mpya.

Kwa mwaka mzima ilipigwa wastani wa mikutano mitatu kila weekend na kufanya jumla ya mikutano 157 iliyoingia vitongoji vyote vya jimbo la Karagwe isipokuwa baadhi ya vitongoji vya kata za Rugu, Nyaishozi, Ihembe na Nyakasimbi ambako umeendaliwa mkakati maalumu wa kuingia kata hizo, unaoakwenda sambamba na mkakati mpya wa lengo la kushinda asilimia 50 ya vitongoji ,vijiji na mitaa katika uchaguzi wa mwaka huu.

Kazi hii imefanyika kwa wafuasi kujitolea kwa fedha zao kuwezesha usafiri na mambo mengine. Hivi karibuni chama kitatangaza kununua vyombo vya matangazo baada ya kada mmoja kujitolea kununua vyombo hivyo baada ya kuridhishwa na kazi inayopigwa na makamanda. Baada ya tathimini itatangazwa operesheni kabambe itakayoenda non stop hadi 2015.

Peoples ..................!
 
kudadadeck zikipigwahizo op majimbo kama 250 hivi lazima inchi itatoka iliko pelekwa sasa ahsanteni sana makamanda bado muda mfupi sana inchi hii itakuwaq huru
 
NAwapongeza sana.. Good move..
 
kudadadeck zikipigwahizo op majimbo kama 250 hivi lazima inchi itatoka iliko pelekwa sasa ahsanteni sana makamanda bado muda mfupi sana inchi hii itakuwaq huru
Tena itakuwa na uhuru kamili kutoka kwa mkoloni na muuza nchi na raslimri zake ccm
 
Wakaze matterqo na kuboreshwa daftari la kudumu la wapiga kura sio mikelele mingi halafu ukifika uchaguzi chali kama juzi kwenye uchaguzi wa marudio wa udiwani ktk kata 27 imeniuma sana.
 
Hizi taarifa bana!

Kwa takwimu hizi unaweza ukadhani kweli ccm imekufa Karagwe, ukija uchaguzi wa ngazi yoyote utasikia ccm kashinda zaidi ya 75%.
Acheni kuwapagawisha watu, wapiga kura wa kweli hawapo jf na ni ngumu sana kutabiri watakavyo "behave" wakati wa uchaguzi hata wakiwa na kadi ya chama chako mkononi
 
safi sana ! Wale waliodhani cdm inatania wabadilishe mawazo !
 
Da!, vzr sana! ntafanya sherehe sk tukiizika ccm karagwe!,,inaniuma xana jimbo la wa2 walioelimika kuongozwa na magamba!,,sasa lim2 kama blandes kwel c haibu? jaman wanakaragwe 2badilike jaman 2seme sasa yatosha......
 
Back
Top Bottom