Oparesheni Barakuda

Oparesheni Barakuda

TUTU wa Jijia

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2016
Posts
727
Reaction score
564
Oparesheni Barakuda

http://www.raiamwema.co.tz/author/admin/

“Hillary Clinton alipotembelea Jamhuri ya Kidemokrasia ya watu Kongo (DRC) Agosti, 2009 aliwashangaza raia wa Kongo alipowaambia wasahau yaliyopita wasonge mbele. Swali ni je, Marekani iko tayari kusahau Septemba 11, na kusonga mbele?” Ndivyo alivyoandika Prof. Georges Nzongola –Ntalaja kwenye Jarida la The Africa Report la Aprili-Mei, 2010.

Waafrika tumesamehe mengi, lakini kamwe hatutasahau madhila na madhara ya biashara ya Utumwa na Ukoloni. Kila kukicha tunakumbushwa utumwa wa kisiasa, kiuchumi na kijamii. Bw. Yesu alisema; “Akupigae shavu la kulia, mgeuzie na la kushoto”. Huwa najiuliza ukisha mpa yote mawili inakuaje?

Waafrika ni taifa moja kwa hiyo yanayotokea kote Afrika yanatuhusu sote. Kwa nini hatushangai Marekani yenye nchi /majimbo zaidi ya 50 au Umoja wa Ulaya nchi zaidi ya 20, zinaongea kwa pamoja na nchi zetu mmoja mmoja.

Hivi hatuoni hili peke yake ni tatizo, hata kama Gaddafi “asingewaswaga” kama baadhi ya viongozi wa Afrika wanavyodai? Mpaka lini kiongozi wa Afrika ataendelea kuvumilia unyonge wakusimama peke yake mbele ya nchi za Marekani au Ulaya katika masuala ambayo yanatuumiza waafrika wote? Je, tunasubiri idhini yao na kibaraka wao ndio tuzinduke?

Tuna changamoto ya kuchanganya “ kusamehe na kusahau”. Kusamehe ni rahisi kwani mtu anaweza kukutia kovu kwa kukusudia au kwa bahati mbaya, ukamsamehe. Lakini itakuwa ni unafiki ukisema utasahau, kwani kovu litakukumbusha. Je mtu huyo akikuumiza tena utafanyaje?

Historia inatabia ya kujirudia ndio maana matukio yote yanaandikwa ili kila kizazi kielewe na kisibweteke. Inaelekea Waafrika tu ndio mabingwa wakusamehe na kusahau. Viongozi wetu wengi wameuawa kikatili na kwa njama; Patrice Emery Lumumba wa Kongo mpaka leo damu yake haijakauka.

Oparesheni Barakuda ya kumuua Patrice Lumumba ni mfano hai kuwa wajukuu wa wakoloni hawabweteki. Udhalimu na dhuluma vipo, kusahau na kusonga mbele bila kujihami ni usaliti.

Marekani wanakumbuka 11.09.2001 na kuhakikisha haitokei tena, Wayahudi wanakumbuka, ili kila kizazi chao kiape yasitokee tena. Iweje sisi na kwa utakatifu gani, tusahau? Kwa nini tunawaandalia watoto na wajukuu wetu utumwa wa hiyari ?

Raoul Peck alitoa maoni yake kuhusu kitabu cha “Mauaji ya Lumumba” kilicho andikwa na Ludo de Witte “…ni hadithi isiyo isha, yenye kujaa dharau, uroho na utemi. Wauaji bado wako kati yetu.” Kila Mwafrika ni lazima akumbuke, yaliyotokea kwa Lumumba ni ushahidi dunia imejaa wanywadamu. Miaka 50 ya Uhuru itukumbushe ufashisti wa kiuchumi uliosababisha Lumumba auwawe Januari 17, mwaka 1961 na Gaddafi Oktoba 20, mwaka 2011. Ludo de Witte anatueleza kwa ufasaha mambo yalivyokuwa Kongo Juni 30, mwaka 1960.

Anasema wageni kutoka nje na ndani ya Kongo na waandishi wa habari walikusanyika Ikulu mjini Leopoldville. Katika lango kuu la kuingilia Ikulu ilikuwapo sanamu ya Leopold 11, “muasisi “ wa nchi ya Kongo, ikikejeli kwamba uhuru huu hautabadilisha chochote.

Mfalme Baudouin wa Ubelgiji alikuwa wa kwanza kuhutubia, na akaonyesha mazuri yaliyofanywa wakati wa ukoloni. “Uhuru wa Kongo ni matokeo ya juhudi za Mfalme Leopold 11 kwa hiyo, mjihadhari msije mkabadili mifumo ambayo tunawakabidhi leo mpaka mkiwa na uhakika kuwa mtafanya vizuri zaidi kuliko sisi… msihofu tuko pamoja na tutajenga uwezo wenu wakujitawala…”

Baada ya Mfalme ikawa zamu ya Joseph Kasa -Vubu, Rais wa kwanza wa Kongo naye aliwafurahisha wakoloni aliposema hata kama wao Waafrika watashika madaraka lakini nyuma ya pazia wazungu wataendelea kuongoza ili mambo yasiharibike. Baada ya Rais Kasa -Vubu kuongea, Spika Joseph Kasongo alimkaribisha Waziri Mkuu Patrice Lumumba, akiwa na umri wa miaka 35 atoe hotuba yake.

Mfalme na waziri wake mkuu Gaston Eyskens wakashikwa na butwaa kwa kuwa Lumumba hakuwepo kwenye ratiba na wala hawakupata nakala ya hotuba yake, japo waandishi wa habari waligawiwa. Maneno yaliyokuwa kwenye hotuba yake yalifanya damu zao zigande. Hotuba ya Lumumba ilikuwa kwa ajili ya Wakongo waliopigana kupata uhuru na kushinda. Sherehe ikahamia katika kuwaenzi Wakongo badala ya wakoloni.

Wakongo waliambiwa kwamba uhuru walioupata si fadhila za Brussels kama Mfalme anavyotaka waamini na si matokeo ya makubaliano kati yao na Ubelgiji. Lumumba alisema “Hakuna Mkongo mwenye heshima yake anaweza kusahau kwamba ni harakati zetu ndio zimetufikisha hapa. Tumepambana kila siku, harakati za dhati…na kila tone la damu lilikuwa ni sehemu ya mapambano.”

Lumumba aliukashifu ukoloni uliosifiwa na Baudouin, kwamba ni utumwa uliosokomezwa kwa Wakongo. Aliendelea kusema; “Tulichoambulia katika ukoloni ni kejeli na matusi, tumevumilia ngumi tangu machweo mpaka kuchwa kwa kuwa sisi ‘nyani’. Nani atasahau kwamba mtu mweusi alikua anaitwa “wee” kwa dharau. Tumeshuhudia jinsi ardhi yetu ilivyonajisiwa na sheria dhalimu ambazo zimewapendelea wazungu wachache.

Tumeshuhudia wazalendo wanaopigania haki na utu wakiwa wakimbizi ndani ya nchi yao, adhabu ambayo ni kubwa kuliko kifo…nani atasahau milio ya bunduki na kaka zetu waliouwawa na jela zilizojaa wanamapinduzi waliokataa utawala wa dhuluma wa wakoloni. Wabelgiji wasingeweza kuzuia uhuru wetu.”

Lumumba alishangiliwa sana na hotuba yake ilikatishwa mara kwa mara; Kongo nzima ilipata habari ya namna Lumumba alivyotema cheche mbele ya Wabelgiji. Kaongea lugha ambayo Wakongo hawakuamini inawezekana mbele ya wazungu. Kwa Wakongo ilikuwa kama zawadi kwa miaka 80 ya utawala wa wabelgiji. Kwa mara ya kwanza Mkongo kazungumza kuashiria ujenzi wa historia ya Kongo mpya na kutia ragba kwa Wakongo kwamba wanastahili kujithamini, kujiamini na kujitawala.

Wakoloni walibaki na mshangao na Brussels ghafla ikajikuta ana kwa ana na mapinduzi iliyokua inayahofia. Ukoloni ulionadiwa na Mfalme kama biashara nzuri, ukanyambuliwa na Lumumba kuwa ni utumwa mbele ya wakoloni wenyewe. Majuma machache kabla, wakoloni walimnanga Lumumba kwamba ni ngumbalo, limbukene, nyani aliepaishwa juu kama jiwe kwenye manati.

Wakati Lumumba anaendelea kutema cheche kulikua na kanali Frederic Vandewalle kiongozi wa upelelezi, ambaye alikuwa anamsikiliza kwa makini. Japo hakupenda maudhui ya hotuba ya Lumumba, alielewa kuwa hayo ndiyo maoni ya wa Kongo wanataka kusikia kutoka kwa viongozi wao. Vandewalle ameandika katika kitabu chake “Siku 1004” jinsi umma wa Kongo ulivyotaka uhuru wao uwe wa dhati na ujidhihirishe katika maisha bora.

Je, Vandewalle alikua ni nani Kongo baada ya Uhuru na kwa nini Moise Tshombe na msafara wake walivutiwa nae? Ni kwa vipi alikua adui hatari wa uhuru wa Kongo? Kwa nini baada ya kustaafu na Kongo kuingia katika machafuko Vandewalle alihitajika tena Kongo?

Sehemu ya pili ya muendelezo wa makala haya tutaona jinsi mwaka 1960 ulivyokuwa wa mafanikio kwa Lumumba lakini pia wenye maafa makubwa. Mwaka 1959 alikuwa jela Katanga, Mei akashinda uchaguzi, Juni Waziri Mkuu. Septemba, akapinduliwa na kuwa chini ya ulinzi, aliuwawa17 Januari 1961.

Inaendelea
 
Ho











Hotuba ya Patrice ilibeba ujasiri na ukweli usiopingika juu ya mateso ya wana Kongo na Afrika wa ujumla
 
[bar-uh-koo-duh]
noun, plural (especially collectively)
bar·ra·cu·da, (especially referring to two or more kinds or species) bar·ra·cu·das
for 1; bar·ra·cu·das for 2.
1. any of several elongated, predaceous, tropical and subtropical marine fishes of the genus Sphyraena, certain species of which are used for food.
2. Slang . a treacherous, greedy person.
 
[bar-uh-koo-duh]
noun, plural (especially collectively)
bar·ra·cu·da, (especially referring to two or more kinds or species) bar·ra·cu·das
for 1; bar·ra·cu·das for 2.
1. any of several elongated, predaceous, tropical and subtropical marine fishes of the genus Sphyraena, certain species of which are used for food.
2. Slang . a treacherous, greedy person.
tafsiri mkuu
 
Oparesheni Barakuda yarudi Afrika II


JUMA lililopita tuliona kitendo cha kumfunga Lumumba na wenzie mwaka 1959 kilifanya Wakongo wapandwe na ari zaidi katika kudai uhuru kamili. Januari, 1960 Serikali ya Eyskens ikasalimu amri na kutangaza Juni 30, mwaka 1960 Kongo itapata uhuru baada ya kushinda vikwazo vingi vya wakoloni isipokuwa kimoja tu.


Wabelgiji walipoiteka Kongo walisingizia eti ni kuokoa maisha ya waafrika kutoka kwa wafanyabiashara ya utumwa wa kiarabu. Kabla ya Juni 30, mwaka 1960, wakoloni wakatambua, kwa nguvu za umma, Lumumba ataongoza Serikali. Ndipo Bunge lao bila idhini ya Wakongo walibadili kipengele kwenye Katiba kuigawa Kongo kimajimbo.


Lumumba alitaka uhuru wa kiuchumi tangu siku ya kwanza ya uhuru. Akasema; “Tutahakikisha ardhi yetu inawafaidisha watoto wetu. Tutafanya tathmini ya sheria zote na kutunga zingine kwa kuzingatia haki na usawa… Wakongo washike hatamu katika kila sekta” na katika hili la hatamu akaanzia afrikanaizsheni jeshini. Hili liliwakera wakoloni.


Wazungu wakuzua propaganda kuwa majeshi ya Lumumba yanawabaka wanawake, na wazungu wanakimbia vikosi vyake katili. Ubeligiji ikatuma majeshi Jimbo la Katanga na machafuko ya Kongo yakaanza Julai 10, mwaka 1960 na siku iliyofuata Julai 11, Jimbo la Katanga lenye tajiri wa madini likajitenga.


Mataifa yenye nguvu za kijeshi ya Magharibi yalibariki “WAASI’ na kumbana Lumumba kwa hila na kwa wazi. Safari hii ilikuwa kuiokoa Afrika kutoka ubeberu wa Wakomunisti! Lumumba hakuwa mkomunisti, alikuwa kiongozi mzalendo lakini walichotaka ‘wakoloni’ ni rasimali za Kongo..


Kikosi cha Belgo-Katanga kilizuia ndege iliyo mchukua Kasa Vubu na Lumumba, isitue Katanga kwa hofu ya kuenea kwa vuguvugu la uzalendo. Lakini migomo ilienea na Balozi wa Ubelgiji, Jean Bosch, akafoka vuguvugu lazima lizimwe na akaanza kutafuta kiongozi atakae shika nchi baada ya kumg’oa Lumumba.


Akampata waziri mmoja wa Lumumba, Justin Bomboko ambaye alikuwa anapeleka taarifa zote ubalozini. Julai 12, mwaka 1960 Serikali ya Lumumba ikatuma simu UNO (Umoja wa Mataifa) kuomba msaada wa kukabiliana na waasi na majeshi vamizi ya kigeni. Katibu Mkuu wa UNO, Dag Hammarskjold, akaueleza ujumbe wa Ubelgiji kwamba “…kama jeshi la wazungu litaingilia, itakua ni kuhalalisha kinachoendelea huko” akimaanisha maasi.


Julai 14, mwaka 1960, Baraza la Usalama likaunda kikosi cha UNO kuisaidia Serikali ya Kongo hadi pale itapotengemaa. Ubelgiji iliondoa askari wake na ikaendelea kuimarisha waasi na hakuna aliyeishutumu. Hammerskjold aliwawekea ‘mikwara’ wote waliotaka kumsaidia Lumumba kwamba wapitishe misaada yao UNO.


Naibu Waziri Mkuu, Antonie Gizenge, alifoka “Wakongo hatuelewi, iweje sisi watendwa katika nchi yetu, tunanyang’anywa na kunyimwa silaha, Ubelgiji ambao ni wavamizi wana silaha….UNO inaruhusu waasi ambao tumewatangaza si halali wajizatiti na Wabelgiji watambe kama Kongo kwao!”


Wakati Lumumba anaendelea kutema cheche Wabelgiji walimuajiri kanali Frederic Vandewalle, kiongozi wa ujasusi kabla ya uhuru aje kuongoza shughuli za maasi. Huyu aliijua Kongo na Wakongo na nyuma ya pazia alifanya kazi kubwa na chafu katika kusambaratisha Serikali ya Lumumba. Mengi ameandika katika kitabu chake kiitwacho “Siku 1004.”


Hammerskjold baada ya kuzongwa sana akawaambia wasaidizi wake kwamba atashauriana na Tshombe ili amhakikishie hatakuwa amepoteza malengo kwa kukukubali majeshi ya UNO. Malengo gani hayo? Picha iliyojengwa ni kwamba Kongo haitawaliki chini ya Lumumba na kuna hatari ya kupoteza mashamba, viwanda na shughuli za kibiashara.

Mfalme Baudounin naye alimponda Lumumba na kumsifia Tshombe kwamba ni mwaminifu, kwa hiyo Ubelgiji ina wajibu wa kumsaidia na UNO kamwe isikubali kuitoa Katanga kwa Serikali ya Kongo. Magazeti kama De Standaard la Julai 16, 1960 liliandika; “Lumumba ni mwanamapinduzi anayetaka kuleta vurugu na fujo, wakati Katanga kuna utulivu na amani kutokana na msaada wa wazungu.”

Julai 26, 1960 likaandika; “ili kuikoa Kongo ni lazima wenye msimamo mkali waondoke ….na kila jimbo lijitawale….” La Libre Belgique lilipakaza Julai 19, 1960 kwamba Lumumba alipokua Marekani alilala nyumba ya wageni wa kiserikali, “… na mtumishi wa pale ni mwanamke, mzee, mzungu. Sijui kama huyo mama atasalimika!”

Marcel de Corte, msomi wa falsafa ya maadili mema alitaka Lumumba auawe akijenga hoja kwamba “…ni mnyama… maafisa wa kibelgiji wanalia kwa hasira kwa sababu wanazuiwa kummaliza” La Gauch baada ya kuuwawa kwa akina Lumumba liliandika Machi 4, 1961; “Vyombo vya habari vimekuwa na hasira na Lumumba kuliko hata Hitler!”

Maasi yaliendelea , Agosti 9, 1960 Kusai Kusini ilijitangazia uhuru chini ya Albert Kalonji. Ilibidi Serikali ya Kongo ichukue hatua dhidi ya vyombo vya habari ambavyo viliunga mkono maasi. Ubelgiji ikadai Lumumba anakandamiza uhuru wa habari na sasa ni utawala wa kipolisi na maisha ya wengi yako hatarini.

Agosti 12, 1960 Hammerskjold alitua Kongo kuzungumza na Tshombe, na walidai UNO ichukue nafasi ya majeshi ya Ubeligiji, ili ya Serikali yasiingilie Katanga. Na kama jeshi la Serikali litaingilia, itabidi UNO iwe upande wa waasi.

Hammerskjold aliambiwa wazi na msaidizi wake Bunche, “Tshombe ni kibaraka wa Belgiji na bila UNO asingethubutu kuasi” lakini hakusikiliza kwani msimamo wa wazungu ulikuwa ni kuisambaratisha Serikali ya Kongo na Julai 26, 1960 Hammerskjold alimtambua muasi Tshombe kiongozi halali wa Katanga.

Agosti 15, 1960 Lumumba alimwandikia Hammerskjold wakati yuko Kongo; “…baada ya kuongea na waziri wa nje Ubelgiji, …..na kudharau serikali ya Kongo… watu na serikali ya Kongo tumepoteza imani na Katibu Mkuu Hammerskjold … tunachohitaji ni waangalizi huru waje waangalie hali halisi ya Kongo… na majeshi ya Afrika na Kongo.”

Gazeti la The Times la Agosti 16, 1960 liliandika Hammerskjold alionyesha wasiwasi kuhusu uhalali wa Lumumba kuongea kwa niaba ya Serikali na akamwandikia Rais Kasa Vubu “… tunaimani na busara zako na UNO itaendelea kutoa ushirikiano alimradi masuala ya utaifa na rangi yazingatiwe ili kufikia lengo letu…”

Kwa kutelekezwa na UNO, Lumumba aliwajibika kuzima fujo na uvunjwaji wa sheria uliofanywa na waasi. Agosti 22 na 23, 1960 askari 1,000 wa Serikali walielekea Kusai na Wabelgiji walijua majimbo yote yanawafuasi wazalendo.


Septemba mosi, 1960 Mobutu Mnadhimu Mkuu aliamua kusitisha vita Kasai bila kushauriana na Serikali. Ndege za majeshi ya Serikali zilihujumiwa na UNO ilikataa kuwapa mafuta. Wakati huohuo, kulikuwa na mipango ya kumpindua Lumumba. Septemba 5, 1960 Lumumba alivuliwa madaraka, na kwa msaada wa UNO viongozi wapya wa kisiasa na kijeshi wakasimikwa Mobutu akiwamo.


Machafuko ya Kongo mwaka 1960 hadi 1964 yanadhihirisha UNO ilikubali kutumiwa na nchi za Magharibi kumpindua na hatimaye kumuua Lumumba. Nchi hizo ziliamini kwamba Lumumba aliwakilisha hatari kubwa zaidi katika kufanikisha mipango ya kuitawala kiuchumi Afrika.

Rais wa Marekani Eisenhower, Waziri Mkuu wa Uingereza na mawaziri wao wa nje walijiuliza; “Kwa nini hatumuui Lumumba sasa? Kama atarudi madarakani kutakuwa na shinikizo kuhusu suala la Katanga, ambalo litatuletea mgogoro wa kisheria… sasa ndio wakati mzuri wa kumshughulikia Lumumba”. Juma lijalo tutaona jinsi Lumumba alivyosalitiwa na taadhira ya kifo chake kwa Afrika


Oparesheni Barakuda


“Hillary Clinton alipotembelea Jamhuri ya Kidemokrasia ya watu Kongo (DRC) Agosti, 2009 aliwashangaza raia wa Kongo alipowaambia wasahau yaliyopita wasonge mbele. Swali ni je, Marekani iko tayari kusahau Septemba 11, na kusonga mbele?” Ndivyo alivyoandika Prof. Georges Nzongola –Ntalaja kwenye Jarida la The Africa Report la Aprili-Mei, 2010.

Waafrika tumesamehe mengi, lakini kamwe hatutasahau madhila na madhara ya biashara ya Utumwa na Ukoloni. Kila kukicha tunakumbushwa utumwa wa kisiasa, kiuchumi na kijamii. Bw. Yesu alisema; “Akupigae shavu la kulia, mgeuzie na la kushoto”. Huwa najiuliza ukisha mpa yote mawili inakuaje?

Waafrika ni taifa moja kwa hiyo yanayotokea kote Afrika yanatuhusu sote. Kwa nini hatushangai Marekani yenye nchi /majimbo zaidi ya 50 au Umoja wa Ulaya nchi zaidi ya 20, zinaongea kwa pamoja na nchi zetu mmoja mmoja.

Hivi hatuoni hili peke yake ni tatizo, hata kama Gaddafi “asingewaswaga” kama baadhi ya viongozi wa Afrika wanavyodai? Mpaka lini kiongozi wa Afrika ataendelea kuvumilia unyonge wakusimama peke yake mbele ya nchi za Marekani au Ulaya katika masuala ambayo yanatuumiza waafrika wote? Je, tunasubiri idhini yao na kibaraka wao ndio tuzinduke?

Tuna changamoto ya kuchanganya “ kusamehe na kusahau”. Kusamehe ni rahisi kwani mtu anaweza kukutia kovu kwa kukusudia au kwa bahati mbaya, ukamsamehe. Lakini itakuwa ni unafiki ukisema utasahau, kwani kovu litakukumbusha. Je mtu huyo akikuumiza tena utafanyaje?

Historia inatabia ya kujirudia ndio maana matukio yote yanaandikwa ili kila kizazi kielewe na kisibweteke. Inaelekea Waafrika tu ndio mabingwa wakusamehe na kusahau. Viongozi wetu wengi wameuawa kikatili na kwa njama; Patrice Emery Lumumba wa Kongo mpaka leo damu yake haijakauka.

Oparesheni Barakuda ya kumuua Patrice Lumumba ni mfano hai kuwa wajukuu wa wakoloni hawabweteki. Udhalimu na dhuluma vipo, kusahau na kusonga mbele bila kujihami ni usaliti.

Marekani wanakumbuka 11.09.2001 na kuhakikisha haitokei tena, Wayahudi wanakumbuka, ili kila kizazi chao kiape yasitokee tena. Iweje sisi na kwa utakatifu gani, tusahau? Kwa nini tunawaandalia watoto na wajukuu wetu utumwa wa hiyari ?

Raoul Peck alitoa maoni yake kuhusu kitabu cha “Mauaji ya Lumumba” kilicho andikwa na Ludo de Witte “…ni hadithi isiyo isha, yenye kujaa dharau, uroho na utemi. Wauaji bado wako kati yetu.” Kila Mwafrika ni lazima akumbuke, yaliyotokea kwa Lumumba ni ushahidi dunia imejaa wanywadamu. Miaka 50 ya Uhuru itukumbushe ufashisti wa kiuchumi uliosababisha Lumumba auwawe Januari 17, mwaka 1961 na Gaddafi Oktoba 20, mwaka 2011. Ludo de Witte anatueleza kwa ufasaha mambo yalivyokuwa Kongo Juni 30, mwaka 1960.

Anasema wageni kutoka nje na ndani ya Kongo na waandishi wa habari walikusanyika Ikulu mjini Leopoldville. Katika lango kuu la kuingilia Ikulu ilikuwapo sanamu ya Leopold 11, “muasisi “ wa nchi ya Kongo, ikikejeli kwamba uhuru huu hautabadilisha chochote.

Mfalme Baudouin wa Ubelgiji alikuwa wa kwanza kuhutubia, na akaonyesha mazuri yaliyofanywa wakati wa ukoloni. “Uhuru wa Kongo ni matokeo ya juhudi za Mfalme Leopold 11 kwa hiyo, mjihadhari msije mkabadili mifumo ambayo tunawakabidhi leo mpaka mkiwa na uhakika kuwa mtafanya vizuri zaidi kuliko sisi… msihofu tuko pamoja na tutajenga uwezo wenu wakujitawala…”

Baada ya Mfalme ikawa zamu ya Joseph Kasa -Vubu, Rais wa kwanza wa Kongo naye aliwafurahisha wakoloni aliposema hata kama wao Waafrika watashika madaraka lakini nyuma ya pazia wazungu wataendelea kuongoza ili mambo yasiharibike. Baada ya Rais Kasa -Vubu kuongea, Spika Joseph Kasongo alimkaribisha Waziri Mkuu Patrice Lumumba, akiwa na umri wa miaka 35 atoe hotuba yake.

Mfalme na waziri wake mkuu Gaston Eyskens wakashikwa na butwaa kwa kuwa Lumumba hakuwepo kwenye ratiba na wala hawakupata nakala ya hotuba yake, japo waandishi wa habari waligawiwa. Maneno yaliyokuwa kwenye hotuba yake yalifanya damu zao zigande. Hotuba ya Lumumba ilikuwa kwa ajili ya Wakongo waliopigana kupata uhuru na kushinda. Sherehe ikahamia katika kuwaenzi Wakongo badala ya wakoloni.

Wakongo waliambiwa kwamba uhuru walioupata si fadhila za Brussels kama Mfalme anavyotaka waamini na si matokeo ya makubaliano kati yao na Ubelgiji. Lumumba alisema “Hakuna Mkongo mwenye heshima yake anaweza kusahau kwamba ni harakati zetu ndio zimetufikisha hapa. Tumepambana kila siku, harakati za dhati…na kila tone la damu lilikuwa ni sehemu ya mapambano.”

Lumumba aliukashifu ukoloni uliosifiwa na Baudouin, kwamba ni utumwa uliosokomezwa kwa Wakongo. Aliendelea kusema; “Tulichoambulia katika ukoloni ni kejeli na matusi, tumevumilia ngumi tangu machweo mpaka kuchwa kwa kuwa sisi ‘nyani’. Nani atasahau kwamba mtu mweusi alikua anaitwa “wee” kwa dharau. Tumeshuhudia jinsi ardhi yetu ilivyonajisiwa na sheria dhalimu ambazo zimewapendelea wazungu wachache.

Tumeshuhudia wazalendo wanaopigania haki na utu wakiwa wakimbizi ndani ya nchi yao, adhabu ambayo ni kubwa kuliko kifo…nani atasahau milio ya bunduki na kaka zetu waliouwawa na jela zilizojaa wanamapinduzi waliokataa utawala wa dhuluma wa wakoloni. Wabelgiji wasingeweza kuzuia uhuru wetu.”

Lumumba alishangiliwa sana na hotuba yake ilikatishwa mara kwa mara; Kongo nzima ilipata habari ya namna Lumumba alivyotema cheche mbele ya Wabelgiji. Kaongea lugha ambayo Wakongo hawakuamini inawezekana mbele ya wazungu. Kwa Wakongo ilikuwa kama zawadi kwa miaka 80 ya utawala wa wabelgiji. Kwa mara ya kwanza Mkongo kazungumza kuashiria ujenzi wa historia ya Kongo mpya na kutia ragba kwa Wakongo kwamba wanastahili kujithamini, kujiamini na kujitawala.

Wakoloni walibaki na mshangao na Brussels ghafla ikajikuta ana kwa ana na mapinduzi iliyokua inayahofia. Ukoloni ulionadiwa na Mfalme kama biashara nzuri, ukanyambuliwa na Lumumba kuwa ni utumwa mbele ya wakoloni wenyewe. Majuma machache kabla, wakoloni walimnanga Lumumba kwamba ni ngumbalo, limbukene, nyani aliepaishwa juu kama jiwe kwenye manati.

Wakati Lumumba anaendelea kutema cheche kulikua na kanali Frederic Vandewalle kiongozi wa upelelezi, ambaye alikuwa anamsikiliza kwa makini. Japo hakupenda maudhui ya hotuba ya Lumumba, alielewa kuwa hayo ndiyo maoni ya wa Kongo wanataka kusikia kutoka kwa viongozi wao. Vandewalle ameandika katika kitabu chake “Siku 1004” jinsi umma wa Kongo ulivyotaka uhuru wao uwe wa dhati na ujidhihirishe katika maisha bora.

Je, Vandewalle alikua ni nani Kongo baada ya Uhuru na kwa nini Moise Tshombe na msafara wake walivutiwa nae? Ni kwa vipi alikua adui hatari wa uhuru wa Kongo? Kwa nini baada ya kustaafu na Kongo kuingia katika machafuko Vandewalle alihitajika tena Kongo?

Sehemu ya pili ya muendelezo wa makala haya tutaona jinsi mwaka 1960 ulivyokuwa wa mafanikio kwa Lumumba lakini pia wenye maafa makubwa. Mwaka 1959 alikuwa jela Katanga, Mei akashinda uchaguzi, Juni Waziri Mkuu. Septemba, akapinduliwa na kuwa chini ya ulinzi, aliuwawa17 Januari 1961.

Inaendelea
 
Back
Top Bottom