katoto kazuri
JF-Expert Member
- Feb 10, 2018
- 6,126
- 5,756
Binti mmoja mwanafunzi wa chuo akiwa ndani ya
pantoni akivuka kutoka Magogoni kuelekea
upande wa Kigamboni alimuona mwanaume
Handsome akiwa ndani ya gari yake nzuri.
Bila wasiwasi yule binti akamfuata mwanaume
yule na Kumwambia; "Hey awww you look
handsome...i like you"
Yule mwanaume akiwa na wasiwasi fulani
akashusha kioo cha gari kidogo kumwambia yule
binti; "Mdogo wangu, mapenzi siyo kitu kizuri
kwako kwa wakati huu, nakuona umetoka chuo
bila shaka, wewe bado ni msichana mdogo kuwa
na tabia kama hii.
Tafadhali sana nenda nyumbani au sijui Hosteli
na usome kwa bidii, wachana na mapenzi soma
ili uje ufanikiwe katika maisha."
Baada ya kusema hayo, Yule mwanaume akatoa
note book yake na kuanza kuandika huku
akisema; "Nakuandikia hapa baadhi ya maneno
ya busara na muongozo katika maisha yako.
Hutakiwi kuwa cheap kiasi hiki mdogo wangu.
Nakuomba sana ukasome haya kabla ya kulala"
Akampa ile karatasi na kufunga kioo cha gari
mpaka juu. Yule msichana alirudi Hosteli kwa
aibu kubwa na usiku kabla ya kulala akafungua
ile karatasi ili aisome.
Karatasi ilisomeka hivi;
"Wewe kipofu nini? Humuoni Mke wangu yupo
kwenye kiti cha abiria amekilaza amelala? Hii ni
namba yangu nipigie muda wowote isipokuwa
asubuhi sana na usiku. Hata hivyo na mimi
nimekupenda sana. Bila shaka hautaniangusha."
WANAUME NA AKILI ZAO ZA MWENDOKASI 😂😂😂😂😂
pantoni akivuka kutoka Magogoni kuelekea
upande wa Kigamboni alimuona mwanaume
Handsome akiwa ndani ya gari yake nzuri.
Bila wasiwasi yule binti akamfuata mwanaume
yule na Kumwambia; "Hey awww you look
handsome...i like you"
Yule mwanaume akiwa na wasiwasi fulani
akashusha kioo cha gari kidogo kumwambia yule
binti; "Mdogo wangu, mapenzi siyo kitu kizuri
kwako kwa wakati huu, nakuona umetoka chuo
bila shaka, wewe bado ni msichana mdogo kuwa
na tabia kama hii.
Tafadhali sana nenda nyumbani au sijui Hosteli
na usome kwa bidii, wachana na mapenzi soma
ili uje ufanikiwe katika maisha."
Baada ya kusema hayo, Yule mwanaume akatoa
note book yake na kuanza kuandika huku
akisema; "Nakuandikia hapa baadhi ya maneno
ya busara na muongozo katika maisha yako.
Hutakiwi kuwa cheap kiasi hiki mdogo wangu.
Nakuomba sana ukasome haya kabla ya kulala"
Akampa ile karatasi na kufunga kioo cha gari
mpaka juu. Yule msichana alirudi Hosteli kwa
aibu kubwa na usiku kabla ya kulala akafungua
ile karatasi ili aisome.
Karatasi ilisomeka hivi;
"Wewe kipofu nini? Humuoni Mke wangu yupo
kwenye kiti cha abiria amekilaza amelala? Hii ni
namba yangu nipigie muda wowote isipokuwa
asubuhi sana na usiku. Hata hivyo na mimi
nimekupenda sana. Bila shaka hautaniangusha."
WANAUME NA AKILI ZAO ZA MWENDOKASI 😂😂😂😂😂
