mtahengerwa
JF-Expert Member
- Jun 28, 2011
- 384
- 173
Mwl nyerere aliyeipenda nchi yake Tanzania na watu wake aliipenda upeo.Mwl alikuwa mzalendo wa hali ya juu, uzalendo wake ulijidhilisha katika maisha halisi aliyoishi kiasi kwamba hata alipopewa zawadi binafsi alizileta kwa watanzania.
Mwl Nyerere alikuwa mwadilifu sana kiasi kwamba wakati alipong'atuka hakuwa na nyumba ya kuishi kijijini kwake mpaka serikali wakaona aibu wakaamua kumjengea.Mwl Nyerere hakujua kujilimbikizia mwenyewe bali alipenda kuwalimbikizia watanzania.
Mwl Nyerere alikuwa mchapa kazi.Muda wake mwingi aliutumia kuwahangaikia watanzania.Lakini moyo huo haupo kwa viongozi wetu sasa ambao hutumia rasilimali za nchi kwa manufaa yao na familia zao.
Mwl Nyerere aliichukia rushwa na kusema rushwa ni adui wa haki sitatoa wala kupokea rushwa.Viongozi wetu wamekuwa wanafiki majukwaani wanakemea rushwa maofisini wanakuwa wa kwanza kuomba rushwa.Mwl Nyerere alichukia sana viongozi wanaotumia rushwa kununua uongozi, Leo hii tumeshudia na tunaendelea kushudia viongozi wanaousaka urais wanatumia fedha nyingi kuwanunua wajumbe watakaowapendekeza kwa kuwapigia kura.
Mwl Nyerere aliweka na kuheshimu miiko ya uongozi na kusema uongozi ni dhamana lazima uwaheshimu na kuwatumikia wananchi waliokupa madaraka hayo.Mwl Nyerere alisema ukiwa kiongozi ni wewe tu na wala sio familia yako (mke wako na watoto wako) hao sio viongozi lakini wanatakiwa waishi kwa kuheshimu miiko ya uongozi.
Baada ya Mwl Nyerere kufariki viongozi wetu walioishi maisha ya kinafiki enzi za Nyerere waligeuka kuwa manyang'au na kuanza kutapanya na mambo mazuri aliyoyaweka Mwl Nyerere kwa faida ya watanzania.
WASSIRA pekee ndiye aliyebaki kuwa kielelezo cha maisha halisi aliyoishi Mwl Nyerere na kuyaamini kati ya viongozi tulionao.WASSIRA ni mwadilifu, mchapa kazi, mzalendo na ni viongozi anayeheshimu miiko ya uongozi.
WASSIRA ndio anayefaa kuwa rais ajaye baada ya kikwete kwa sababu nilizozitaja hapo juu na amekuwa kiongo mkubwa sana katika uongozi wa kikwete katika mambo mbalimbali.Hii inatokana na sifa kubwa aliyonayo ya kujiamini na uwezo mkubwa wa kupambanua mambo mbalimbali akaeleweka.
Ndo maana nasema bado tunaye Nyerere anayeishi kwa WASSIRA tumuungo mkono wassira katika mbio zake za urais arudishe hesima ya taifa hii ambayo inaenda kuwa historia na kuwekwa mwenye makumbusho ya taifa.
Mwl Nyerere alikuwa mwadilifu sana kiasi kwamba wakati alipong'atuka hakuwa na nyumba ya kuishi kijijini kwake mpaka serikali wakaona aibu wakaamua kumjengea.Mwl Nyerere hakujua kujilimbikizia mwenyewe bali alipenda kuwalimbikizia watanzania.
Mwl Nyerere alikuwa mchapa kazi.Muda wake mwingi aliutumia kuwahangaikia watanzania.Lakini moyo huo haupo kwa viongozi wetu sasa ambao hutumia rasilimali za nchi kwa manufaa yao na familia zao.
Mwl Nyerere aliichukia rushwa na kusema rushwa ni adui wa haki sitatoa wala kupokea rushwa.Viongozi wetu wamekuwa wanafiki majukwaani wanakemea rushwa maofisini wanakuwa wa kwanza kuomba rushwa.Mwl Nyerere alichukia sana viongozi wanaotumia rushwa kununua uongozi, Leo hii tumeshudia na tunaendelea kushudia viongozi wanaousaka urais wanatumia fedha nyingi kuwanunua wajumbe watakaowapendekeza kwa kuwapigia kura.
Mwl Nyerere aliweka na kuheshimu miiko ya uongozi na kusema uongozi ni dhamana lazima uwaheshimu na kuwatumikia wananchi waliokupa madaraka hayo.Mwl Nyerere alisema ukiwa kiongozi ni wewe tu na wala sio familia yako (mke wako na watoto wako) hao sio viongozi lakini wanatakiwa waishi kwa kuheshimu miiko ya uongozi.
Baada ya Mwl Nyerere kufariki viongozi wetu walioishi maisha ya kinafiki enzi za Nyerere waligeuka kuwa manyang'au na kuanza kutapanya na mambo mazuri aliyoyaweka Mwl Nyerere kwa faida ya watanzania.
WASSIRA pekee ndiye aliyebaki kuwa kielelezo cha maisha halisi aliyoishi Mwl Nyerere na kuyaamini kati ya viongozi tulionao.WASSIRA ni mwadilifu, mchapa kazi, mzalendo na ni viongozi anayeheshimu miiko ya uongozi.
WASSIRA ndio anayefaa kuwa rais ajaye baada ya kikwete kwa sababu nilizozitaja hapo juu na amekuwa kiongo mkubwa sana katika uongozi wa kikwete katika mambo mbalimbali.Hii inatokana na sifa kubwa aliyonayo ya kujiamini na uwezo mkubwa wa kupambanua mambo mbalimbali akaeleweka.
Ndo maana nasema bado tunaye Nyerere anayeishi kwa WASSIRA tumuungo mkono wassira katika mbio zake za urais arudishe hesima ya taifa hii ambayo inaenda kuwa historia na kuwekwa mwenye makumbusho ya taifa.