Ombi la kazi/ kibarua

Joined
Jul 6, 2025
Posts
14
Reaction score
19
Salaam za heshima,
Natumaini ujumbe huu unawafikia mkiwa salama.

Mimi ni kijana wa kiume, mwenye umri wa miaka 26, ninaishi Mbagara Kuu. Elimu yangu ni kidato cha nne.

Naomba kazi au kibarua chochote halali kinachopatikana, kama vile:

Kuuza dukani

Uwinga

Kufanya usafi kwenye ofisi au maeneo mbalimbali

Kazi yoyote ya mikono iliyo halali


Niko tayari kufanya kazi kwa bidii, uaminifu na kujituma bila kuchagua kazi.

Hitimisho:
Naomba tusaidiane kwa sababu hali ya maisha ni ngumu sana mtaani, hasa sisi vijana wasio na kazi au kibarua chochote, tunapitia changamoto kubwa na wakati mwingine kudharaulika. Msaada wowote au taarifa ya kazi nitashukuru sana.
 
Mkuuu kazi hizo duuh ni ngumu ungepambana kwenye saidia fundi au mcheki huyu dada Seran
 
Mbagala kuu kuna wanga sana huko vijana wanaishia kuwa bodaboda. Uwinga pia sio kaz ya kuomba, ni kaz ya kuamua
 
Kama dakika 20 nikukute kituoni kwa damu damu...Kuna rumio nyeusi ukiiona njoo..

Now nipo natoka chamazii narud kwangu kigamboni..
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…