Amama Mbabazi
Wiki hii chama tawala nchini Uganda kimemvua ukatibu mkuu Bw Amama Mbabazi kwa kosa la kuanza kampieni za urais kabla ya wakati. Mbabazi mwenye miaka 65 pia ni waziri mkuu wa serikali ya Mseveni anatuhumiwa kumtumia mke wake kuzunguka nchi nzima kumchafua Mseveni na kupigia debe mme wake. Katika mkutano wa wabunge wa chama hicho uliofanyika Ikulu Kololo mjini Kampala kwa kauli moja wamemvua uongozi na hatua za kumvua uanachama zikitarajiwa kufuata.
My take: Kwa upande wa Ccm tuliotangaziwa wamewekwa chini ya uangalizi wa mwaka mmoja wanagombea uenyekiti wa bunge la Katiba! Kama chama kichanga kama Chadema wanachukua hatua kwa kiongozi kama ZZK inauwaje kwa chama kikongwe? Hata NRM ni chama cha juzi tu, maana kmebadilika mwaka 2002 kutoka Vuguvugu la ukombozi yaani chama cha waasi wakati huo hadi kuwa chama cha siasa.