Mondoros
JF-Expert Member
- Aug 29, 2015
- 629
- 474
* VIGOGO WALIOTAZAMIWA KUHAMIA CDM WAWATOLEA NJE.
MWAPACHU - Namuunga mkono Lowasa, lakini siwezi kuhama CCM kwenda CDM. CDM hawajitambui ila wamempata mwanaume.NCHIMBI - Nimesoma hizo habari magazetini.. na nimefuatwa na viongozi wa CDM kunibembeleza nihamie kwao.. hivi uanachama mtu anaombwa au anaomba.
MWANDOSYA - Ni kweli nahama.. lakini nahama kutoka Dar kwenda kijijini kwetu Lufilyo Busekelo.. ni kweli CCM walinikwaza lakini siwezi kujidhalilisha kuhamia CDM chama ambacho siku zote nimehubiri kuwa ni wababaishaji.
SOFIA SIMBA - Nimefuatwa na vigogo wa CDM wakiniomba niungane nao kuleta mabadiliko, nimewajibu mabadiliko ya kweli yataletwa na Magufuli na si Lowasa. tulifanya makosa makubwa kutoka kikaoni, tuliona dalili za mtu kuandaliwa.. tuliomba msamaha na maisha yanaendelea.. lakini ninachofurahi ule mgomo wetu ulisaidia kuwafanya CCM kuchagua mgombea mwenye sifa.
ANTHONY DIALO- Katika vyama vya kipumbavu hapa nchini ni chadema na washirika wao, kama wanasiasa wapuuzi hapa nchini lowassa anaongoza, sijawahi kufikiri kufikiri wala sitowahi kufukiri kukihama chama cha mapinduzi, wala kumuunga mkono fisadi papa lowassa. vyombo vyangu vya habari ikiwemo STAR TV nimetoa bure kwa chama kurusha matangazo ya kampeni zetu, pia mimi ninasimamia ushindi wa chama kanda ya ziwa.
KINGUNGE- Uzushi haukuanza leo, hata wakati wa mwalimu swala la azimio la arusha lilikua na utata watu wakanizushia nimehama nchi. kwahiyo sitowashaangaa wao kusema mwanachama mwenye kadi namba nane(8) anahama.wapuuzwe.