Nyamayao
JF-Expert Member
- Jan 22, 2009
- 6,966
- 2,350
Hii kwangu ilikaa vibaya. Mwanzoni nilidhani masihara mpaka niliposhuhudia makonde na chupa zikirushwa. Kisa? bar maid.
Ni kwamba kuna ka baameid kamoja ka kimbulu kameleta zahma kwenye bar moja mitaa ya kwetu (lazima nikiri ni kazuri, kwakuwa hata mzee mzima nilikuwa napanga kukasarandia). Njemba moja kumbe ndio inakaweka mjini; imekapangia chumba na inakapa fedha za matumizi. Kumbe swahiba wake njemba ambaye anajua uhusiano ule akawa anakaiba kisirisiri. Siri ikafichuka jana, baada ya mabaameidi wenye wivu kumtonya mwenye mali.
Njemba yenye mali, ikapandisha na kushusha presha. Ikamsubiri swahiba wake anayemwibia. Kama masihara vile, njemba mwizi ilipotinga kaunta na kuagiza ka valeur kake ikashangaa inakwidwa kwa nyuma. Wadau kwakuwa tunaujua uswahiba wao, tukadhani masihara mpaka ulipoibuka mtiti wa kufa mtu.
Kibaya zaidi hizi njemba zote zimeoa, na zinaishi maeneo ya jirani. Nadhani mpaka mida hii, habari zitakuwa zimefika kwa wake zao. (Labda na kwa wife wangu pia, huwezi jua. Nasubiria nipigiwe simu kuulizwa kulikoni kwakuwa njemba zenyewe ni washkaji zangu pia.)
Kutandikana kwa sababu ya penzi la baameidi imenishangaza sana. Na kumgharamia baameidi kiasi kile wakati wale ni watu wa kumegwa na kila mtu atakaye ndilo limenishangaza zaidi. Ni mimi tu nimebakia, ni mimi tu kuwaletea habari.
Wasalaam.
umeshakiri ni kazuri na mwenyewe ulikuwa unakasarandia...kwani na wewe c mume wa m2...wale walee tu huna tofauti....mnawatongoza wenyewe mkijua ni baamedi na mnajua wanao wanaume wengi sasa kinachokushangaza hapo ni nini na yote hayo mnayajua? si mnajitakia wenyewe?....halafu penzi ni penzi mnachotakiwa ni kujiheshimu tu nyie wanaume...hakuna cha baamedi, house gal wala cjui kitu gani huko c ndio mnafata hayo mapenzi ya shap shap?....hujabakia lolote kuleta habari wewe mwenyewe wale wale tuu.