jojipoji koromije
JF-Expert Member
- Mar 22, 2017
- 991
- 1,412
Nipo hapa makumbusho anapiga show na band yake ya Bogos Musica!! Kuna wazungu wamejaa hapo mbele then anawapongeza wazungu kwa kucheza mziki wake then anasema “nyie waswahili mmekaa tu hata hamchezi wakati wazungu wanacheza, ngoja tuwapigie nyimbo zenu waswahili!!”
Huyu jamaa nahisi kashiba na kuvimbiwa uhuru wa kufanya mziki Bongo!! Huyu kasahau kabisa wakati yuko na FM Academia jinsi watu walivyokuwa wakijaa na kucheza mziki wa FM academia tena yeye akiwa Kiongozi!
Anashindwa kujua hajafikia levels za FM academia na kuishia kututukana sisi “Wachache” tuliojitokeza kuona ana jipya gani!!? Tena kwa gharama zetu!
Tuna Choma mafuta muda ! Mamaae! Kwa matusi haya nathibitisha sitohudhuria show yake labda aombe msamaha. Kama vp aende Ulaya akapige mziki wazungu watahudhuria kila siku.
Kaongea utumbo sana leo!! Tunamheshimu sana ila kwa dharau hizi basi Mamlaka imruhusu akajaribu maisha Kinshasa!! Si ndo nyumbani kwao!! Eeh!!basi aende.