Nusu shilingi ya VODACOM

samirnasri

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
1,388
213
Miezi ya mwishoni mwa mwaka 2010 kampuni ya simu za mkoni ya vodacom ilianzisha huduma ya kupiga simu voda kwenda voda kwa nusu shilingi kwa sekunde katika mikoa ya Dsm, Morogoro na mikoa mingine ya jirani.

Siku za hivi karibuni makato hayo yamekuwa tofauti. Kwa mfano leo niliweka vocha ya sh. 500 nikiwa Dsm na kumpigia mteja mwingine wa vodacon.

Kilichonishangaza ni vocha hiyo kumalizika ndani ya dakika nne. Nililazimika kupiga simu huduma kwa wateja ili kujua kama huduma ya nusu shilingi kwa mkoa wa Dsm na mikoa jirani bado inaendelea au imesitishwa.

Muhudumu alinihakikishia kwamba huduma hiyo bado ipo isipokuwa katika mikoa mingine ndo wanapiga voda- voda kwa sh moja na nusu pamoja na VAT.

Nilipomuuliza kulikoni sh. 500 ikaisha ndani ya dakika nne aliniambia nimpigie baada ya masaa mawili atakuwa ameniangalizia nini tatizo. Kwa kuwa ilikuwa sa sita kasoro dakika 2 usiku nilishindwa kuvumilia hadi sa nane usiku. Nawaomba vodacom watuweke wazi kama nusu shilingi bado ipo au wameshaiondoa..
 
Customercare ya Vodacom iko hovyo kuliko Customer care ya mtandao wowote nchini. Wanapokea simu hovyo na hawakuattend ipasavyo. Nimeshaachana na voda mimi
 
hawa jamaa hawakujipanga kuingia ktk mfumo huu mpya, wanaburuzwa sana
na tigo. halafu hiyo ya sh moja na sent fifty pamoja na vat vipi? ina maana vat
ni 50%? waweke wazi scale zao
 
Kwa kweli Voda wamechoka, na huduma zao nyingi zipo kwenye matangazo tu, hazipo kiuhakika katika matumizi, na wanatuumiza sana wateja wao. Embu huo utawala mpya ujipange upya la sivyo hali itakuwa tete siku sio nyingi.
 
Welcome to Tanzania! ki-nchi kinachoendeshwa ilimradi kimeenda! kero kibao, shida millioni!
 
Hili tatizo hata Airtel nmeliona kwa mara ya kwanza jana. Niliweka sh 1000 jioni, cha kushangaza niliongea na mtu wa airtel kama sio dk 6 basi ni 7, cm ikanipigia alarm ya hela kumalizika, nlipojaribu kuangalia salio et imebaki sh 5, mpaka sa hz sijaelewa nini kilitokea, wanabadilisha ofa zao kimya, kimya bila kututaarifu wateja, sio vizuri, mbona wakianza kutoa hizo ofa zao matangazo kila dk, "ongea sh 1 kwa sekunde masaa 24". Wajirekebishe wanatukera wateja.
Miezi ya mwishoni mwa mwaka 2010 kampuni ya simu za mkoni ya vodacom ilianzisha huduma ya kupiga simu voda kwenda voda kwa nusu shilingi kwa sekunde katika mikoa ya Dsm, Morogoro na mikoa mingine ya jirani.

Siku za hivi karibuni makato hayo yamekuwa tofauti. Kwa mfano leo niliweka vocha ya sh. 500 nikiwa Dsm na kumpigia mteja mwingine wa vodacon.

Kilichonishangaza ni vocha hiyo kumalizika ndani ya dakika nne. Nililazimika kupiga simu huduma kwa wateja ili kujua kama huduma ya nusu shilingi kwa mkoa wa Dsm na mikoa jirani bado inaendelea au imesitishwa.

Muhudumu alinihakikishia kwamba huduma hiyo bado ipo isipokuwa katika mikoa mingine ndo wanapiga voda- voda kwa sh moja na nusu pamoja na VAT.

Nilipomuuliza kulikoni sh. 500 ikaisha ndani ya dakika nne aliniambia nimpigie baada ya masaa mawili atakuwa ameniangalizia nini tatizo. Kwa kuwa ilikuwa sa sita kasoro dakika 2 usiku nilishindwa kuvumilia hadi sa nane usiku. Nawaomba vodacom watuweke wazi kama nusu shilingi bado ipo au wameshaiondoa..
 
Kwa kweli Voda wamechoka, na huduma zao nyingi zipo kwenye matangazo tu, hazipo kiuhakika katika matumizi, na wanatuumiza sana wateja wao. Embu huo utawala mpya ujipange upya la sivyo hali itakuwa tete siku sio nyingi.

hawa vodacom wana matatizo,ni kuwahama tuu....ukija kwenye internet ndio wezi wa kutupwa, eti 50mb ni sh 2000 wakati wenzao airtel 400mb ni 2500, wizi mtupu
 
Back
Top Bottom