Obama Ameshasahau Yaliyotokea Kenya 2008, au anataka tu kuweka historia.

Stroke

JF-Expert Member
Feb 17, 2012
34,679
40,931
Rais wa Marekani Barak Hussein Obama, anatarajia kuzuru kenya mnamo mwezi july mwaka huu.

Ziara yake inakuja mara baada ya kusubiri Muda mrefu sana, kutokana na pingamizi mbali mbali za ndani na nje ya nchi yake.

Mapingamizi hayo yanatokana na uwepo wa mashtaka ya kijinai katika mahakama ya kimataifa ya kijinai kwa viongozi wakuu wawili wa Kenya.

Mashtaka hayo ni matokeo ya makubaliano Baina ya Rais Mwai Kibaki na Raila Odinga , kuunda tume itakayofanya uchunguzi wa kuvumbua wahusika wakuu wa vurugu zilizotokea baada ya uchaguzi mnamo mwaka 2007-2008.

Baada ya makubaliano hayo Jaji Waki alitoa ripoti yenye list ya majina ya watu waliohusika katika vurugu hizo, lakini mpaka sasa waliofikishwa mahakamani ni sita tu, ikiwemo viongozi hao wakuu wa nchi. Kumekua na maombi mbali mbali yakitaka serikali ya kenya kutoa majina yote ya wahusika yaliyomo kwenye ripoti ya waki jambo ambali halikufanyika mpaka sasa.

Baada ya wahusika kufikishwa mahakamani, Rais Obama alikua na haya ya kusema, nanukuu;

I urge all of Kenya's leaders, and the people whom they serve, to cooperate fully with the ICC investigation and remain focused on implementation of the reform agenda and the future of your nation. Those found responsible will be held accountable for their crimes as individuals. No community should be singled out for shame or held collectively responsible. Let the accused carry their own burdens – and let us keep in mind that under the ICC process they are innocent until proven guilty. As you move forward, Kenyans can count on the United States as a friend and partner.

—Barack Hussein Obama.

ingawa wahusika wakuu waliofikishwa mahakamani wamefutiwa mashtaka yao, lakini bado kuna kumbukumbu mbichi kwa wahanga wa vurugu hizo zilizosababisha watu zaidi ya 1,200 kupoteza maisha na wengine 500,000 kuyakimbia makazi yao.

Ziara ya Kiongozi mkuu wa Taifa lenye sifa ya kipekee ya kidemokrasia kwa taifa ambalo bado linaongozwa na waliokua wakituhumiwa katika vurugu zilizosababisha upotevu wa mali na maisha ni kama dharau kwa wale waliofikwa na majanga hayo.

Naona kama vile Rais Obama anataka kuweka historia binafsi zaidi ya kusimamia misingi iliyolijenga Taifa la Marekani na kulifanya kuwa kuu, kwa kuheshimu utu na uhai wa binadamu.

Kama Rais Obama anataka kubakiza heshima yake na ya taifa lake, basi ni wakati mzuri kwake kusitisha ziara yake hiyo na kusubiri mpaka atoke ikulu, na kwenda kuzuru Nchi ya Baba Yake. Hata kama akifanya hivyo bado katika historia iatabaki kua Marekani ilishawahi kupata kiongozi mwenye asili ya Kenya.

OBAMA LINDA HESHIMA YAKO NA YA TAIFA LAKO KWA KUSITISHA ZIARA YAKO KENYA.


 
stroke, I think the US operates under the principle one is innocent until proven otherwise.
No court of law has thus far proven beyond reasonable doubt that mr. Uhuru Kenyatta or W. Ruto are indeed guilty of the crimes they are accused of.
The ICC is yet to determine all that.

Let the legal process take its course.
 
Last edited by a moderator:
stroke, I think the US operates under the principle one is innocent until proven otherwise.
No court of law has thus far proven beyond reasonable doubt that mr. Uhuru Kenyatta or W. Ruto are indeed guilty of the crimes they are accused of.
The ICC is yet to determine all that.

Let the legal process take its course.
huoni kwamba marekani kama kaka mkuu wa dunia atakua amekiuka misingi yake ya utu na heshima kwa binadamu, simply kwa ziara ya kiongozi wao, ambayo inaonekana kutaka kufuta yaliyotokea Kenya, ndugu, wamekufa watu 1,200 hiyo sio kitu kwa marekani kwakua ni rafiki na patna wa Kenya, kwahiyo urafiki na upatna huo haujali utu na uhai wa binadamu?? kwanini Obama kama mtetezi mkuu wa haki za wanyonge kama anavyofahamika, hakufanya ziara Nchi kama Zimbabwe ambapo ndipo kumebakia kiongozi wa kihistoria wa afrika, au kwakua mataifa ya magharibi hayataki kuwa karibu na Mugabe ambaye aliwapa wananchi wake ardhi kutoka kwa wazungu waliokua wamejimilikisha ardhi kubwa, kinachoonekana hapa ni double standard na nia ya kutaka tu kuweka historia binafsi kwa Obama. Ziara hiyo haina manufaa kwa watetea haki za wale waliofiwa na ndugu zao kwenye hayo machafuko. Ni aibu kwa taifa la marekani.
 
stroke, I think the US operates under the principle one is innocent until proven otherwise.
No court of law has thus far proven beyond reasonable doubt that mr. Uhuru Kenyatta or W. Ruto are indeed guilty of the crimes they are accused of.
The ICC is yet to determine all that.

Let the legal process take its course.
[h=2]'Widespread disappointment'[/h]Human Rights Watch, which has accused the Kenyan government of acting as a roadblock, said: "It's clear that a long tradition of impunity in Kenya and pressure on witnesses have been serious obstacles to a fair process before the ICC."
Fergal Gaynor, a lawyer who represents victims of the violence, told the BBC's Focus on Africa programme that there was a "widespread feeling of disappointment" at the dropping of charges.


About 1,200 people were killed in the violence in 2007-8 and 600,000 were displaced.
Mr Ruto is on trial at the ICC on similar charges to Mr Kenyatta, after his legal team's efforts to have the case thrown out failed.


He and Mr Kenyatta were on opposing sides during the 2007 election, with Mr Ruto accused of fuelling violence to bolster opposition leader Raila Odinga's chances of becoming president. He denies the charges.


Mr Ruto subsequently formed an alliance with Mr Kenyatta in the 2013 election, opening the way for him to become deputy president.
 
huoni kwamba marekani kama kaka mkuu wa dunia atakua amekiuka misingi yake ya utu na heshima kwa binadamu, simply kwa ziara ya kiongozi wao, ambayo inaonekana kutaka kufuta yaliyotokea Kenya, ndugu, wamekufa watu 1,200 hiyo sio kitu kwa marekani kwakua ni rafiki na patna wa Kenya, kwahiyo urafiki na upatna huo haujali utu na uhai wa binadamu?? kwanini Obama kama mtetezi mkuu wa haki za wanyonge kama anavyofahamika, hakufanya ziara Nchi kama Zimbabwe ambapo ndipo kumebakia kiongozi wa kihistoria wa afrika, au kwakua mataifa ya magharibi hayataki kuwa karibu na Mugabe ambaye aliwapa wananchi wake ardhi kutoka kwa wazungu waliokua wamejimilikisha ardhi kubwa, kinachoonekana hapa ni double standard na nia ya kutaka tu kuweka historia binafsi kwa Obama. Ziara hiyo haina manufaa kwa watetea haki za wale waliofiwa na ndugu zao kwenye hayo machafuko. Ni aibu kwa taifa la marekani.

Robert Mugabe mtetezi wa haki ya kibanadamu? Ama kweli!
 
Haijadhibitishwa iwapo kweli rais na makamu wake walihusika kwa mauaji ya watu 1200.
Wangekanwa na Amerika nchi za magharibi iwapo wangekataa kushirikiana na korti ya ICC, lakini despite ya vyeo vyao walifika mbele ya mahakama hiyo. Sababu ya rais El Bashir kuwa isolated si ati kwasababu amekuwa proven guilty, bali amekataa kuti amri ya mahakama ya ICC walivyofanya akina Uhuru.

Wawili hawa bado hawana hatia hadi the justice machineries zidhibitishe hayo na kutoa hukumu yao.
 
Back
Top Bottom