Observational study: CCM kubeba ubunge Karatu

bato

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2012
Posts
3,960
Reaction score
3,474
Wilaya ya Karatu ni kati ya wilaya chache za mwanzo zilizokubali mageuzi.

Imekuwa ni mfano Wa kuigwa kwa wanamageuzi.Kwa muda mrefu ni marejeo hasa kwa CDM jinsi upinzani ulivyoleta nafuu kwa maisha ya wananchi.

Ni Halmashauri ya kwanza kufuta kodi ya kichwa,ya baiskeli(shagingi la mkulima),ya Mama Wafanyabiashara barabarani,ya mifugo.Wengine wakaiga.

Kwa siku hizi za karibini mwamko Wa wananchi umekuwa chini sana kwa CDM baada EL kuingia CDM,hatimaye kuwa mgombea urais.

Wana CDM wanashindwa kujibu mashambulizi kutoka kwa watani zao CCM kuhusu ujio Wa EL.Pia CCM kumleta mgombea makini DR Wilbert Lorri. Enzi za CDM Karatu inafikia ukingoni.

Ni tahadhari tu kwa CDM mpya.
 
Dr Lorri alishakataliwa siku nying ni mtu wa kurudi karatu wakati wa uchaguzi pole yako
 

Wilbert Slaa Lori alipiga sana hela za miradi ya food aid.
 
N​goja aje apambane na mzigo mzito wa Dr W. Peter Slaa ndo atajua maumivu ya kushindwa.
 
Nadhani Huwajui wana Karatu si watu wa kuyumba yumba kama unavyotaka kujinasibu, Tuulize sisi wanakaratu wenyewe tangu enzi za TANU. Tulieni tu sindano iingie. Tunachowashangaa wana CCM ni kubadilika na kuwa maafisa habari wa CHADEMA kuhusu suala la Dk. Slaa. Kama mnao uhakika kwa nini kuanza kutoa siri za ushindi wenu? Ningekuwa upande wenu CCM ningekaa kimya kabisa kama alivyowahi kufanya Mh. Lowassa tangu alipojiuzulu na Bungeni alikaa kimya tu. Leo baada ya kufanya uamuzi sahihi na Uamuzi Mgumu naona mmeanza kuyumba ikiwa ni pamoja na akina Prof. Dr. Bana.

Tuache suala la muda lichukue wajibu wake. "Time will tell"
 
Dr. Lorry labda agombee Dar es salam huko anakoishi. Labda CCM wamweke mtu anayefahamu Karatu na ana mapenzi kwa Karatu
 
Wana CDM Karatu wanakosa hoja za kumtetea EL. CCM wanahoji kuwa kwa nini awe fisadi,halafu awe kamanda muadilifu akiwa CDM. Ni hoja tu,si matusi. Ukweli mchungu kwa CDM ni kuwa Jimbo la Karatu ni ngumu kuitetea.
 
Mi naona kwa vile muda uliobaki ni mdogo, wabunge wa chadema wapigiwe kura popote wanapogombea, hata karatu, ila za uraisi kwa Lowasa hapana. Ziende kwa Magufuli. Lowasa anautaka urais kwa nguvu, na kwa gharama yoyote, kuna walakini na hilo. Hatujui anataka nini hasa. Hakuna sababu ya kupoteza kura kumpigia mtu ambaye ana hila zake.
 
Dr. Lorry labda agombee Dar es salam huko anakoishi. Labda CCM wamweke mtu anayefahamu Karatu na ana mapenzi kwa Karatu
Dr Lori ni mkazi na mwenyeji Wa wilaya ya Karatu,kata ya Rotya,kijiji cha Kaynam-Rotya,kitongoji cha kaynam- kusini. Ni kweli amejenga Dar,maeneeo ya Changanyikeni,Kama watanzania wengine. Hali halisi ni kuwa CDM karatu siyo shwari kabisa. Wanauliza kwa nini waambiwe asiyetaka yanayoendelea aondoke? CDM wamefanya operesheni nyingi kufikisha elimu kwa umma,lakini kipindi hiki badala ya kuelimishwa,wanakemewa Kama watoto. Chama kimekuwa mali ya Mbowe.
CCM watalichukua jimbo wakichanga karata zao vizuri.
 
N​goja aje apambane na mzigo mzito wa Dr W. Peter Slaa ndo atajua maumivu ya kushindwa.
Dr Slaa Yuko re-treat baada kuambiwa haya ni mafuriko,Kama huwezi kuogelea chapa lapa.
 
Yego, Chikaka Sumuni, na wewe ni mwana Karatu?.
 
Last edited by a moderator:
Ni kweli kwa haya yanayoendelea sasa, Mbowe anataka kuonesha kuwa Chadema ni mali yake, lakini siyo, ndiyo maana nasema muda uliopo ni mdogo, wabunge wapewe kura, baada ya hapo tutaona cha kufanya. Lorry hapati kura za kutosha Karatu, kwani hata hiyo kijiji chake uliyotaja ya Rhotia-Kainam, na kata uliyotaja ya Rhotia anaonekana tu wakati huu wa uchaguzi. Kujenga nyumba Dar sio ishu, ila yeye anakaa huko Dar, kwanini asibahatishe kugombea huko?
Afai kuwa mbunge wa kuchaguliwa labda wa kuteuliwa asubiri baada ya uchaguzi.
 
Dopas CDM wameanza kutofautiana wenyewe kutokana na matokeo ya kura za maoni. Bwana Lazaro hakuridhika na mchakato ulivyoenda. CCM itashinda safari hii. Tusubiri,October imeshafika.
 
Last edited by a moderator:
Karatu,Arusha Manispaa lazima yarudi ccm
 

Je ushawahi kujiuliza kwa nn ccm wanang'ang'ania ikulu?
 
Karatu kumekucha. CCM wako kikazi zaidi. CDM hawana chao,wamepoa kabisa. Dr Slaa(GS-CDM) hatajihusisha kumfanyia kampeni mgombea wa CDM. CCM wanakwenda kushinda.
 
karatu hata wakimweka ngombe kwa ajili ya cdm anamshinda Lorry, huyo si ndo yule ambaye hajasubiri matokeo 2010?
 
Tafàdhari jingàlao, acha ujinga, usitumie neno lazima, hakuna ulazima kwenye demokrasia, ccm achane kutumia neno hili maana linaleta tafasiri ya kutoweka kwa amani ka kulazimisha ushi iwapo mtashindwa, stop this plse



Karatu,Arusha Manispaa lazima yarudi ccm
 
Last edited by a moderator:
Ccm karatu kurudi ni kama ndoto za mchana.

Karatu mgombea makini wa cdm.
Ndugu. Willy qulwi qambalo.


Karatu ccm haiwezi rudi.
Ukiangalia.serikali za.mitaa.hakuna sehemu ccm wameshinda labda mbulu mbulu tu.

Subiri na tuone
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…