NSSF yaelekea kufilisika

Ngongo

Platinum Member
Joined
Sep 20, 2008
Posts
21,183
Reaction score
37,492
Wanajamvi heshima mbele,

NSSF imeanza zoezi la kuwabembeleza/kulazimisha wateja wake wakubwa [waajiri] kutoa mchango yao ya kila mwezi kabla ya wakati.Ni kawaida waajiri kupeleka michango ya kila mwezi mmoja nyuma[mfano mshahara wa mwezi tano michango yake inatakiwa ipelekwe mwezi sita],sasa NSSF inawataka waajiri wakubwa [waajiri wenye idadi kubwa ya wafanyakazi] kupeleka michango ya wafanyakazi mwezi mmoja mbele au mwezi huu wa sita ili kukabiliana na hali mbaya ya fedha inayoliandama shirika hilo la wafanyakazi nchini.

Taarifa toka chanzo cha uhakika ndani ya shirika hilo zinadai serekali imechota fedha toka NSSF kwaajili ya kugharamia mishahara ya watumishi wake baada ya chanzo chake muhimu cha mapato TRA kushindwa kupata fedha za kutosha kulipa mishahara ya watumishi wa serekali pamoja na shughuli nyingine muhimu.

Zipo taarifa za uhakika serekali ina mkakati wa kuwalazimisha wanachama wote wa NSSF na mashirika mengine ya hifadhi ya jamii kutokulipwa mafao yao hadi wafikishe umri wa kustaafu. Mkakati utasaidia kukabilia na upungufu mkubwa wa fedha unaotarajiwa kutokea kwakuwa fedha zinazochotwa na serekali hazitarajiwi kurejeshwa.

Source: Ngongo - Arusha.

 
Hata mimi nimeisikia hiyo lakini mimi nakuwa na wasiwasi na hii issue kama itafanikiwa, je kama mimi mpango wangu labda ni kufanya kazi miaka mitano halafu naachana na kazi ya kuajiriwa naanza ujasiriamali kwa say labda nimeacha nina miaka 32 kwa hiyo itabidi nisubiri hadi nifike miaka 60 ndo nilipwe hela yangu?
 
Ni kweli NSSF iko taabani lakini sababu ni nyingi moja kubwa ni hili swala la kugharamia uendeshaji wa serekali lingine ni miradi yake mingi haina tija na kujikuta fedha zake nyingi zikipotea bure.Mradi wa ujenzi wa UDOM umechota fedha nyingi wakati hata mkataba haujasainiwa,miradi ya majengo mengi ni kwaajili ya ulaji wa wakubwa.Chama cha wafanyakazi wa sekta mbali mbali yafaa waungane kupinga uonevu wa wafanyakazi unaandaliwa chini ya mwavuli wa kuficha utawala mbovu wa serekali ya CCM.
 
Mkuu Masuke kama sheria itabadilishwa maana yake itabidi usubiri hadi utakapofikisha miaka sitini.Hapo hapo lazima utie akili wastani wa umri wa mtanzania ni chini ya hiyo miaka sitini ?.Jiulize serekali ina mpango gani na wafanyakazi wa nchi hii.

 
Duh siasa za ccm kweli za ajabu, juzi kwenye mkutano wao kule jangwani wanasema Daraja litaanza kujengwa mwaka huu na NSSF ndo wamepewa hio kazi ya kutoa nusu ya gharama za mradi, kule Kiwira wanatakiwa wazalishe umeme 200 megawatt, kuondoa Mgao wa umeme na NSSF walipewa kazi hio, sijui UDOM kama NSSF wamemaliza kujenga na majengo yanavuja! Kweli ccm ni DHAIFU, "JJ Mnyika Ukweli ni Uhuru"
 
Na Mkurugezi si walimsifu sana wenzetu na wakasema anatungiwa sheria ili atoke, Duh! hii ni aibu, na Udhaifu mkubwa sana, Linamfia na utetezi wake wa kibaguzi
 
ikifikia serikali ikaanza kutumia fedha za wafanyakazi kwa miradi yake na mishahara Ngongo unategemea NSSF ittacha kufilisika ,halafu TUCTA wamekaa wakichekacheka nao makubwa
 
Ni wezi wakubwa vitega uchumi vyote wanakula pesa mipesa yetu tunaweka haiji na riba wakati wao wanafanyia biashara
Na mbaya zaidi huwezi kupewa pesa hatu mgongo uwe umepinda si adhabu hii!!Basi watoe kariba fulani kwa wateja wao angalau ionekane unajaliwa wao wanajinadi na pesa ya mazishi na wao wafiwe tukawape pesa zakuzikia,na pesa ya mamamjamzito!!wehu kweli na ni majangili siyo majambazi!!
 
Mkuu Froida,

Mkuu wangu hili zoezi lilianza wiki ilipita hapa Arusha maafisa NSSF wamezunguka kampuni zote zenye wafanyakazi zaidi ya 20 na kuendelea.Bahati nzuri maafisa wa NSSF walipokuja ofisini kwangu nilipata wasaa wa kuhojiana nao na wakanieleza ni zoezi la Tanzania nzima ingawa linafanywa kwa siri na kwa uangalifu mkubwa.

Fedha za NSSF ni kama shamba la Bibi hakuna uwazi wa kutosha,hakuna uangalizi wa kutosha,hakuna uadilifu.NSSF ni sehemu ambayo wanasiasa wanachota fedha hovyo kwa faida za kisiasa[miradi ya kisiasa eg daraja la kigamboni & UDom].Wafanyakazi [wadau au ukipenda wanahisa wakuu] hawana mwakilishi halisi ndani ya bodi ya shirika wajumbe wote wa bodi ni wateule wa waziri wa kazi na mwenyekiti ni mteule wa Rais.

Hakika tungewapata wanasiasa aina ya Mch Mtikila au wanasheria mahiri ningefungua kesi mahakama kuu kupinga fedha zangu kuchukuliwa kwa nguvu na kutokuwa na msimamizi mwenye uakilishi wa wafanyakazi.


ikifikia serikali ikaanza kutumia fedha za wafanyakazi kwa miradi yake na mishahara Ngongo unategemea NSSF ittacha kufilisika ,halafu TUCTA wamekaa wakichekacheka nao makubwa
 
Mkuu Masuke kama sheria itabadilishwa maana yake itabidi usubiri hadi utakapofikisha miaka sitini.Hapo hapo lazima utie akili wastani wa umri wa mtanzania ni chini ya hiyo miaka sitini ?.Jiulize serekali ina mpango gani na wafanyakazi wa nchi hii.
Sijui niache kazi kabla hakijanuka maana mwaka huu ni wa mwisho nijiajiri sasa nikisubiri si itakula kwangu.....
 
Yes, absolutely, serikali kuchota fedha is only a tertiary reason for the NSSF books being the red, but primarily the core investment projects are misguided and incompetent.

NSSF imejiingiza kwenye miradi ya kujenga madaraja ya angani, sijui mara wanajenga mall la Wamachinga, mara sijui Chuo Kikuu, jamani, NSSF ina investment and financial expertise gani zaidi ya kukusanya hela za watu na kuwaorodhesha majina kwenye ma kaunta buku?

Kingine, uongozi wa NSSF hauko under pressure ya kutoa results, hakuna anaejali performance ya uongozi, ukishateuliwa wewe ndio CEO wa NSSF basi ndio imetoka, tena huwa wanafanya party, halafu una relax, kazi kutembea kwenye vijiwe vya vilabu vya PAN AFRICA kupiga picha na wachezaji wa zamani, lazima ubweteka!

 
Sijui niache kazi kabla hakijanuka maana mwaka huu ni wa mwisho nijiajiri sasa nikisubiri si itakula kwangu.....

Shemeji hata ukiacha, kwa jinsi utakavyopata usumbufu kufatilia hiyo pesa mpaka utakasirika,nimeteseka kufatilia mafao ya uzazi, nikisikia mtu anaongelea habari za NSSF nasikia vibaya sana.
 
Shemeji hata ukiacha, kwa jinsi utakavyopata usumbufu kufatilia hiyo pesa mpaka utakasirika,nimeteseka kufatilia mafao ya uzazi, nikisikia mtu anaongelea habari za NSSF nasikia vibaya sana.

Shemeji mbona unanitisha hiyo NSSF naitegemea eti baada ya kuacha kazi karibuni sasa kama ni kimbembe kuipata unanifanya nichanganyikiwe na nizidi kuichukia zaidi serikali ya CCM....hivi chama cha wafanyakazi kiko wapi au wamesha katiwa chao..............
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…