Ngoja nikupe kisa kimoja kilimkuta rafiki yangu mmoja ivi kmpala ug naona km inawezekana huo mkenge ndo uliouingia.
Alinunua cm galaxy s5 kwa ush1050000 cm ikiwa kwenye box na kila kitu chake lkn bei halisi ya iyo simu wakati huo ilikuwa ush1500000 yeye aliona kaokota embe chini ya mlimao,after 3mnth simu ilanza kuzingua kia ajabu ajabu yeye akaichukulia poa ikamsogeza km miezi 6 hivi akaiuza baada kumsumbua sana
Akenda kununua s4 duka hilo hilo km kawaida alifata urahisi wa bei tena alimpeleka na dada yake wakanunu wote s4,baada ya wiki 2 yake ikaibiwa baada ya mwezi ya dada ake ikaanza kuzima zima,mara inashika sana moto wakati wa kuichaji.Tukaipeleka kwa fundi,kuicheki akatuambia hii sio s4 ni s3 tena used inaonekana ilibadilishwa tu mashine kwenye jumba la s4 wajuzi hawashindwi hilo,hatukutilia sana maanani tukaona mafundi nao wezi tu wakati kitu ukikiwasha kinaonesha kabisa Android Samsung s4
Siku kadhaa baada kuzichanga nikampeleka kwenda kununua simu kwenye hayo maduka yake km kawaida anafata mteremko safari hii alitaka kununua samsung A7 au A8 tukaulizia bei ush700000 kwa A7 na 800000kwa A8 tena being ya kwanza b4 negotiations.Kama bahati tukaona ngoja tuendelee kuulizia bei kwingine labda tutapata mteremko zaidi ndipo tulipolivaa duka lililotupa ukweli,kwanza A7 bei ya mwisho wanauza 850000 na A8 bei ya mwisho 1050000 tukashangaa iweje duka liko opposite ulizidi bei zaidi ya laki 2 kwa bidhaa ile ile? Jamaa akajibu nakuuzia cm original,nakupa guarantee miezi 12 tatizo lolote lile lisilosababishwa na wewe rudi duka mlilotoka hawana guarantee na kwa sababu cm wanazouza used wanazifix tu kuja kwenye upya,zingine fake zingine unaweza kuona ni aina fulani kumbe sio ni copy tu
Sasa nafikiri hili ndo janga lililokupata kwa sababu km umenunua simu na ina guarantee usingeyaleta humu hayo matatizo moja kwa moja ila inaonekana hiyo cm umenunua kimteremko ushaona waliokuuzia hawaingiliki kwa sababu hawajakupa hata guarantee,na bei ya note 4 wadau wanaijua apa tuoneshe picha ya risiti tuone bei uliyonunulia labda ni cheap sana kulingana na bei halisia ya kitu au usikute hwajakupa kabisa hata iyo risiti,km hayo yote ndo yaliyopo hamna simu apo mkuu wamekuuzia tekno,unapoamua kununua simu dukani kuwa makini maduka mengine ya masela tu wanauza simu za ujanja ujanja tu