NUCLEAR WEAPONS

Inawezekana mzee ni noma kwa nuclear kwa vitendo ndo maana analindwa na UN ili asifundishe hii kitu kwa wengine.

Mwingine alikuwa marehemu Pius Mwandu(R.I.P)

Mtaalam Pius Ngw'andu alikuwa ni mtaalam wa Biology na sio Physics na alistaafia Australia Kama sikosei.
 
Yani kwa kifupi ni kwamba urusi ukiachana nyukilia anauwezo gani mwingine wa kupigana vita.
 
Nipokuwa Advance kuna mwalim wa physics nilimuulisa swal rahisi tu, ovious nilkuwa simkubali na alijua ilo maana my favouright teacha wangu walimfukuza (mr Busanji, best teacher)

Swal lilikuwa ni la gravitation na sikutegemea angeshindwa kunielewa
β€œ nilimuuliza, ivi police wakipiga risasi juu hewani af uneglect air resistance maana yake itarudi chini na kufika point ile kwa speed iliyotoka nayo. Sa kwann bado mapolice wanapiga risasi juu

Sa usitegemee walim kama hao wakakufundisha ukaelewa in details
 

Huwezi kuwa msomi af unashindwa kuelezea hizo terminologies kwa lugha ya kinyumbani, hii inaonesha hujaelewa umekalili tu
 
Yani kwa kifupi ni kwamba urusi ukiachana nyukilia anauwezo gani mwingine wa kupigana vita.
Muulize Zelensky pia Muulize yule babu anaepungia hewa na kusalimia upepo kilichomkuta kule vietcong alipokamatwa mateka na kukabidhiwa kwa Putin ili asifurukute na hakufurukuta for 2 years chini ya Putin na kwanini akabidhiwe kwa putin na akati babu alikuwa na cheo na ujuzi kuliko Putin? Jibu ni uwezo wa kupigana wa Putin ndiyo aliweza kumdhibiti Putin.
 
Hayo madude kama yana madhara kiasi hicho ni kwann wanayamiliki? Na ata hawayatumii, hiv kweli hayo madude yana exist?
 
Huwezi kuwa msomi af unashindwa kuelezea hizo terminologies kwa lugha ya kinyumbani, hii inaonesha hujaelewa umekalili tu
Wewe unaeelewa kiswahili mtafsirie bibi yako wa kule nyangao hizi sentesi zifuatazo:
1. Dehydrohallogenation of alkyl hallide under limainshubula de mupuantee
2. Restricteda rumbwegesiensis
3. Decarboxylation of ribulose biphosphate under unbwimbwilized sacharomycetes
 
Hayo madude kama yana madhara kiasi hicho ni kwann wanayamiliki? Na ata hawayatumii, hiv kweli hayo madude yana exist?

Wakisema kuyapunguza Urusi anakataa maana ndo kinampa ubabe, akisema ayapunguze uku hana uwezo na vifaa kama vya magaribi ni ujinga
 
Tatizo lako unakalili article unaileta tu apa,
Elezea kwa bby uelewa kama msomi na si kuchukua article ambayo mtu kaelezea kwa maono yake
Ata nipokuwa shule nilkuwa spend walim wanaokalili na ukipindisha article kidogo tu anachanganyikiwa
... hizi elimu zetu za kukariri kwingi hazitufikishi popote kwa kweli.
 
... kwani hiyo ni fani yake? Ni jukumu lako mwenye fani kuelezea kwa lugha ya kueleweka na sio suala la mwingine kutafsiri. Kupenda kuongea kwa misamiati (jargons) ya kitaalamu kwa wasio wataalamu wa fani husika ni dalili za kukariri.
 
... kwani hiyo ni fani yake? Ni jukumu lako mwenye fani kuelezea kwa lugha ya kueleweka na sio suala la mwingine kutafsiri. Kupenda kuongea kwa misamiati (jargons) ya kitaalamu kwa wasio wataalamu wa fani husika ni dalili za kukariri.
Ukiona hivyo bado lugha yetu ni nyembamba kutafsiri baadhi ya hizo technical jargons other utayakuta hayo ma jargon yakibandikwa kama yalivyo hapo utaona uchachu wa elimu eg dihaidrohalojenesheni ovu alikaili halaidi
 
Nuclear physics ni somo linalo husiana na mwingiliano wa nucleus za atom.

Katikati ya kila atom kuna nucleas. Nucleas ndani yake kuna proton(+) na nyutron. Zimegandana pamoja kwa nguvu/nishati kubwa.

Kutoka katika chemistry:
Kuunganisha maada kunahitaji nishati (nuclear fusion) na kutenganisha maada kunahitaji nishati pia (nuclear fusion). What happens there is incridibly complicated.

Ukiweza kuzitenganisha protons na neutron kivyake (fission) kutoka nucleas basi utapata nishati na ndiyo mwanzo wa bomu la nuclear (atomic bomb) na uzalishaji wa umeme. Vilevile ukiweza kuziunganisha nuclear(fusion) utapata nishati ZAIDI ya fission(atomic bomb) ambayo inaunda hydrogen bomb(thermonuclear bomb)

Bomu linalotokana na njia ya fission ni atomic bomb mfano yaliyo tumika japana.

Na bomu linalotokana na fusion ni hydrogen bomb (thermonuclear bomb).

Katika elements za chemistry kuna stable na unatable elements. Yaani elements ambazo nucleas yake inaweza kuvunjwa na elements ambayo nucleas yake haivunjiki kirahisi(very laymanly). Katika hizo hapana shaka nafikiri kuanzia element ya 82 au zaidi na kuendelea ni unstable elements/nuclei.

Uranium na Plutonium at least processes zake zinawezekana including availability and very unstable. Plutonium anaweza kupatikana kutoka uranium pia.

Process ya kuchimba uranium kutoka chini ya maji au mazingira hadimu, kuisafisha na kuanza kuihuisha(enrichment) kufikia kiwango cha kuweza kutumika kutengeneza nucleae energy ni gharama zaidi ya bajeti za nchi. Nchi tajiri zimeweza.

Kwa uranium iliyotayari ili kupata nishati ya nuclear inabidi utenganishe protons na neutrons. Kutenganisha hizi particles kunahitaji nishati nyingine kubwa sana sawa au zaidi ya nguvu (binding energy iliyozishika).

Kuna aina mbili za nuclear bombs
1. Atomic bomb(from fission peocess)
2. Hydrogen bomb/thermonuclear (from fusion process).

Kutenganisha protons na neutrons kutoka nucleas ya uranium unahitaji neutron nyingine. Hii neutron nyingine inazalishwa kutoka katika neutron generator ama particle accelerator machine. Neutron generator ni particle accelerator inayotumia voltage 100,000V mpaka 500,000V ku toa power supply katika neutron tube ambayo inazisafirisha isotope za hydeogen mbili zinatembea karibia na speed ya mwanga zinagongana na kuzalisha neutron na helium gas au ion.

Hii neutron iliyozalishwa inatembea na speed kubwa karibia na mwanga kwenda kwenye uranium material/nucleas na kusambalatisha protons na neutrons ambazo zinaachia nishati kubwa (E =mC^2) inayotoa sauti ya blast, mwanga na inayowaka inachoma hewa iliyopo karibu kusababisha joto kali linalochoma kilakitu karibu na kusambaa ukubwa wa tufe kwenda angani na kilometer kadhaa ardhini. Hiyo ni Atomic bomb yenye gramm kadhaa za uranium.

neutrons zilizosambaratishwa nazo zinaenda kufumua nucleas ya uranium nyingine na kusababisha energy nyingine hii tunaita chain reaction. Baada ya sekunde kadhaa uranium yote inatumia huku kilomita za vijiji zimeliwa.


Hyrogen bomb(thermonuclear bomb)
Hili ni nuclear bomb linalotumia nuclear fusion (nishati inatoka baada ya kuunganisha nucleas nyepesi nyingi)

Hydrogen bomb ya tani kadhaa inanguvu zaidi ya milion tani kadhaa za atomic bomb(aina ya yaliyotumika nagasaki na hiroshima).

Hydrogen bomb ina atomic bomb kama fuel ndani yake.

Neutron generator inatoa neutron zinazovunja nucleas za uranium ambapo fission ya hapa inatoa nishati na mlipuko wa bomu la atomic. Huu mlipuko wakati unaendelea kumaliza vijiji unachoma gesi ya hyrogen iliyopo mwanzo wa nuclear warhead. Hydrogen fuel ina gandamiza uranium material iliyopo chemba nyingine kwenye bomu moja. Mgandamizo(compression kama engine principle) unasababisha joto na pressure kupanda. Joto na pressure vinasababisha nucleas za uranium kuungana (fusion) na baadae kupasuka na protons na neutrons kusambaratika ambapo inatoa nishati kubwa yapili. Neutrons zilizotoka zinasababisha chain reaction ya tatu. Kwahiyo nuclear bomb ni fission(atomic bomb) + fusion+ chain reaction.

Kilo kadhaa za hydrogen bomb zina obliterate mji.

Nafikiri umepata maelezo mafupi ya kinachotokeaga.
 
Okey watery
 
... hivi kuna physics ya Tanzania inaweza kujibu hayo maswali kweli? Sidhani. By the way, akili inanituma kwamba physics wanazotuletea huku ni fake, watakuwa na physics zao sio kwa madude hayo wanayo-develop!
Hapa umemaliza kiongozi 🀣🀣🀣
Hii physics ya matumizi ya pendulum hapa tutadanganyana tu πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Hapo umetafsiri moja kwa moja hujaeleza na ndio utofauti unapo anzia wa wasomi wetu. Anaweza kutafsiri aliyoyameza kwa kizungu ila kuyafafanua kwa lugha rahisi hawezi.. Kuyaweka katika uhalisia pia hawezi. Unapo shimdwa kuyafafanua kwa lugha rahisi hata kuyaleta kwenye uhalisia hutaweza pia.
dudus
 
Nuclears zilipigwa sana kimajaribio na kuna footage kibao za test za nuclear, search google na youtube utazipata.
Tangu mwaka 1945 test 2,476 zimefanyika za nuclear kwa chini ya ardhi, majini na angani.

Hiroshima na nagasaki zilikuwa ya kwanza kutumika kwa binadamu kama silaha.
 
ntaleta maelezo rahisi ndugu yangu usjal, nakosa nafasi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…