Ombi la kusaidiwa

Ombi la kusaidiwa

Mkyamise

JF-Expert Member
Joined
Apr 14, 2014
Posts
526
Reaction score
677
Habari za leo ndg wanaJF? Mimi ni Mwanafunzi wa Chuo kikuu kimoja kilichopo kanda ya ziwa.

Ninasoma mwaka wa tatu na nipo semester ya mwisho. Ninafahamu sheria na taratibu za hapa ndio maana ninajaribu kujiweka wazi.

Ninajisomesha mwenyewe toka mwaka wa kwanza hadi hapa nilipofika. Tatizo linalonisibu mpaka kunisukuma kuja hapa JF ni kukosa ada ya kulipia semester hii ya mwisho.

Kwa kweli nimejitahidi kutafuta kwa ndg, jamaa na marafiki hali imekuwa ngumu. Nimekuwa nikijilipia kutoka kwenye kazi niliyokuwa nafanya kable ya kuja chuoni na michango kutoka kwa ndugu na jamaa.

Ninadaiwa jumla shilingi 880,000/= kama ada ya semester ya pili (630,000/=), Hostel (150,000/=) na fine kwa kuchelewesha malipo haya (100,000/=) Fine hii imekuja kwa sababu mwisho wa kulipa michango hii ilikuwa ni tarehe 30/04/2018.

Wakati wote nilikuwa nahangaika huku na kule bila mafanikio mpaka fine ikanikuta na sina option nyingine mpaka sasa. Mpaka kuamua kuja hapa naomba mjue kweli hali imekuwa mbaya.

Mpaka sasa nina uhakika wa kupata shilingi laki mbili kutoka kwa jamaa yangu mmoja ambaye ameniahidi.

Kwa hiyo kutakuwa na pungufu ya 680,000/= Ndg zangu, bila kulipa kiasi hiki cha fedha sitaruhusiwa kufanya mtihani wa mwisho wa semester hii (UE).

Mitihani hii tunatarajia itaanza mwezi wa saba. Ninakuja kwenu ndg zangu nikiomba mnisaidie Watanzania wenzangu. Kadiri utakavyoguswa ninakuomba unisaidie kwa chochote.

Wengine wanaweza kushauri niuze simu lkn ninatumia simu ndogo na hapa nimetuma habari hii kwa kuomba modem na computer kwa wenzangu.

Ninaomba msaada wenu Watanzania. Ninaahidi kuleta risiti za malipo haya hapa pindi nitakapofanikiwa kupata kiasi hiki cha fedha mara moja na kukiweka kwenye akaunti ya chuo.

Kama utaona inafaa naomba unitumie kwenye simu yangu 0767151519.

Asanteni.
 

Attachments

  • IMG_20180510_202515.jpg
    IMG_20180510_202515.jpg
    84.6 KB · Views: 64
  • IMG_20180510_202530.jpg
    IMG_20180510_202530.jpg
    82.1 KB · Views: 55
  • IMG_20180510_202553.jpg
    IMG_20180510_202553.jpg
    87.2 KB · Views: 62
Hivi ni kwamba kiwango cha elimu kimeshuka au ni kitu gani..??

Mtu unaomba msaada alafu unafichaficha vitu au uweki details za kina.

Nasoma chuo kimoja kanda ya ziwa...!!!!nini maana yake..??
Weka Jina la Chuo,Jina lako na risiti zako za malipo toka mwaka wa kwanza mpaka sasa.

Yani ungekuwa karibu ningekucharaza viboko wewe...
 
Weka jina lako kamili,chuo unachosoma,registration number yako,course unayosoma,account number ya chuo na benk ya kulipia nikakulipia ada,utapata pay in slip utakayokwenda kubadilisha accounts na kupata receipts na kunipa feedback,simple like that!
 
Ninashukuru kwa maoni yenu. Kuhusu vielelezo, naomba mnipe muda niombe smartphone ili nipige picha nitavi-upload hapa. Kadhalika huyu mwanaJF uliyeomba risiti za mwaka wa kwanza hadi sasa zingine zipo nyumbani. Hapa ninazo za semester iliyopita tuu. Asanteni
 
Mkuu ungeambatanisha hata na vielelezo vyako ili kusapoti maelezo uliyotoa,humu matapeli wengi siku hizi
Asante ndg yangu. Naomba nipate muda niombe smartphone nivipige picha nitaviweka hapa
 
Ninashukuru kwa maoni yenu. Kuhusu vielelezo, naomba mnipe muda niombe smartphone ili nipige picha nitavi-upload hapa. Kadhalika huyu mwanaJF uliyeomba risiti za mwaka wa kwanza hadi sasa zingine zipo nyumbani. Hapa ninazo za semester iliyopita tuu. Asanteni
Hizo hizo za semester iliopita wewe ziweke zitatosha
 
Ungeweka details zako zote kwani kuomba sio vby, a bergar has no choice bloke. Sasa chuo flan,weka details zako zote hata ukiweza picha kwani nini bana
 
Weka jina lako kamili,chuo unachosoma,registration number yako,course unayosoma,account number ya chuo na benk ya kulipia nikakulipia ada,utapata pay in slip utakayokwenda kubadilisha accounts na kupata receipts na kunipa feedback,simple like that!
Ninashukuru ndg yangu kwa moyo na utayari wako wa kunisaidia bila kujali. Nimekujibu inbox
 
Nina
Ungeweka details zako zote kwani kuomba sio vby, a bergar has no choice bloke. Sasa chuo flan,weka details zako zote hata ukiweza picha kwani nini bana
shukuru ndg. Nimeomba nipate muda ili niombe smartphone nipige vielelezo picha ili niviweke hapa. Asante.
 
Hivi ni kwamba kiwango cha elimu kimeshuka au ni kitu gani..??

Mtu unaomba msaada alafu unafichaficha vitu au uweki details za kina.

Nasoma chuo kimoja kanda ya ziwa...!!!!nini maana yake..??
Weka Jina la Chuo,Jina lako na risiti zako za malipo toka mwaka wa kwanza mpaka sasa.

Yani ungekuwa karibu ningekucharaza viboko wewe...[/QUOTE
Asante kwa maoni yako ndg yangu. Nimeomba kuwa nitaviweka hapa very soon. Ila baadhi siko navyo hapa nilipo. Nitaweka vichache nilivyo navyo hapa. Ubarikiwe sana.
 
Hapa nakumbuka mwaka fulani nilipatwa na shida nikawa naomba kusaidiwa ,nilikuwa muwazi kiasi kwamba ndani ya siku mbili tu nilikuwa nimeshakifikia nilichokuwa nakihitaji
 
Habari za leo ndg wanaJF? Mimi ni Mwanafunzi wa Chuo kikuu kimoja kilichopo kanda ya ziwa.

Ninasoma mwaka wa tatu na nipo semester ya mwisho. Ninafahamu sheria na taratibu za hapa ndio maana ninajaribu kujiweka wazi.

Ninajisomesha mwenyewe toka mwaka wa kwanza hadi hapa nilipofika. Tatizo linalonisibu mpaka kunisukuma kuja hapa JF ni kukosa ada ya kulipia semester hii ya mwisho.

Kwa kweli nimejitahidi kutafuta kwa ndg, jamaa na marafiki hali imekuwa ngumu. Nimekuwa nikijilipia kutoka kwenye kazi niliyokuwa nafanya kable ya kuja chuoni na michango kutoka kwa ndugu na jamaa.

Ninadaiwa jumla shilingi 880,000/= kama ada ya semester ya pili (630,000/=), Hostel (150,000/=) na fine kwa kuchelewesha malipo haya (100,000/=) Fine hii imekuja kwa sababu mwisho wa kulipa michango hii ilikuwa ni tarehe 30/04/2018.

Wakati wote nilikuwa nahangaika huku na kule bila mafanikio mpaka fine ikanikuta na sina option nyingine mpaka sasa. Mpaka kuamua kuja hapa naomba mjue kweli hali imekuwa mbaya.

Mpaka sasa nina uhakika wa kupata shilingi laki mbili kutoka kwa jamaa yangu mmoja ambaye ameniahidi.

Kwa hiyo kutakuwa na pungufu ya 680,000/= Ndg zangu, bila kulipa kiasi hiki cha fedha sitaruhusiwa kufanya mtihani wa mwisho wa semester hii (UE).

Mitihani hii tunatarajia itaanza mwezi wa saba. Ninakuja kwenu ndg zangu nikiomba mnisaidie Watanzania wenzangu. Kadiri utakavyoguswa ninakuomba unisaidie kwa chochote.

Wengine wanaweza kushauri niuze simu lkn ninatumia simu ndogo na hapa nimetuma habari hii kwa kuomba modem na computer kwa wenzangu.

Ninaomba msaada wenu Watanzania. Ninaahidi kuleta risiti za malipo haya hapa pindi nitakapofanikiwa kupata kiasi hiki cha fedha mara moja na kukiweka kwenye akaunti ya chuo.

Kama utaona inafaa naomba unitumie kwenye simu yangu 0767151519.

Asanteni.
Ndg Watanzania, nimeshaweka picha za risiti za malipo ya ada na accomodation pamoja na kitambulisho changu cha mtihani niliyofanya last semester. Vithibitisho vingine vipo mbali na hapa nilipo kwa sasa. Asanteni.
 
Hapa nakumbuka mwaka fulani nilipatwa na shida nikawa naomba kusaidiwa ,nilikuwa muwazi kiasi kwamba ndani ya siku mbili tu nilikuwa nimeshakifikia nilichokuwa nakihitaji
Mkuu tayari nimeweka baadhi ya risiti za malipo niliyofanya last semester pamoja na ID ya mtihani. Hopeful mtanielewa Watanzania.
 
Back
Top Bottom