Bwana Chuki, Nakushauri siku moja utembelee vijijini uone wananchi wanavyoteseka kwa maisha magumu, then usome ripoti ya CIG uone viongozi waliokutuma uandike haya wanavyotafuna pesa za maskini walipakodi. Ukiwa mkweli kwa nafsi yako, njoo utuambie tena hayo umeyoyaandika leo. Hii sio ccm aliyoiacha mwalimu, bwana chuki, hebu soma vitabu alivyoandika mwalimu utaona mambo yasivyoenda sawa. Mimi sikuchukii lakini nakuhakikishia kuwa watanzania wanateseka sana kwa sababu yenu, hebu fikiria wewe binafsi kwa siku unalipa kodi kiasi gani, kila kitu unachonunua kwa siku unachangia 18%, kwa uchache mtanzania wa kawaida analipa zaidi ya sh.3600 kwa siku kama kodi, ukichukua walau watanzania mil 20 utapata 72 bilioni kwa siku, zidisha hizo kwa mwezi theni kwa mwaka. Hapo bado kodi za magari, bandari, kodi zetu wafanyakazi, mafuta, madini, utalii nk, ukipata jibu nieleze kwa nini sisi watanzania ni omba omba???? kwa nini tunapoteza kodi za watanzania kwenda kuombaomba??? hamuoni haibu nchi yetu nyenye rasilimali zote hizi mnatufanya kuwa omba omba?? tuache siasa tuzumngumzie mstakabali wa taifa letu!!!!
Bwana chuki, hivi unafikiri tukiendelea hivi tutaishia wapi??? mwaka 2003 nauli ya daladala hapa dar, maximum ilikuwa sh.100, leo hii hata miaka 10 haijapita imefikia zaidi ya sh.500, je mwaka 2020 itakuwa sh. ngapi? nipe jibu kaka yangu, mi naumia sana kuona wenzetu mnaacha mambo ya msingi yanayoliangamiza taifa letu mnakalia mara oohh sangara, mgebuka.. sijui wachaga, hivi mnaipenda Tanzania!!!!! Mungu akubariki!!!!!